Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 12 2020-01-29

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:-

Barabara za Mji Mafinga hazipitiki kwa mwaka mzima na kati ya kilomita 407 kwa mujibu wa DROMAS lami ni kilometa 5.58.

Je, Serikali ipo tayari kuongezea fedha TARURA ili ijenge barabara za kupitika kwa mwaka mzima?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa DROMAS Mji wa Mafinga una Mtandao wa barabara wenye urefu wa kilometa 325.67. Aidha, urefu wa mtandao wa barabara unatarajiwa kuongezeka pindi zoezi la uhakiki wa mtandao wa barabara linaloendelea litakapokamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kutoa fedha kwa ajili ya matengenezo ya barabara za Mji wa Mafinga ili kuhakikisha zinapitika wakati wote na imeongeza bajeti ya matengenezo ya barabara kwa Halmashauri ya Mji wa Mafinga kutoka Shilingi milioni 876.81 mwaka kwa fedha 2017/2018 hadi Shilingi bilioni 1.036 mwaka wa fedha 2019/2020. Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini yaani (TARURA) unakamilisha zoezi la kuhakiki mtandao wa barabara zake na itaweka vipaumbele vya ujenzi na matengenezo ya barabara na madaraja kwa kuzingatia urefu na umuhimu wa barabara husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kupitia formula ya mgao wa fedha za Mfuko wa Babarara ili kuona namna bora ya kuiwezesha TARURA kwa kuiongezea fedha ili iweze kuboresha miundombinu ya barabara na madaraja katika halmashauri mbalimbali nchini, ahsante.