Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y. MHE. DAVID E. SILINDE) aliuliza:- Zoezi la usambazaji wa umeme wa REA katika Wilaya ya Momba bado haujakamilika hadi sasa:- (a) Je, ni lini Serikali itaanza mchakato wa kupeleka umeme katika kata ambazo hazijafikiwa na miradi hiyo katika Jimbo la Momba? (b) Je, ni lini mradi wa kuwasha umeme Tarafa ya Kamsamba utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza, Mheshimiwa Waziri ametaja mkandarasi anayesimamia ujenzi kwenye hivyo vijiji, lakini amekuwa akifanya kazi hii kwa taratibu sana na analalamika kwamba hapewi pesa yake ya kukamilisha kazi zake kwa wakati. Je, Mheshimiwa Waziri uko tayari kutueleza hivi viporo vya REA II vitakamilika lini specifically?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; matatizo yaliyopo Jimbo la Momba kwenye masuala haya ya umeme yanafanana moja kwa moja na shida pia zilizopo kwenye Jimbo la Ndanda, Wilaya ya Masasi, hasa zaidi kwenye Vijiji vya Mkwera, Mumburu, Chipite, Mdenga, Liputu, Ndoro pamoja na Mbaju pamoja na Kata za Msikisi na Mlingula. Vijiji hivyo nilivyovitaja vyote vinapitiwa na umeme mkubwa juu wa kilowati 33 lakini chini wanakokaa wananchi hakuna umeme. Je, ni lini Serikali kwa makusudi kabisa itatekeleza kazi hii ya kushusha umeme walau kwenye vile vijiji vinavyopitiwa na umeme mkubwa unaoelekea Masasi?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kumshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri katika swali la msingi, lakini nimpongeze sana Mheshimiwa Mwambe katika maswali yake mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, ni kweli yapo maeneo yaliyobaki katika utekelezaji wa REA II na maeneo yote yaliyobaki katika utekelezaji wa REA II yamechukuliwa na Mradi wa REA III unaoendelea sasa. Kwa maendeleo yote, hasa katika Jimbo la Mheshimiwa kama alivyotaja, eneo lote la kutoka Sumbawanga kwenda Tunduma kwenda mpaka Mpanda, yaliyobaki yote yamechukuliwa na Mradi wa REA III unaoendelea. Kwa hiyo nimpe tu taarifa Mheshimiwa Mbunge kwa niaba ya muuliza swali kwamba maeneo yote yaliyobaki yatachukuliwa na REA III inayoendelea kufanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na swali la pili, ni kweli kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mwambe; maeneo ya Ndanda, hasa eneo la Liputi pamoja na Mbemba pamoja na Kitongoji cha Ndoro, yako chini ya line inayopita KVA 33, lakini kama ambavyo nimeshatoa utaratibu na Mheshimiwa Mbunge anafahamu, hivi sasa TANESCO wanapeleka umeme katika vitongoji vyote hivyo. Bahati nzuri sana Kitongoji cha Ndoro kiko nyuma ya Sekondari ya Ndanda ambayo tayari ina umeme. Kwa hiyo, maeneo haya yatafanyiwa kazi na yatakamilishwa ifikapo mwisho wa mwezi Juni, mwaka huu.

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y. MHE. DAVID E. SILINDE) aliuliza:- Zoezi la usambazaji wa umeme wa REA katika Wilaya ya Momba bado haujakamilika hadi sasa:- (a) Je, ni lini Serikali itaanza mchakato wa kupeleka umeme katika kata ambazo hazijafikiwa na miradi hiyo katika Jimbo la Momba? (b) Je, ni lini mradi wa kuwasha umeme Tarafa ya Kamsamba utakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kupewa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza nipende tu kuwashukuru Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri, waliweza kufanya ziara katika Jimbo la Mbeya Vijijini na katika ziara hiyo waliahidi kuwa wangepeleka umeme katika Kata za Maendeleo, Itawa na Shizuvi, ikiwa ni pamoja na vijiji vinavyolizunguka Jiji la Mbeya. Sasa je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye Kata za Maendeleo, Itawa na Shizuvi?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oran Njeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tulitembelea Mkoa wa Mbeya, hususan Jiji la Mbeya na si chini ya mara mbili na kuwaahidi wananchi wa Kata za Maendeleo na Kata ambayo ameitaja ya Itawa, kwamba tutawapatia umeme na hususan katika mradi unaoendelea wa ujazilizi awamu ya pili, mzunguko wa kwanza, ambao hatua za manunuzi zimeshakamilika na kiasi cha shilingi bilioni 169 zimetengwa. Mkoa wa Mbeya ni miongoni mwa mikoa tisa ambayo itapata fursa ya ujazilizi awamu ya pili, mzunguko wa kwanza kama ambavyo imepata fursa ya ujazilizi awamu ya kwanza kutokana na mahitaji makubwa. Kwa hiyo nimpongeze Mheshimiwa Mbunge na nimuahidi kwamba maeneo haya yatapatiwa umeme katika mradi ambao utaanza Julai, 2019. Ahsante sana.

Name

Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y. MHE. DAVID E. SILINDE) aliuliza:- Zoezi la usambazaji wa umeme wa REA katika Wilaya ya Momba bado haujakamilika hadi sasa:- (a) Je, ni lini Serikali itaanza mchakato wa kupeleka umeme katika kata ambazo hazijafikiwa na miradi hiyo katika Jimbo la Momba? (b) Je, ni lini mradi wa kuwasha umeme Tarafa ya Kamsamba utakamilika?

Supplementary Question 3

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Serikali katika REA awamu ya pili ilichukua umeme kutoka Mjini Sumbawanga na kupitisha katika jimbo langu kupeleka Mkoa wa Katavi maeneo ya Kibaoni bila kushusha umeme katika Vijiji vya Mbwilo, Mnazi, Kalumbaleza, Mpete, Mtapenda, Mfinga na Kizungu. Je, ni lini Serikali itashusha umeme katika maeneo hayo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Malocha, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze kwa kazi nzuri anayofanya kwenye jimbo lake na yeye mwenyewe anathibitisha tulishafanya ziara pia katika Mkoa wa Rukwa na Jimbo lake zaidi ya mara mbili. Nataka nimwarifu maeneo hayo ambayo ameyataja ambapo umeme ulipita wakati unaelekea Mkoa wa Katavi kwamba tumeshatoa maelekezo maeneo hayo yaingie kwenye REA awamu ya tatu, mzunguko wa pili unaoanza Julai, 2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kama ambavyo Mkandarasi Nakuroi anaendelea na kazi katika Mkoa wa Rukwa na hususan katika jimbo lake na maeneo ambayo tulitembelea pamoja yanaendelea na kazi vizuri na yatawashwa umeme kwa kipindi kinachoendelea. Kwa hiyo kwa maeneo haya na kwa kuwa umeme ulipita na nafurahi leo ninaposimama hapa pia kama ambavyo mnafahamu Rais wa Benki wa Dunia ameshatoa fursa ya mradi wa kusafirisha umeme katika msongo wa KV 400 ambao unaelekea Sumbawanga, Mpanda, Nyakanazi, Kigoma, kwa hiyo kutakuwa na uhakika wa umeme katika maeneo aliyotaja Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y. MHE. DAVID E. SILINDE) aliuliza:- Zoezi la usambazaji wa umeme wa REA katika Wilaya ya Momba bado haujakamilika hadi sasa:- (a) Je, ni lini Serikali itaanza mchakato wa kupeleka umeme katika kata ambazo hazijafikiwa na miradi hiyo katika Jimbo la Momba? (b) Je, ni lini mradi wa kuwasha umeme Tarafa ya Kamsamba utakamilika?

Supplementary Question 4

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nami niulize swali dogo la nyongeza. Kuna kata iko pale inaitwa Kata ya Sirari, kata kubwa kabisa, ina wakazi zaidi ya 45,000, watu wana majumba mpaka ya milioni 200 pale; Kitongoji cha Nyamorege, Niroma, kuna maeneo ya Kimusi, tumezungumza na Waziri muda mrefu sana, watu wanahitaji umeme na wana uwezo wa kulipia. Ni lini hao watu watapata umeme kwenye hayo maeneo niliyoyataja kwa sababu watu wanahitaji umeme na wana nguvu za kulipa?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, ni kweli nilitembelea eneo hilo na kutoa maelekezo na nimshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa sababu anafahamu. Utekelezaji wa kupeleka umeme katika eneo hilo mpakani kabisa na Sirari umeshaanza na Kitongoji anachokisema cha Nyamorege ambacho kiko jirani sana na wilaya moja wapo ya mkoa wa kwanza kutoka Kenya tayari kuna umeme na wakandarasi kupitia kampuni yetu inayopeleka umeme vijijini kule Mara umeshaanza. Tarehe ya kumaliza kazi hiyo, nimwambie Mheshimiwa Mbunge ni tarehe 12 Juni, mwaka huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Ezekiel Magolyo Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y. MHE. DAVID E. SILINDE) aliuliza:- Zoezi la usambazaji wa umeme wa REA katika Wilaya ya Momba bado haujakamilika hadi sasa:- (a) Je, ni lini Serikali itaanza mchakato wa kupeleka umeme katika kata ambazo hazijafikiwa na miradi hiyo katika Jimbo la Momba? (b) Je, ni lini mradi wa kuwasha umeme Tarafa ya Kamsamba utakamilika?

Supplementary Question 5

MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Nimetoka kuongea na rafiki yangu, Mheshimiwa Dkt. Kalemani, hapa lakini nataka awatangazie wananchi wa Msalala. Halmashauri ya Msalala Makao Makuu yake yako Ntobo na wameshahamia, lakini shughuli zote inabidi zifanyikie mjini, kwenda kutoa photocopy, hata shughuli za kibenki au za kiuhasibu kwa sababu ya ukosefu wa umeme. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye Kijiji cha Ntobo yalipo Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kwa dharura?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nijibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Maige, Mbunge wa Msalala, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni kweli, ni kama takribani nusu saa tumemaliza kuongea na Mheshimiwa Mbunge. Kazi ya kupeleka umeme katika Kijiji cha Ntobo ambacho kiko kilometa nane kutoka umeme unapoishia inaanza Jumatatu ijayo na tayari leo wakandarasi wamekwenda ku-survey. Niwape taarifa wananchi wa Msalala, hasa wa Ntobo, kwamba kuanzia wiki ijayo kazi ya kupeleka umeme kwenye kijiji kizima na vitongoji vya Ntobo inaanza Jumatatu wiki ijayo.

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y. MHE. DAVID E. SILINDE) aliuliza:- Zoezi la usambazaji wa umeme wa REA katika Wilaya ya Momba bado haujakamilika hadi sasa:- (a) Je, ni lini Serikali itaanza mchakato wa kupeleka umeme katika kata ambazo hazijafikiwa na miradi hiyo katika Jimbo la Momba? (b) Je, ni lini mradi wa kuwasha umeme Tarafa ya Kamsamba utakamilika?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Moja ya wilaya ambazo zilipata maeneo machache sana mwanzoni ni Wilaya ya Hanang na sasa bado changamoto ni kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri aliniahidi kwamba atatembelea Hanang, mimi nasubiri naomba awaambie wananchi wa Hanang ni lini atakwenda kule ili kuona changamoto zile na tushirikiane naye ili tuweze kuondoa hizo changamoto?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nijibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Mary Nagu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, tarehe 2, mwezi ujao, baada ya bajeti yetu kumalizika tutafuatana mimi na Mheshimiwa Mbunge, twende kwenye jimbo lake.