Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 30 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 246 2019-05-17

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y. MHE. DAVID E. SILINDE) aliuliza:-

Zoezi la usambazaji wa umeme wa REA katika Wilaya ya Momba bado haujakamilika hadi sasa:-

(a) Je, ni lini Serikali itaanza mchakato wa kupeleka umeme katika kata ambazo hazijafikiwa na miradi hiyo katika Jimbo la Momba?

(b) Je, ni lini mradi wa kuwasha umeme Tarafa ya Kamsamba utakamilika?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa David Ernest Silinde, Mbunge wa Momba, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Momba ina jumla ya vijiji 72, kati ya hivyo, Vijiji 13 vya Nkangano, Chiwanda, Isanga, Kakozi, Ndalambo, Chitete, Tindingoma, Ntungwa, Mkonko, Kamsamba, Masanyinta, Itumbula na Mpapa, vimepata umeme kupitia Mradi wa REA II na wateja wa awali 854 wameunganishiwa umeme. Jumla ya Vijiji 15 vya Halmashauri ya Momba vya Nakawale, Ikana, Ivuna, Ipatikana, Muungano, Myunga, Machindo, Mfuto, Isanga, Tindingoma na Kikozi vimepatiwa umeme kupitia Mradi wa REA Awamu ya Tatu mzunguko wa kwanza unaoendelea kutekelezwa na Kampuni ya STEG International Services. Kazi za kupeleka umeme katika vijiji hivi itakamilika ifikapo mwezi Juni, 2020.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi za mradi zinahusisha ujenzi wa kilometa 168 za njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 na kilometa 109 za njia za umeme msongo kilovoti 0.4, kufunga transfoma 37 na kuunganisha wateja wa awali 1,775. Gharama ya mradi ni shilingi bilioni 11.23. Hadi kufikia mwezi Aprili, 2019, mkandarasi ameshafunga transfoma 15 kati ya 21 na kuwasha umeme. Jumla ya wateja wa awali 244 wameunganishiwa umeme. Mkandarasi anaendelea na kazi ya kuvuta waya kufunga transfoma katika Vijiji vya Ipata, Mpui, Msungwe na Kapele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tarafa ya Kamsamba ilipatiwa umeme kupitia Mradi wa REA awamu ya pili ambapo kazi ya kusambaza umeme katika baadhi ya vitongoji vya tarafa hiyo inaendelea chini ya TANESCO kwa bei ya shilingi 27,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi kukamilika kwa Mradi wa REA awamu ya tatu, mzunguko wa kwanza, jumla ya vijiji 24 vitapatiwa umeme katika Halmashauri ya Momba. Vijiji 44 vilivyosalia vitapatiwa umeme katika Mradi wa REA II, mzunguko wa pili unaotarajia kuanza mwezi Julai, 2020.