Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO aliuliza:- Je, Serikali imetenga fedha kiasi gani ya ujenzi wa mabwawa ya maji ili kupunguza matatizo ya maji katika Wilaya ya Kilolo?

Supplementary Question 1

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri alifanya ziara katika Mji wa Ruaha Mbuyuni baada ya kuonekana kuna shida kubwa sana ya maji na kipindupindu kinatokea kila mara na akaahidi pale kwamba kichimbwe kisima kwa tahadhari ili wananchi waanze kupata maji. Lakini kwa masikitiko makubwa wale wataalam wamepuuzwa hakuna aliyefika pale. Sasa Mheshimiwa Naibu Waziri atakubali tena kwenda kuona hali ilivyo na wananchi wanazidi kuteseka?

Swali la pili, kwa kuwa Serikali kuna wahisani ambao huwa wanansaidia Serikali, kuna tatizo kubwa katika Kijiji cha Udekwa na Mlafu, tayari Serikali ya Italy, kupitia Shirika linaitwa WAMAKI liko tayari kusaidia, lakini linataka commitment ya Serikali, yenyewe litasaidia kiasi gani, ili na wao waweze kusaidia fedha. Je, Serikali sasa itakuwa tayari kusaidia ili WAMAKI waweze kutoa maji safi na salama kwa kata mbili.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nikiri kabisa nilifika Kilolo na nimeona kazi nzuri ambayo inafanywa na Mheshimiwa Mbunge Venance Mwamoto katika Jimbo lake. Lakini kikubwa tulifika kweli Ruaha Mbuyuni na tukaona changamoto ile na tukatoa agizo, watu wa Bonde walikwenda walishafanya tafiti ya upatikanaji wa maji. Labda nimuagize sasa Mhandisi wa Mkoa, ahakikishe kabisa kile kisima kinachimbwa ili wananchi wale waweze kupata maji na anipatie taarifa.

Mheshimiwa Spika, lakini kuhusu suala lake la pili, pamoja Serikali imekuwa ikitatua tatizo la maji, imekuwa ikishirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, sisi kama Serikali tupo tayari kukaa nao, tuangalie ni namna gani tunaweza tukashirikiana katika kuhakikisha tunatatua changamoto hii. Ahsante sana.