Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 26 Water and Irrigation Wizara ya Maji 215 2019-05-13

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO aliuliza:-

Je, Serikali imetenga fedha kiasi gani ya ujenzi wa mabwawa ya maji ili kupunguza matatizo ya maji katika Wilaya ya Kilolo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Venance Mwamoto, Mbunge wa Jimbo la Kilolo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Halmashauri ya Kilolo kw aupande wa Vijijini ni asilimia 71. Kilolo Mjini ni asilimia 80 na Ilula ni asilimia 47.5. Aidha, halmashauri ya Wilaya ya Kilolo imekamilisha ujen zi wa miradi ya vijiji 10 kupitia Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji pamoja na Ujenzi wa vijiji vitano kupitia ufadhili wa Taasisi isiyo ya Kiserikali ya WARIDI.

Mheshimiwa Spika, kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019, Halm ashauri ya Wilaya ya kilolo inatekeleza miradi ya maji katika vijiji vitatu vya Lundamatwe, Kitelewasi na Ilambo. Pia miradi miwili katika miji midogo ya Kilolo na Ilula. Aidha, Halmashauri ya Kilolo kwa kutumia fedha za ndani inakarabati mabwawa matatu yaliyopo katika vijiji vya Uhambingeto, Image na Mgowelo kwa ajili ya binadamu na mifugo.

Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na channgamoto ya uhaba wa maji kwa mwaka huu wa fedha 2018/2019 Halmashauri ya Kilolo imepokea jumla ya shilingi bilioni 1.7 ili kuhakikisha miradi ya maji inatekelezwa na kukamilika na kuwapunguzia keri ya maji wananchi wa wilaya hiyo.