Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:- Je, ni lini Serikali italeta fedha za on call allowance kwa madaktari wanaofanya zamu hasa katika hospitali za Wilaya na vituo vya afya ambavyo mapato yake ni madogo kwani sasa ni zaidi ya miaka miwili fedha hiyo haijaletwa na Serikali?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza niipongeze Serikali kwa kuweza kudhibiti mianya ya upotevu wa fedha ya Serikali. Lakini Mheshimiwa Waziri pamoja na kwamba mmeelekeza ile asilimia 15 ya mapato kutoka kwenye hospitali na vituo vya afya ziende kulipa on call allowance kwa madaktari hawa, lakini bado kuna changamoto kwa sababu kuna halmashauri ambazo ni nyingi zina mapato madogo sana.

Sasa je, nyie kama Wizara mmejipangaje kuhakikisha kwamba zile halmashauri ambazo mapato yake ni madogo mtumie njia gani nyingine ambayo itakuwa muafaka ili kuweza kuhakikisha kwamba madaktari hawa wanapata stahiki zao?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kwa kuwa bado kumekuwa na changamoto za kupandishwa vyeo kwa mfano kutoka clinical officer kwenda kuwa daktari lakini vile vile kutoka mkunga kwenda kuwa muuguzi na vile vile promotion zao bado tumeziona zikiwa zina suasua. Je, nyie kama Wizara mmejipanga vipi kuhakikisha kwamba mnatatua changamoto hii pia?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, kwanza naomba uniruhusu kipekee nitumie fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Neema, amekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kwamba wananchi wa Mkoa wa Njombe wanapata huduma nzuri ya afya. Binafsi ameonekana akichangia mifuko ya saruji lakini pia nikimuona amepeleka mashuka kwa ajili ya kusaidia wagonjwa wetu.

Mheshimiwa Spika, baada ya pongezi hizo, katika swali lake la kwanza anaongelea namna ambavyo uwezekano mdogo kwa baadhi ya halmashauri. Kwanza katika kuimarisha tumeajiri wahasibu zaidi ya 350 ambao katika vituo vya afya wameenda kusimamia na mapato yameongezeka. Hakika fedha hii ikiweza kusimamiwa vizuri hakuna uwezekano wa kwamba madaktari na wauguzi wanaweza wasilipwe on call allowance. Nilienda kituo cha afya Kisosora pale Tanga nimekuta katika fedha ambazo zinapatikana mpaka wanafanya na ukarabati katika vituo vya afya. Kwa hiyo, ni suala tu la kusimamia vizuri na hakika maeneo yote ambayo yanasimamiwa vizuri, fedha inatosha na hatujapata malalamiko hivi karibuni.

Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili anaongelea suala zima la kuwapandisha vyeo. Hizi n afasi zinategemeana na ujuzi kwa hiyo si rahisi kwamba mtu atapanda bila kwenda kuongeza ujuzi na ni matarajio ya Mheshimiwa Mbunge kwamba asingependa akapandishwa cheo mtu ambaye hana ujuzi mahsusi na ndiyo maana zimekuwa zikitolewa fursa za wao kujiendeleza na pale anapojiendeleza na kuhitimu akirudi huwa anapandishwa cheo.