Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 26 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 212 2019-05-13

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali italeta fedha za on call allowance kwa madaktari wanaofanya zamu hasa katika hospitali za Wilaya na vituo vya afya ambavyo mapato yake ni madogo kwani sasa ni zaidi ya miaka miwili fedha hiyo haijaletwa na Serikali?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema William Mgaya, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, hapo awali Serikali iliweka utaratibu wa kulipa fedha za on call allowance kupitia Hazina, ambapo halmashauri ziliwasilisha orodha za madaktari na wataalamu wote wanaostahili kulipwa fedha za on call allowance. Ofisi ya Rais TAMISEMI ambayo hupeleka madai hayo Wizara ya Fedha na Mpipango. Hata hivyo utaratibu huo ulipelekea baadhi ya wataalam wasiyo waaminifu kutoa taarifa ambazo siyo sahihi na hivyo kusababisha madeni makubwa kwa Serikali.

Mheshimiwa Spika, ili kuondokana na hali ya kuwa na madeni makubwa yasiyo na uhalisia, halmashauri zilielekezwa utaratibu wa kuweka fedha za on call allowance kwenye mipango na bajeti zao ili kuweza kulipa stahiki hizi. Pamoja na kuweka fedha za on call allowance kwenye mipango na bajeti, ilibainika kuwa zipo halmashauri zenye uwezo mdogo wa kimapato hivyo maelekezo yaliyotolewa hospitali na vituo vya afya kutenga asilimia 15 kutoka kwenye mapato yatokanayo na uchangiaji wa huduma za afya kwa ajili ya kulipa motisha kwa wataalam ikiwa ni pamoja na on call allowance.