Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:- Kwa muda mrefu tumepigania kuboreshwa kwa maslahi ya Madiwani ikiwepo posho za vikao na Serikali imekuwa ikisisitiza kuongeza mapato ili halmashauri ziweze kuwalipa Madiwani vizuri kadri ya uwezo, wito ambao umeitikiwa vizuri, mwezi Februari, 2019 tumepokea barua toka TAMISEMI ikielekeza Madiwani walipwe posho za vikao shilingi 40,000 na si vinginevyo. Je, kwa nini Serikali isiache halmashauri kulipa posho kadri ya uwezo kama ambavyo msisitizo umekuwa toka awali?

Supplementary Question 1

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana na nashukuru kwa majibu ya Serikali. Nina maswali mawili ya nyongeza, kwanza fursa za vyanzo vya mapato na uwezekano wa kuongeza mapato inatofautiana baina ya halmashauri na halmashauri. Hili suala la malalamiko lina kosa msingi linabaki kuwa dhana.

Sasa je, Serikali huwezi kulinganisha kati ya Kondoa au Geita au hata Dar es Salaam fursa za mapato zilizopo, na Madiwani ni sehemu ya wanaoweka nguvu ya kukusanya mapato na kuongeza mapato. Serikali haioni umuhimu wa kuwaruhusu walipe kadiri ya uwezo wa halmashauri zao ili pia iwe sehemu ya motisha?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, lini sasa maana tulipata Waraka wa kutuambia tulipe 40,000 na hapa tunazungumzia posho za vikao peke yake, lini sasa maslahi mengine tunaendelea kuruhusu kadiri ambavyo inafanya kazi. Lini sasa tutapata Waraka wa kufafanua ili ule Waraka uliotolewa mwezi Januari uweze kupitwa maana Serikali inafanya kazi kwa maandishi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Waheshimiwa Madiwani wanafanya kazi kubwa sana ya kusimamia mapato, kwa kukusanya lakini pia na ndiyo maana fedha nyingi hapa tunapeleka halmashauri Waheshimiwa Madini kupitia vikao vyao na Kamati mbalimbali ndiyo wanapaswa kusimamia na kwa kweli tunawashukuru sana wamekuwa wakifanya hivyo. Majibu yangu ni kwamba ni kweli Mheshimiwa Waziri wa Nchi wakati anamalizia hoja yetu hii ya bajeti ya TAMISEMI, aliahidi mbele ya Bunge lako Tukufu kwamba jambo hili linafanyiwa kazi na naomba niwaahidi kwamba, Waheshimiwa Wabunge wote na Waheshimiwa Madiwani popote walipo wavute subira ndani ya wiki hii Mheshimiwa Waziri atatoa maelekezo na jambo hili litafikia mwisho ambapo tunaamini kwamba utakuwa ni mwisho mwema, ahsante.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:- Kwa muda mrefu tumepigania kuboreshwa kwa maslahi ya Madiwani ikiwepo posho za vikao na Serikali imekuwa ikisisitiza kuongeza mapato ili halmashauri ziweze kuwalipa Madiwani vizuri kadri ya uwezo, wito ambao umeitikiwa vizuri, mwezi Februari, 2019 tumepokea barua toka TAMISEMI ikielekeza Madiwani walipwe posho za vikao shilingi 40,000 na si vinginevyo. Je, kwa nini Serikali isiache halmashauri kulipa posho kadri ya uwezo kama ambavyo msisitizo umekuwa toka awali?

Supplementary Question 2

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, suala linaloulizwa na Mheshimwa Sannda na sisi pia watu wa halmashauri ya Masasi linatuletea shida. Halmashauri ya Wilaya ya Masasi ilipanga kulipa posho Madiwani na stahiki zao nyingine kutokana na makusanya yaliyokuwa yanakusanywa kutoka kwenye ushuru wa korosho ambao Mheshimiwa Rais amesema hatapeleka tena. Sasa swali langu, ni je, Serikali haioni umuhimu wa kuwalipa Madiwani hawa posho moja kwa moja kutoka kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimeeleza kwenye majibu yangu ya msingi kwamba suala la posho za Madiwani, kwanza kimsingi yanatokana na mapato ya ndani na suala lingine ni uwezo wa halmashauri yenyewe na Mheshimiwa Rais alishatoa maelekezo kwa Wilaya hizi ambazo zilikuwa zinakusanya mapato kupitia korosho wajipange kwa msimu mwingine wa korosho wafanye kazi vizuri ili waweze kupata mapato hayo. Sisi maelekezo yetu ni kwamba tutatoa maelekezo na halmashauri italipa Madiwani kulinga na uwezo wao wa ndani, ahsante.

Name

Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:- Kwa muda mrefu tumepigania kuboreshwa kwa maslahi ya Madiwani ikiwepo posho za vikao na Serikali imekuwa ikisisitiza kuongeza mapato ili halmashauri ziweze kuwalipa Madiwani vizuri kadri ya uwezo, wito ambao umeitikiwa vizuri, mwezi Februari, 2019 tumepokea barua toka TAMISEMI ikielekeza Madiwani walipwe posho za vikao shilingi 40,000 na si vinginevyo. Je, kwa nini Serikali isiache halmashauri kulipa posho kadri ya uwezo kama ambavyo msisitizo umekuwa toka awali?

Supplementary Question 3

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa halmashauri ambazo zinalima korosho maamuzi yanayohusiana na ununuzi wa korosho ndiyo yaliyopelekea wao kupoteza mapato. Kuna halmashauri ambazo makusanyo yake sasa hivi ni 6% tu kwa sababu fedha zake zote walikuwa wanategemea korosho, Serikali haioni ni busara kufanya compensation ya fedha hizi ili halmashauri hizi ziweze kuendelea na shughuli zao kama kawaida ikiwemo kuwalipa Madiwani?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, nadhani jambo hili kila halmashauri inapanga mipango yao na kilichofanyika na Serikali ni kwamba ilikuwa ni lazima tuchukue hatua kuwawezesha watu wetu waweze kuuza korosho zao, lakini halmashauri zenyewe maelekezo ya Serikali ni kwamba kwa kuwa hiki kilikuwa ni kipindi cha mpito tunaamini kwamba msimu ujao watajipanga vizuri waweze kukusanya kwa kuzingatia Sheria na miongozo yao. Kwa sasa suala la compensation halitakuwepo kwa sababu hiyo bajeti hatuna, ahsante.