Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 26 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 210 2019-05-13

Name

Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:-

Kwa muda mrefu tumepigania kuboreshwa kwa maslahi ya Madiwani ikiwepo posho za vikao na Serikali imekuwa ikisisitiza kuongeza mapato ili halmashauri ziweze kuwalipa Madiwani vizuri kadri ya uwezo, wito ambao umeitikiwa vizuri, mwezi Februari, 2019 tumepokea barua toka TAMISEMI ikielekeza Madiwani walipwe posho za vikao shilingi 40,000 na si vinginevyo.

Je, kwa nini Serikali isiache halmashauri kulipa posho kadri ya uwezo kama ambavyo msisitizo umekuwa toka awali?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Edwin Mgante Sannda, Mbunge wa Kondoa Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli Serikali imetoa ufafanuzi kupitia barua Kumb. Na. CCB. 215/443/01 ya tarehe 02 Januari, 2019 juu ya ulipaji wa posho mbalimbali za Madiwani ikiwemo posho za kuhudhuria vikao. Sheria ya Serikali za Mitaa Sura Namba 288 Kifungu cha 42 na Sura ya 287 Kifungu cha 70, inamtaka Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa kupitisha viwango vya posho za Madiwani. Hivyo posho hizo zinapaswa kulipwa kwa kuzingatia miongozo na maelekezo ya Waziri mwenye dhamana wa Serikali za Mitaa. Maelekezo yanayotolewa yanasaidia kuweka usawa wa viwango vya posho za Madiwani katika halmashauri zetu nchini, hivyo kuondoa malalamiko kutoka wa Waheshimiwa Madiwani.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuimarisha mifumo ya ukusanyaji na udhibiti wa mapato na itendelea kuongeza posho na maslahi ya Madiwani kulingana na kuimarika kwa uwezo wa halmashauri kwa kukusanya mapato yake ya ndani.