Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakarabati Shule ya Sekondari ya Mpanda Girls?

Supplementary Question 1

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Shule hii ni kongwe halafu iko kwenye eneo ambalo ni hatarishi, kuna bwawa ambalo lina wanyama wakali ambao wanaingia katika eneo la shule kwa sababu shule hii haina uzio kabisa; na shule hii ina upungufu mkubwa sana wa madarasa na vilevile ina upungufu wa mabweni; na kwa kuwa Serikali imepanga fedha na imesema hapa kuwa imeji-commit na pesa tayari zipo; sasa naomba commitment, ni lini Serikali itakarabati shule hii kwa sababu wanafunzi wa shule hii wanapata taabu sana?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, shule hii ina wasichana takribani watoto 888, ni watoto wa kike ambao wanapata shida sana; usiku wakiugua hakuna gari katika shule hii: kwa kuwa hii shule ni kongwe, ni lini Serikali itatuletea gari katika shule hii ya Sekondari ya Mpanda Girls?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi ni kwamba zimetengwa fedha shilingi bilioni 16 kwa ajili ya kukarabati shule nyingine mwaka huu wa fedha na commitment ya Serikali ni kwamba ukarabati huu unaanza mara tu tutakapoanza kutekeleza bajeti ya mwaka 2019/ 2020.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ametoa hoja ya gari na ni kweli kwamba kwa shule hizi kongwe na kutokana na mazingira ambayo ameyataja Mheshimiwa Mbunge, naomba tupokee ombi hili tutalifanyia kazi kwa kadri uwezo wa Serikali utapopatikana.

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakarabati Shule ya Sekondari ya Mpanda Girls?

Supplementary Question 2

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, nikirejea hapo katika Shule ya Wasichana ya Mpanda kimechimbwa kisima kirefu, tatizo lililobaki ni ufungaji wa pump na ukizingatia ni shule ambayo ina watoto wa kike peke yake.

Ni lini Serikali itakamilisha suala la ufungaji wa pump kwenye shule hii?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Tunapokarabati hizi shule kwanza tunaangalia mfumo wa majengo, mabweni, bwalo, madarsa, Ofisi, majengo ya utawala, mfumo pia wa maji na mfumo wa umeme. Kwa hiyo, kama alivyozungumza kwamba kuna kisima ambacho kimechimbwa katika eneo hilo, wakati wa ukarabati litaangaliwa. Tutatenga fedha kwa ajili ya kupata maji katika eneo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huwezi kuwa na wanafunzi wengi katika shule hii kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge kwamba ni zaidi ya wanafunzi 800, watoto wa kike, halafu kusiwe na huduma ya maji. Ahsante.

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakarabati Shule ya Sekondari ya Mpanda Girls?

Supplementary Question 3

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa matatizo ya ukarabati katika shule za sekondari yanafanana na shule za msingi, Mkoa wa Tabora katika Manispaa ya Tabora, Shule ya Kanyenye iliezuliwa karibuni madarasa manne tangu mwaka 2018 Machi, mpaka leo haijafanyiwa ukarabati, wanafunzi wanapata taabu. Nini kauli ya Serikali kwa leo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba nipokee maombi na maelekezo ya Mheshimiwa Mbunge tutayafanyia kazi. Mpaka Bunge lijalo tutakuwa tumepata majibu ya tatizo hili katika eneo la Tabora. Ahsante.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakarabati Shule ya Sekondari ya Mpanda Girls?

Supplementary Question 4

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Shule ya wasichana ya Tabora (Tabora Girls) ni shule kongwe sana hapa nchini ambayo pia ina vipaji maalumu. Shule hii kwa muda mrefu imetelekezwa kuhusu uzio. Ile shule haina uzio kabisa kwa miaka mingi na tayari juhudi za viongozi mbalimbali nikiwemo mimi mwenyewe tumeshaanza mkakati wa kujenga uzio huo.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kutusaidia katika kukamilisha uzio huo wa Shule ya Wasichana Tabora?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, nakushukuru. Namwomba Mheshimiwa Mbunge tuonane tuone. Kama wananchi wameanza kujitolea na wadau mbalimbali akiwepo Mheshimiwa Mbunge kwa kazi nzuri ya wananchi wake anaowawakilisha hapa Bungeni, basi tuonane tuone ni changamoto gani zilizopo na sehemu gani ya kuweza kusaidia kumalizia uzio huo.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakarabati Shule ya Sekondari ya Mpanda Girls?

Supplementary Question 5

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi nami naulize swali dogo la nyongeza. Katika jitihada za kuboresha miundombinu ya elimu Mkoani Lindi, kwa misimu miwili, mitatu iliyopita tulikubaliana kukata fedha kutokana na malipo ya korosho ya shilingi 30/= kwa kila kilo ili kukarabati miundombinu na kujenga miundombinu mipya. Sasa iko miundombninu ambayo ilianza kujengwa kwa sababu ya hali ambayo sote tunaijua, miundombinu hiyo sasa imesimama kwa sababu hiyo fedha haikupatikana.

Je, Serikali iko tayari kusaidia kumalizia miundombinu hii katika Mkoa wa Lindi hasa upande wa elimu?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, ni nia ya Serikali kuendelea kukamilisha miundombinu ya elimu na hasa ile ambayo imeanzishwa na wananchi na ndiyo maana tumepeleka fedha za kiutawala mwezi Januari, tumepeleka fedha za maboma karibu shilingi bilioni 29.9. Kwenye bajeti hii ambayo imepitishwa, zaidi ya shilingi bilioni 90 inaenda kusimamia miundombinu ya elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nipokee maombi ya Mheshimiwa Mbunge, tutazingatia maoni yake. Ahsante.