Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 18 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 146 2019-04-30

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakarabati Shule ya Sekondari ya Mpanda Girls?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anna Richard Lupembe, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kufanya ukarabati wa Shule za Sekondari Kongwe nchini kwa awamu kulingana na hali ya upatikanaji wa fedha. Katika Awamu ya kwanza, Serikali imekarabati shule za sekondari 53 kwa gharama ya shilingi bilioni 53.6 ikijumuisha ujenzi wa Shule za Sekondari za Nyakato na Ihungo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Awamu ya pili Serikali imepanga kukarabati shule 17 kongwe za Sekondari nchini ikiwemo Shule ya Sekondari ya Wasichana Mpanda. Jumla ya shilingi bilioni 16 zimetengwa kukarabati shule hizo. Miongoni mwa fedha hizo shilingi milioni 986 zimetengwa kwa ajili ya Shule ya Wasichana ya Mpanda. Ahsante.