Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

John John Mnyika

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. JOHN J. MNYIKA aliuliza:- Tarehe 4 Februari Serikali ikijibu hoja binafsi kuhusu upatikanaji wa maji iliahidi kuwa ifikapo mwaka 2016 matatizo ya maji yangekuwa yamemalizika katika Jiji la Dar es Salaam:- (a) Je, ni kwa nini ahadi hiyo haijatekelezwa kwa wakati? (b) Je, ni Mitaa ipi katika Jimbo la Kibamba maji hayatoki na ni lini DAWASA itahakikisha maji yanatoka katika maeneo hayo? (c) Je, Serikali iko tayari kuwasilisha katika kila Mkutano wa Bunge Taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maji nchini kama ilivyokubali katika Bunge la Kumi?

Supplementary Question 1

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, katika majibu yake, Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba asilimia 80 ya wananchi wa Kibamba wanapata maji ya bomba, jambo ambalo ni taarifa ya uongo imetolewa Bungeni. Kwa sababu ukiangalia mtandao wa maji ulivyo, kuna maeneo mengi hayana kabisa mabomba ya maji na hata yenye mabomba ya maji, bado kuna maeneo ambayo hayatoi maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikitoa mfano, kuna kata sita tu Jimbo la Kibamba; Kata ya Goba, Mitaa ya Goba, Matosa, Tegeta A, na kadhalika. Pamoja na Mheshimiwa Waziri kuahidi kwamba Februari maji yatatoka, lakini hayatoki; Kata ya Mbezi, Mitaa ya Mbezi Luisi, Makabe, Msakuzi hakuna kabisa mabomba; Makabe mabomba yapo lakini maji hayatoki; Fijimagohe na Msumi hakuna mambomba; Kata ya Kibamba kule Hondogo, Kibwegere, hakuna mtandao wa maji wa kuwezesha maji kutoka; Kata ya Kwembe, Kinazi B na mitaa mingine kwa ujumla; Kata ya Msigani, maeneo ya Msingwa, maeneo ya Malamba na maeneo mengine yote yale.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri ametoa jibu la Uongo Bungeni, sasa je, yuko tayari kutoa Takwimu ya ukweli ya hali halisi ya upatikanaji wa maji Jimbo la Kibamba na orodha mtaa kwa mtaa ya upatikanaji wa maji na hatua za utekelezaji? Hilo swali la kwanza.

Swali la pili, siku chache zilizopita, Mheshimiwa Rais akiwa ziarani, amesema kwamba Wizara ya Maji ni kati ya Wizara ambayo ina ma-Engineers wana-perform ovyo ovyo. Kuna miradi mingi ya maji kwa assessment ya Wizara ya Maji ambayo ni miradi hewa, badala ya kutoka maji, inatoka hewa. Sasa kwa kuwa Mheshimiwa Rais ameshatoa hiyo kauli na naamini kauli ya Rais ni agizo:-

Je, Wizara ya Maji iko tayari kuleta Bungeni taarifa ya assessment ya Wizara ya Fedha aliyoisema Mheshimiwa Rais ili tupitie hatua kwa hatua, tuchukue hatua juu ya miradi hewa katika maeneo mbalimbali nchini?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote napenda nimhakikishie kaka yangu Mheshimiwa Mnyika, Serikali imefanya kazi kubwa sana, naye anafahamu kabisa. Kipindi cha nyuma kulikuwa kuna mgao mkubwa sana, lakini sasa hivi kuna utekelezaji zaidi ya asilimia 85 ya upatikanaji wa maji katika Jiji la Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mnyika anasema taarifa tuliyoisema ni ya uongo. Nisome swali lake kipengele cha (b), anataka kujua ni mitaa ipi katika Jimbo la Kibamba maji hayatoki. Sasa kama Mbunge mitaa yako hujui ipi inayopata maji, unawezaje kuniuliza mimi Mheshimiwa Waziri?

Mheshimiwa Naibu Spika, labda kwa ushauri mdogo tu, nimshauri kaka yangu, afanye ziara katika Jimbo lake, aone kazi kubwa inayofanywa na Serikali. Aende Hodongo aone utekelezaji wa mradi unaofanyika, aende katika katika Kata ya Matosa aone utekelezaji wa miradi unavyofanyika. Nami niko tayari kuongozana naye nikamwonyeshe kazi nzuri inayofanywa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimhakikishie, anayelala na mgonjwa ndio unayejua mihemo ya mgonjwa. Namshauri aende Jimboni na afanye ziara aone kazi kubwa inayofanyikwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusu swali la pili, tunatambua kabisa baadhi ya utekelezaji wa miradi ya maji imekuwa ya kusuasua. Sisi kama Wizara ya Maji tumekuwa tukichukua hatua kwa Wahandisi wababaishaji, lakini pia tumeanzisha Wakala wa Maji Vijijini. Nataka niwahakikishie, tumejipanga vizuri katika kuhakikisha tunatatua tatizo la maji. Wahandisi wote wababaishaji hawana nafasi katika Wizara ya Maji, tumejipanga katika kuhakikisha Wakalaa huu unaenda kutatua tatizo la maji vijijini. Ahsante sana.

Name

Hassan Elias Masala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. JOHN J. MNYIKA aliuliza:- Tarehe 4 Februari Serikali ikijibu hoja binafsi kuhusu upatikanaji wa maji iliahidi kuwa ifikapo mwaka 2016 matatizo ya maji yangekuwa yamemalizika katika Jiji la Dar es Salaam:- (a) Je, ni kwa nini ahadi hiyo haijatekelezwa kwa wakati? (b) Je, ni Mitaa ipi katika Jimbo la Kibamba maji hayatoki na ni lini DAWASA itahakikisha maji yanatoka katika maeneo hayo? (c) Je, Serikali iko tayari kuwasilisha katika kila Mkutano wa Bunge Taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maji nchini kama ilivyokubali katika Bunge la Kumi?

Supplementary Question 2

MHE. HASSAN E. MASALA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Maeneo ya Mji wa Nachingwea katika Kata za Namatula, Nangwe, Mteruka, pamoja na Kilimanihewa yamekuwa yanapata maji kwa kusuasua sana, lakini wakati huo huo tuna chanzo kikubwa cha maji kinachotokana na chanzo cha maji ya Mbwinji.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujua mpango wa Serikali juu ya kutoa fedha ili kuweza kufanya utanuzi wa kusambaza maji katika maeneo ambayo nimeyataja.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nampongeza Mheshimiwa Mbunge. Nimepata nafasi ya kutembelea katika Jimbo lake, lakini kiukweli katika kuhakikisha tunatatua tatizo la maji, lazima tuangalie namna gani tunaweza tukatumia kile chanzo kikubwa cha Mbwinji. Sisi kama Wizara ya Maji tuko tayari na tumejipanga katika kuhakikisha tunatafuta fedha ili tuweze kutumia chanzo kile cha maji ili wananchi wake waweze kupata maji safi, salama na yenye kuwatosheleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Joseph Osmund Mbilinyi

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. JOHN J. MNYIKA aliuliza:- Tarehe 4 Februari Serikali ikijibu hoja binafsi kuhusu upatikanaji wa maji iliahidi kuwa ifikapo mwaka 2016 matatizo ya maji yangekuwa yamemalizika katika Jiji la Dar es Salaam:- (a) Je, ni kwa nini ahadi hiyo haijatekelezwa kwa wakati? (b) Je, ni Mitaa ipi katika Jimbo la Kibamba maji hayatoki na ni lini DAWASA itahakikisha maji yanatoka katika maeneo hayo? (c) Je, Serikali iko tayari kuwasilisha katika kila Mkutano wa Bunge Taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maji nchini kama ilivyokubali katika Bunge la Kumi?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Tatizo la maji la Jiji la Dar es Salaam linafanana kabisa na tatizo la maji la Jiji la Mbeya. Katika Jiji la Mbeya, wataalam wameshasema, solution ya tatizo ni kutoa maji kutoka mto Kiwira, feasibility study imeshafanyika, taarifa tunazo na mto Kiwira hauko mbali, ni kilomita chache sana kutoka Mbeya. Naamini Mheshimiwa Waziri anajua hata bajeti inayotakiwa kutokana na ile feasibility study.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ni lini fedha itapelekwa katika ile project ili ile project ifanyike tuondoe tatizo la maji kwenye maeneo ya Uyole, Mwakibete na hususan maeneo kama Shewa ambako wananchi wanapata taabu sana na wako Jijini, wanalipa kodi za Jiji.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, nikubaliane na Mheshimiwa Mbunge wa Jiji la Mbeya, kaka yangu Sugu, amezungumza suala la msingi sana. Kweli tunatambua kabisa katika suala zima la maji katika Jiji la Mbeya kumekuwa na ongezeko kubwa sana la watu, lakini tunaona kabisa tukiyatoa maji mto Kiwira na kuyaleta tutakuwa tumetatua kabisa tatizo la maji. Nataka nimhakikishie kwamba utekelezaji wa miradi ya maji unategemeana na fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kama Wizara ya Maji tumejipanga katika kuhakikisha kupitia mapato yetu ya ndani lakini pia kwa wafadhili mbalimbali tupate fedha ili tuwekeze na wananchi wa Mbeya waondokane na tatizo hili la maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Halima Abdallah Bulembo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOHN J. MNYIKA aliuliza:- Tarehe 4 Februari Serikali ikijibu hoja binafsi kuhusu upatikanaji wa maji iliahidi kuwa ifikapo mwaka 2016 matatizo ya maji yangekuwa yamemalizika katika Jiji la Dar es Salaam:- (a) Je, ni kwa nini ahadi hiyo haijatekelezwa kwa wakati? (b) Je, ni Mitaa ipi katika Jimbo la Kibamba maji hayatoki na ni lini DAWASA itahakikisha maji yanatoka katika maeneo hayo? (c) Je, Serikali iko tayari kuwasilisha katika kila Mkutano wa Bunge Taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maji nchini kama ilivyokubali katika Bunge la Kumi?

Supplementary Question 4

MHE. HALIMA A. BULEMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na jitihada kubwa zinazofanywa na Wizara ya Maji kuhakikisha inawafikishia wananchi wote maji Tanzania, lakini kumekuwa na kero kubwa na mbaya zaidi kutoka Wizara ya Maji ya kubambikia wananchi bili.

Je, ni lini Wizara hii itaweka mkakati wa kutatua kero hii kwa wananchi?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni haki ya mwananchi kupatiwa maji, lakini pamoja na haki hiyo ya kupatiwa maji, mwanachi naye ana wajibu wa kulipia bili za maji, lakini siyo kulipia tu, anatakiwa alipie bili za maji ambazo siyo bambikizi. Sisi kama viongozi wa Wizara tumeshawaita Wakurugenzi wote wa Mamlaka za Maji na tukawapa agizo na kuwaandikia hadi mkataba, kwa maana ya kuhakikisha kwamba hili tatizo wanaliondoa kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, mkataba ambao tumekubaliana ni katika kuhakikisha Mamlaka zote tunatoka sasa katika mfumo wa zamani tuwe katika pre-paid meter. Nataka nitumie nafasi hii tena kuwaagiza kuanzisha suala zima la pre-paid meter katika kuhakikisha tunaondokana na malalamiko haya ili kuhakikisha kwamba wananchi wanalipia maji kadri wanavyotumia.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.