Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 5 Water and Irrigation Wizara ya Maji 40 2019-04-08

Name

John John Mnyika

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. JOHN J. MNYIKA aliuliza:-

Tarehe 4 Februari Serikali ikijibu hoja binafsi kuhusu upatikanaji wa maji iliahidi kuwa ifikapo mwaka 2016 matatizo ya maji yangekuwa yamemalizika katika Jiji la Dar es Salaam:-

(a) Je, ni kwa nini ahadi hiyo haijatekelezwa kwa wakati?

(b) Je, ni Mitaa ipi katika Jimbo la Kibamba maji hayatoki na ni lini DAWASA itahakikisha maji yanatoka katika maeneo hayo?

(c) Je, Serikali iko tayari kuwasilisha katika kila Mkutano wa Bunge Taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maji nchini kama ilivyokubali katika Bunge la Kumi?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa John Myika, Mbunge wa Jimbo la Kibamba, lenye sehemu (a), (b) na (c) kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo mengi ya Jiji la Dar es Salaam yanapata maji kama Serikali ilivyoahidi kupitia Bunge lako Tukufu baada ya kukamilisha miradi mikubwa ya maji ambayo ilikamilika mwaka 2016. Serikali inatambua kuna baadhi ya maeneo ya jiji hilo hayajapata maji kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ongezeko la watu na ukuaji wa Jiji la Dar es Salaam pamoja na upatikanaji wa maeneo ya kupitisha miundombinu ya miradi.

Mheshimiwa Naibu Spika, asilimia 80 ya wakazi wa Jimbo la Kibamba wanapata huduma ya maji. Maeneo ambayo hayapati maji kwa sasa ni maeneo ambayo yapo kwenye miinuko mikubwa. Ili kuhakikisha wananchi wote wa Jimbo la Kibamba wanapata maji, hasa wanaoishi katika miinuko mikubwa, Serikali inaendelea na ujenzi wa matenki katika eneo la Msakuzi Kusini na Maramba Mawili Juu kwa lengo la kuhakikisha wananchi wote wa Jimbo hilo wanapata huduma ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa miradi Kiti kilishalitolea mwongozo suala hili katika Mkutano wa Pili, Kikao cha Tisa kilichofanyika tarehe 5 Februari, 2016. Katika mwongozo wa Kiti ilielekezwa kama ifuatavyo; naomba kunukuu; “Bunge la Kumi na Moja litakuwa linaweka utaratibu wake wa namna bora kufikisha maelezo kwa Waheshimiwa Wabunge kwa nyakati tofauti.”

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.