Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE.DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Katika Ilani ya CCM kuhusu huduma za afya nchini ni kujenga zahanati katika vijiji na kituo cha afya katika kila kata; kwa sasa Jimbo la Igunga lina vituo vya afya viwili tu katika kata 2 kati ya 17 na zahanati kwenye vijiji 19 tu kati ya vijiji 68:- (a) Je, ni lini Serikali itajenga vituo vya afya kwenye kata 15 zilizosalia? (b) Je, ni lini Serikali itajenga zahanati kwenye vijiji 49 vilivyosalia?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Pia naishukuru Serikali kwa kutuletea fedha kwa ajili ya kujenga vituo vya afya viwili. Pamoja na majibu hayo, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa Ilani ya Chama cha Mapinduzi inaelekeza kwamba tujenge zahanati kila kijiji na Wilaya ya Igunga na Jimbo la Igunga mahsusi kuna vijiji ambavyo zahanati zimejengwa zikakamilika zaidi ya vijiji 10 kikiwepo Kijiji cha Kagongwa, Mgongolo, Makomelo, Chagana, Imalanguzu, Mwamakona na vijiji vingine. Ni lini Serikali itakwenda kukamilisha yale yaliyobaki pia kuleta watumishi ili zahanati hizo ziweze kuanza kufanya kazi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Wilaya ya Igunga pamoja na Jimbo la Igunga na nchi nzima kwa ujumla wananchi walijenga maboma mengi sana ya zahanati ili kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi lakini mpaka sasa hivi maboma hayo yapo tu na tumeomba sana tangu mwaka juzi Serikali itusaidie maboma haya yakamilike ili zahanati zianze kutumika kwa wananchi wetu katika vijiji vyetu. Je, ni lini Serikali itakamilisha maboma hayo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Dkt. Dalaly Peter Kafumu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Mheshimiwa Dkt. Kafumu ameshatoa taarifa hii katika Ofisi ya Rais - TAMISEMI na ukilinganisha Igunga na maeneo mengine pia kuna maboma na zahanati nyingi ambazo zimekwishafanyiwa kazi. Tumeshaomba kibali kwa Mheshimiwa Waziri wa Nchi (Utumishi) ili tupate kibali cha kupata watumishi na wataalamu wa tiba katika maeneo haya ili waweze kutoa huduma. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Mbunge aendelee kuvumilia, tukipata kibali hicho na kadri fedha zitakavyopatikana basi tutaajiri na kuhakikisha kwamba vituo vyote vinafanya kazi kama ambavyo nguvu za wananchi zimetumika katika eneo hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ni kweli kwa taarifa tuliyonayo maboma ambayo yamekamilishwa nchini ni mengi kama ambavyo Jimbo la Igunga na Tabora kwa ujumla wamefanya. Hili nalo tunaomba tuahidi kwamba huu ni mwaka wa fedha, tumetenga fedha kwa bajeti ya mwaka 2019/2020 ili tumalizie maboma haya. Tunaomba wananchi waendelee kuisaidia Serikali kujenga maboma, tujitahidi kukamilisha ili huduma iweze kupatikana. Ahsante.

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE.DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Katika Ilani ya CCM kuhusu huduma za afya nchini ni kujenga zahanati katika vijiji na kituo cha afya katika kila kata; kwa sasa Jimbo la Igunga lina vituo vya afya viwili tu katika kata 2 kati ya 17 na zahanati kwenye vijiji 19 tu kati ya vijiji 68:- (a) Je, ni lini Serikali itajenga vituo vya afya kwenye kata 15 zilizosalia? (b) Je, ni lini Serikali itajenga zahanati kwenye vijiji 49 vilivyosalia?

Supplementary Question 2

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Ni sera ya Serikali kuwa na hospitali katika kila wilaya. Wilaya ya Karatu haina Hospitali ya Wilaya na hivi karibuni Halmashauri imetenga eneo la kutosha kwa ajili ya kujenga hospitali hiyo na wananchi kwa kutumia mapato yao ya ndani pamoja na wadau mfano Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro wameanza kujenga…

NAIBU SPIKA: Uliza swali lako Mheshimiwa Qulwi.

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali sasa iko tayari kutoa fedha ili kukamilisha ujenzi wa hospitali hiyo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ni kweli kwamba sasa hivi Serikali ipo kwenye hatua ya kujenga Hospitali za Wilaya mbalimbali nchini na hatua ya kwanza tulianza na hospitali 67 na awamu ya pili inaendelea. Tunawapongeza wananchi wa Karatu kwa kuendelea kuchangia huduma hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri tukamilishe kwanza hizi zilizopo baada ya hapo tutachangia na kumalizia Hospitali ya Mheshimiwa wa Karatu pia na maeneo mengine nchini. Hatua ya kwanza majengo yamekamilika tunapeleka vifaa tiba na kuna hatua ya pili ya wataalam mbalimbali. Tukianza kutoa huduma katika vituo hivyo nafikiri tutaenda na eneo letu la Karatu. Ahsante.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE.DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Katika Ilani ya CCM kuhusu huduma za afya nchini ni kujenga zahanati katika vijiji na kituo cha afya katika kila kata; kwa sasa Jimbo la Igunga lina vituo vya afya viwili tu katika kata 2 kati ya 17 na zahanati kwenye vijiji 19 tu kati ya vijiji 68:- (a) Je, ni lini Serikali itajenga vituo vya afya kwenye kata 15 zilizosalia? (b) Je, ni lini Serikali itajenga zahanati kwenye vijiji 49 vilivyosalia?

Supplementary Question 3

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Tunashukuru Serikali kwa kujenga Kituo cha Afya cha Kaloleni katika Jiji la Arusha pamoja na kutujengea jengo la mionzi lakini kituo hiki hakina mashine ya X-ray. Je, ni lini Serikali itatuletea mashine ya X-ray katika Kituo cha Afya cha Kaloleni katika Jiji la Arusha?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Catherine Magige, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi Serikali iko katika maandalizi ya mpango wa kufanya uboreshaji wa huduma za mionzi nchini na tumeanza kwanza katika Hospitali za Rufaa za Kanda, Mikoa na baadhi ya Wilaya. Tutakapomaliza hapo tutakuja sasa kuangalia vituo vya afya ambavyo vina uwezo kuweza kupata hizo huduma na wataalamu ambao wanaweza kutoa hizo huduma.

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE.DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Katika Ilani ya CCM kuhusu huduma za afya nchini ni kujenga zahanati katika vijiji na kituo cha afya katika kila kata; kwa sasa Jimbo la Igunga lina vituo vya afya viwili tu katika kata 2 kati ya 17 na zahanati kwenye vijiji 19 tu kati ya vijiji 68:- (a) Je, ni lini Serikali itajenga vituo vya afya kwenye kata 15 zilizosalia? (b) Je, ni lini Serikali itajenga zahanati kwenye vijiji 49 vilivyosalia?

Supplementary Question 4

MHE. MENDRARD L. KIGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kuna Vituo vya Afya vya Mtwango, Nunga na Iramba tushaezeka na kila kitu tayari. Je, Serikali itamalizia lini yale majengo ili wananchi waanze kuvitumia?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Mufindi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Mufindi kuna kituo cha afya kimekamilishwa na wananchi lakini vituo vingi vya afya vimejengwa nchini kama nilivyosema katika jibu langu la msingi. Tunawapongeza wananchi kwa kushirikiana na Serikali kuiunga mkono katika hatua hii muhimu ya kuboresha huduma za afya. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutawasiliana tuone wamefikia hatua gani kwa kushirikiana na Halmashauri na kama kuna mpango wao basi tuone namna ya kumaliza kituo hiki ili kuunga mkono nguvu za wananchi ili zisipotee bure.