Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Catherine Nyakao Ruge

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE N. RUGE aliuliza:- Bado kuna kata ambazo hazina shule za sekondari hivyo kufanya baadhi ya wanafunzi kusafiri umbali mrefu kwenda na kurudi shuleni, kutokana na hali hiyo baadhi ya wazazi wameamua kuwapangishia vyumba watoto wao mitaani kwenye mazingira ambayo si salama. Je, kwa nini Serikali isije na mpango mahususi wa ujenzi wa mabweni kama inavyofanya kwenye madawati ili kuwapunguzia wanafunzi hasa wa kike adha ya kutembea umbali mrefu kwenda na kurudi nyumbani?

Supplementary Question 1

MHE. CATHERINE N. RUGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini nachelea kusema level ya seriousness kwenye hili jambo bado ipo chini sana. Nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2016/2019 Serikali ilitenga shilingi milioni 750 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni katika shule za sekondari kwenye kata zenye mazingira magumu, lakini kwenye taarifa hii ya utekelezaji ukurasa wa 132 mpango huu umetekelezwa kwa asilimia sita tu. Ningependa kufahamu, ukiwa umebaki mwaka mmoja kukamilika kwa mpango huu ni lini sasa Serikali itakamilisha ujenzi wa wabweni haya kwenye shule kumi ili kupunguza adha kwa wanafunzi wa kike. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Serengeti yenye Kata 30 ina shule za sekondari kwenye Kata 21 tu na Kata 9 hazina shule za Kata. Kata hizo ni Lung’avule, Getasamo, Kiambai, Morotonga, Sedeko na kadhalika. Ningependa kufahamu ni lini sasa Serikali itakamilisha ujenzi wa shule za sekondari kwenye hizi kata tisa? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Ruge amenukuu Mpango wa Taifa wa miaka mitano na mimi kwa niaba ya Serikali napenda nimuhakikishie kwamba mpango ule tunaendelea kuutekeleza mwaka hadi mwaka na itakavyofika mwisho mwaka wa utekelezaji wa mpango wa miaka mitano, malengo mengi yaliyomo yatakuwa yametekelezwa. Mheshimiwa Mbunge naomba asiwe na wasiwasi na awaarifu wananchi ambao anawawakilisha kwamba tutatekeleza mpango ule na utakapofika mwisho wa mwaka utekelezaji wake tutakuwa tumefikia malengo mengi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ameuliza kwenye Wilaya ya Serengeti kwamba ina kata 30; kata 21 zina shule za sekondari na kata tisa hazina shule za sekondari na akauliza lini tutajenga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye swali lake la msingi ni wazi kwamba kata hizo ambazo hazina shule sekondari wanafunzi wake ni miongoni mwa wanafunzi ambao wanatembea umbali mrefu kufuata shule kwenye kata za jirani. Nimehimiza kwenye jibu la msingi kwamba Halmashauri iendelee kushirikiana na wadau wengine pamoja na wananchi kuhakikisha kwamba Kata hizo zinaanza ujenzi wa shule na Serikali itaingia kusaidia mara watakapoanza ujenzi huo. (Makofi)

Name

Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE N. RUGE aliuliza:- Bado kuna kata ambazo hazina shule za sekondari hivyo kufanya baadhi ya wanafunzi kusafiri umbali mrefu kwenda na kurudi shuleni, kutokana na hali hiyo baadhi ya wazazi wameamua kuwapangishia vyumba watoto wao mitaani kwenye mazingira ambayo si salama. Je, kwa nini Serikali isije na mpango mahususi wa ujenzi wa mabweni kama inavyofanya kwenye madawati ili kuwapunguzia wanafunzi hasa wa kike adha ya kutembea umbali mrefu kwenda na kurudi nyumbani?

Supplementary Question 2

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa Mkoa wa Mara ilionekana kwamba mtoto wa kike hana thamani kwa upande wa elimu. Sasa Serikali imeona kabisa kwamba kuna shida ya mabweni ya watoto wa kike. Mtoto wa kike anapotoka shule kwenda nyumbani anakwenda kufanya kazi za nyumbani na anapotoka tena nyumbani kwenda shuleni ni umbali mrefu anafika amechoka sana.
Kwa nini Serikali isichukue hatua ya haraka kuhakikisha inajenga mabweni katika shule za Mkoa wa Mara? Ahsante.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama alivyosema ni kweli katika baadhi ya mazingira tunaweka kipaumbele kujenga mabweni kwa mfano katika maeneo ya wafugaji na baadhi ya maeneo katika baadhi ya mikoa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ya kujenga mabweni kwenye kila shule ya sekondari nchini ni kubwa sana, lakini vilevile katika mazingira ambayo shule imesajiliwa kama shule ya kutwa kwa mazingira yake siyo vizuri sana kuweka mabweni wakati mtoto anaweza akatembea umbali wa kilomita mbili, moja ama mita 500 akafika shuleni. Kwa hiyo, ni jambo ambalo tunaliangalia case by case kwa mazingira na tunahimiza kwamba wazazi, wananchi na Halmashauri zijenge dahania (hostel) ambazo zitasaidia hasa watoto wa kike wasitembee umbali mrefu kwenda nyumbani na shuleni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hicho ndicho kitu tunachohimiza na Serikali itawaunga mkono katika kuendesha yale mabweni. Shule ikipandisha hadhi tu ikapata hadhi ya kuchukua wanafunzi kutoka mikoa mingine, Serikali inaingiza mkono moja kwa moja hapo kusaidia, ahsante. (Makofi)

Name

Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. CATHERINE N. RUGE aliuliza:- Bado kuna kata ambazo hazina shule za sekondari hivyo kufanya baadhi ya wanafunzi kusafiri umbali mrefu kwenda na kurudi shuleni, kutokana na hali hiyo baadhi ya wazazi wameamua kuwapangishia vyumba watoto wao mitaani kwenye mazingira ambayo si salama. Je, kwa nini Serikali isije na mpango mahususi wa ujenzi wa mabweni kama inavyofanya kwenye madawati ili kuwapunguzia wanafunzi hasa wa kike adha ya kutembea umbali mrefu kwenda na kurudi nyumbani?

Supplementary Question 3

MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye majibu ya msingi ya Mheshimiwa Naibu Waziri ametuhamasisha Waheshimiwa Wabunge tuwahamasishe wananchi ili waweze kujenga shule za sekondari kwenye Kata ambazo hazina sekondari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Jimbo langu la Kigoma Kusini tunazo shule mbili za sekondari; tunayo Shule ya Basanza na Shule ya Mwakizega, lakini kinachosikitisha ni kwamba tangu hizi shule wananchi wamejenga wameweka madarasa kumi, ofisi za walimu na sasa hivi wanakimbizana na maabara. REO Mkoa wa Kigoma na Ukaguzi hawataki kabisa kuzisajili hizi shule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini TAMISEMI na Wizara ya Elimu hawakai pamoja na kuona ni jinsi gani shule ambazo mnatuhamasisha tuwaambie wananchi wajenge muwe pia mnazipa kipaumbele katika usajili? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimhakikishie dada yangu, Mheshimiwa Hasna kwamba TAMISEMI na Wizara ya Elimu tunafanya kazi kwa vizuri zaidi, ndiyo maana mimi na pacha wangu, Mheshimiwa Profesa Ndalichako tunakwenda vizuri, lakini hata hivyo naomba niwahakikishie kwamba tumefanya hamasa kubwa sana watu wajenge hizi shule kwa ajili ya kupunguza umbali wa watoto kusafiri na hasa kesi ya mimba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na inawezekana kuna maeneo mengine kuna case by case, naomba niichukulie kesi hii ya Mkoa wa Kigoma, Uvinza kuona kuna nini kinachoendelea. Lakini hata hivyo, naomba nitumie fursa hii kumuagiza Mkurugenzi wangu wa Elimu pale Ofisi ya Rais, TAMISEMI kufuatilia jambo hilo haraka iwezekanavyo ili mradi kwamba kama vigezo vyote vimekamilika kuweka mchakato wa haraka kuhakikisha shule hizo zinasaidiwa haraka iwezekanavyo.

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimshukuru Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa majibu mazuri ambayo ameyatoa na nimesimama hapa kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge kwamba Wizara yangu ndiyo inayohusika na usajili wa shule na hakuna urasimu wowote katika kusajili shule. Kinachotakiwa ni kwamba wanapoomba usajili vigezo na masharti viwe vimekamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu shule ambazo Mheshimiwa Mbunge, dada yangu, amezisema, bahati nzuri hizo shule nazifahamu na ukaguzi ulishafanyika. Kuna mapungufu ambayo yameonekana na hatua iliyopo sasa hivi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza ameshaji- commit kwamba ndani ya miezi mitatu, ifikapo Disemba, 2018 atakuwa amekamilisha mapugufu yaliyopo na timu yangu itarudi kukagua na kama viko vizuri usajili utatolewa kwa sababu tuko hapa kwa ajili ya kuwezesha juhudi za wananchi watoto wakasome.