Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA aliuliza:- Migogoro ya wakulima na wafugaji katika Wilaya za Mvomero na Kilosa Mkoani Morogoro inaendelea kugharimu maisha ya watu, mifugo pamoja na uharibifu wa mazao. Je, Serikali imejipanga vipi katika kutafuta suluhu ya kudumu?

Supplementary Question 1

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Spika, migogoro ya wakulima na wafugaji katika Mkoa wa Morogoro umetokana hasa na kutokuwepo na mipango mizuri ya matumizi ya ardhi. Maeneo yanayofaa kwa kilimo wamepewa wafugaji na maeneo yanayofaa kwa wafugaji wamepewa wakulima. Je, Serikali inampango gani kuainisha upya maeneo hayo ili kuwapa wananchi na kuondoa hii migogoro?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kwa kuwa migogoro hii ya wakulima na wafugaji mingi imechangiwa na Watendaji wa Ardhi katika Vijiji na Kata: Serikali haioni sasa kuna haja ya kuwalipa fidia wananchi ambao wamebaki na makovu kutokana na migogo hii?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, swali la kwanza ameongelea habari ya matumizi bora ya ardhi katika maeneo na amesema kwamba maeneo ya ufugaji wamepewa wakulima na maeneo ya wakulima wamepewa wafugaji.

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa napenda nimdhibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba upangaji wa matumizi ya ardhi haufanywi na Wizara. Upangaji wa matumizi wa ardhi, mdau wa kwanza ni mwananchi wa eneo husika. Tunapokuja ku-facilitate lile zoezi la upangaji, wananchi wenyewe wanakuwa wameshaainisha maeneo yao kwa ajili ya ufugaji na maeneo kwa ajili kilimo. Kwa hiyo, kinachofanyika pale ni kuweka mipaka kwa maana ya kwamba maeneo ya ufugaji yafahamike na maeneo ya kilimo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, pale inapotokea vurugu, ni kati ya watumiaji wa ardhi wanapokiuka makubaliano ya awali, kwamba mfugaji anatoka kwenye eneo lake la ufugaji anakwenda kwenye maeneo ya kilimo; au mtu wa kilimo anakwenda kulima kwenye maeneo ya wafugaji. Kwa hiyo, mgogoro mkubwa ulioko hapa ni kwa watumiaji wa ardhi.

Mheshimiwa Spika, nitoe rai tu katika maeneo yote yenye migogoro kati ya wakulima na wafugaji na ambapo mpango wa matumizi bora ardhi umepangwa, waheshimu maamuzi ambayo wameyafikia wao wenyewe na yanakuwa yameingia katika mpango wa matumizi bora ya ardhi. Kwa hiyo, hili ni jambo la watumiaji ardhi ambapo tunasisitiza waheshimu pale ambapo haijafanyika. Kwa wale ambao hawajapanga matumizi bora ya ardhi, basi nitoe rai tu kwamba mpango huo ufanyike na Wizara ipo tayari kwa ajili ya kuratibisha zoezi hilo ili angalau wananchi wote waweze kuwa na maeneo yao yaliyopangiwa matumizi kuepuka hii migogoro na inapotokea wanakiuka utaratibu, basi sheria ziweze kuchukuliwa.

Mheshimiwa Spika, swali lingine amesema Watendaji ambao wanachangia pengine kupata migogoro na licha ya hivyo kunakuwa na fidia za watu, niseme kwamba Watendaji hao kama wapo, ndiyo maana Wizara kuna baadhi ya Watendaji imewasimamisha kazi na wengine wameondolewa kwa kukiuka maadili ya utendaji wao.

Mheshimiwa Spika, suala la kusema kwamba kunakuwa na suala la kulipa fidia, hilo ziwezi kulitolea maamuzi sasa kwa sababu hatujawa na changamoto nalo kama Wizara na kuangalia hasa changamoto hii imetokana na nini? Kwa Watendaji waliokiuka taratibu zao, hatua zinachukuliwa. Sasa hivi tunamshukuru Mungu kwamba angalau wameanza kuwa na maadili kiutendaji tofauti na siku za nyuma.