Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 6 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 68 2019-02-04

Name

Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA aliuliza:-

Migogoro ya wakulima na wafugaji katika Wilaya za Mvomero na Kilosa Mkoani Morogoro inaendelea kugharimu maisha ya watu, mifugo pamoja na uharibifu wa mazao.

Je, Serikali imejipanga vipi katika kutafuta suluhu ya kudumu?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Devotha Mathew Minja, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ili kukabiliana na migogoro ya matumizi ya ardhi katika Wilaya za Mvomero na Kilosa, Wizara yangu kwa kushirikiana na Halmashauri husika imekuwa ikichukua jitihada mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuandaa mpango wa matumizi ya ardhi ya vijiji na Wilaya kwa ajili ya kuainisha matumizi mbalimbali ikiwemo suala la kilimo na ufugaji; kupima mipaka ya vijiji na kuiwekea alama za kudumu; kupima vipande vya ardhi za wananchi na kuwapatia hati za hakimiliki za kimila, lakini pia kubatilisha miliki za mashamba yasiyoendelezwa na kuyapangia matumizi mengine na kufanya ziara za mara kwa mara katika maeneo yenye migogoro ili kuyapatia ufumbuzi.

Mheshimiwa Spika, pamoja na juhudi hizo Wizara inaelekeza mradi wa majaribio ya kuwezesha umilikishaji wa ardhi ya vijiji (Land Tenure Support Program) katika Wilaya ya Kilombero, Ulanga na Malinyi. Mradi huu unatarajiwa kusambaa (ku-scale up), katika Wilaya zingine za Mkoa wa Morogoro zikiwemo Wilaya za Mvomero na Kilosa. Lengo la kukamilika kwa kazi hii ya uandaaji wa mpango wa matumizi bora ya ardhi, upimaji wa mipaka na vijiji na upimaji wa vipande vya ardhi na kukamilisha kumilikisha wananchi na hivyo kupunguza migogoro ya matumizi ya ardhi katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, natoa rai kwa wananchi katika Wilaya ya Kilosa na Kilombero kuendelea kuheshimu Sheria za Ardhi, hususan kufuata mipango ya matumizi ya ardhi iliyoainishwa na hivyo kuondoa uwezekano wa kuibuka kwa migogoro isiyokuwa ya lazima.