Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:- Pamoja na kuhudumia wagonjwa wengi wakiwemo watokao Wilaya ya Kondoa, Chemba, Kiteto, Babati na wakati mwingine hata Hanang’, lakini Hospitali ya Mji wa Kondoa haina gari la wagonjwa (Ambulance) na uhitaji wa huduma za dharura na rufaa umeongezeka sana baada ya kukamilika kwa barabra kuu itokayo Dodoma – Babati:- Je, ni lini Serikali itaipatia gari la wagonjwa hospitali hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na pia nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu. Labda niseme tu kweli tunaishukuru Serikali kupata, nitumie lugha ya haka kagari, tumepata gari aina ya Suzuki Maruti ndogo sana ambayo kwa mazingira ya Jimbo la Kondoa lina uwezo wa kufanya shunting katika kata tatu za mjini tu, huku pembezoni litakuwa haliwezi kwenda kabisa kwa sababu njia haziruhusu. Je, ule umuhimu wa uhitaji wa huduma hii, Serikali haioni?.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; barabara kubwa imekamilika ya kutoka Dodoma kwenda Babati. Ongezeko la uhitaji wa huduma za dharura umekuwa mkubwa kweli, ajali ni nyingi kila uchao tunapata taarifa hizi, gari hili haliwezi kumudu. Je, ni lini sasa Serikali itatuletea gari la wagonjwa lenye kukidhi mahitaji ya hospitali ya Mji Kondoa?(Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Sannda anaita ‘kagari’ lakini gari zile zimetengenezwa kwa ajili ya mazingira ya Kiafrika na ukitazama jiografia ya Kondoa ukilinganisha na maeneo mengine ambayo gari zile zimepelekwa, nimtoe wasiwasi, wanasema ‘ukubwa wa pua siyo wingi wa makamasi’. Ile gari itamudu kufanya kazi iliyokusudiwa na katika maeneo ambayo gari kama zile zimepelekwa hatujapata malalamiko yoyote. Ni vizuri, wanasema ‘asiyeshukuru kwa kidogo hata ukimpa kikubwa hawezi kushukuru’. Ni jitihada za Mheshimiwa Rais na tuna kila sababu ya kuziunga mkono. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili, anauliza ni lini sasa itapatikana gari nyingine. Naomba nimhakikishie kwamba ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba inapunguza adha ya usafiri hasa kwa wagonjwa wetu, pale ambapo uwezo utaruhusu zikapatikana gari zingine tutaanza kuzipeleka maeneo ambayo hawakupata magari kabisa. (Makofi)

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:- Pamoja na kuhudumia wagonjwa wengi wakiwemo watokao Wilaya ya Kondoa, Chemba, Kiteto, Babati na wakati mwingine hata Hanang’, lakini Hospitali ya Mji wa Kondoa haina gari la wagonjwa (Ambulance) na uhitaji wa huduma za dharura na rufaa umeongezeka sana baada ya kukamilika kwa barabra kuu itokayo Dodoma – Babati:- Je, ni lini Serikali itaipatia gari la wagonjwa hospitali hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali moja la nyongeza. Kwa kuwa, Kituo cha Afya cha Mbori kinachojengwa kinakaribia kukamilika pamoja na kwamba hakijapata milioni 500, lakini kwa kuwa kituo hiki kitahudumia Kata ya Lupeta, Kimagai, Godegode, Mlembule na Matomondo. Je, Mheshimiwa Waziri uko tayari kuwapeleka gari la wagonjwa kwa sababu litahudumia watu zaidi ya laki moja.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba kwa dhati kabisa nimpongeze Mheshimiwa Lubeleje jinsi ambavyo amekuwa akiwapigania wananchi wake na hasa kuhusiana na suala zima la afya. Baada ya kupongeza ni vizuri Mheshimiwa Lubeleje kwa kushirikiana na wananchi na Halmashauri yake wakahakikisha hicho kituo cha afya ambacho anakisema hakijamalizika jitihada ziongezwe ili kiweze kukamilika kwa wakati. Pia nimhakikishie kwamba ni azma ya Serikali pale ambapo uwezo unaruhusu kupeleka gari za ambulance maeneo ambayo yana uhitaji mkubwa.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:- Pamoja na kuhudumia wagonjwa wengi wakiwemo watokao Wilaya ya Kondoa, Chemba, Kiteto, Babati na wakati mwingine hata Hanang’, lakini Hospitali ya Mji wa Kondoa haina gari la wagonjwa (Ambulance) na uhitaji wa huduma za dharura na rufaa umeongezeka sana baada ya kukamilika kwa barabra kuu itokayo Dodoma – Babati:- Je, ni lini Serikali itaipatia gari la wagonjwa hospitali hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona, naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri. Hospitali yetu ya Mkoa wa Lindi ya Sokoine haina gari la Mganga Mkuu wa Mkoa na hii hupelekea Mganga Mkuu wa Mkoa kutumia gari yake ya binafsi (private car). Je, ni lini hospitali yetu ya Lindi ya Mkoa itapelekewa gari kwa ajili ya Mganga Mkuu? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Mheshimiwa Salma Kikwete kwa jinsi ambavyo amekuwa akilifuatilia jambo hili. Mimi binafsi ameshanifuata na suala hili nikalichukua na kulipeleka Ofisi ya Rais, TAMISEMI na tulikuwa tunafanya logistics juu ya tatizo hili na ukubwa wake. Naomba nimhakikishie, Ofisi ya Rais, TAMISEMI imelipokea kwa sababu siyo hali ya kawaida kwa Mganga Mkuu wa Mkoa kutumia gari yake binafsi katika kufanya shughuli za Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba atupe muda kwa kadri tutakavyoweza tukipata nafasi ya kwanza kabisa suala hili tutalitatua.

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:- Pamoja na kuhudumia wagonjwa wengi wakiwemo watokao Wilaya ya Kondoa, Chemba, Kiteto, Babati na wakati mwingine hata Hanang’, lakini Hospitali ya Mji wa Kondoa haina gari la wagonjwa (Ambulance) na uhitaji wa huduma za dharura na rufaa umeongezeka sana baada ya kukamilika kwa barabra kuu itokayo Dodoma – Babati:- Je, ni lini Serikali itaipatia gari la wagonjwa hospitali hiyo?

Supplementary Question 4

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, magari ambayo ameyazungumzia Mheshimiwa Sannda kwetu Mchinga tunayahitaji sana. Kituo cha Afya Kitomanga kinahitaji gari la wagonjwa lakini hakuna, nataka kujua tu, ni sifa gani ambazo haya magari yanapatikana ili tufuate hizo procedure kwa sababu taarifa tulizonazo humu ndani kuna Wabunge wamepewa mpaka magari mawili, wengine matatu, wakati wengine hatuna hata moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni hilo kwamba tutumie vigezo gani tupate haya magari?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamba kuna sifa specific ambayo inabidi itumike ili kupata gari, hilo sina. Kinachozingatiwa ni uhitaji mkubwa wa maeneo ambayo yanahitaji magari na kwa uwiano kwamba zimepatikana gari ngapi ndipo zinagawiwa. Kwa hiyo, hakuna specific procedure kwamba sasa Mheshimiwa Bobali sasa hiyo sifa uwe nayo ili uweze kupata gari hiyo. Pale ambapo kuna uhitaji mkubwa na kwa kuzingatia jiografia ya maeneo husika na umbali wa wananchi kuweza kwenda kupata huduma hizo ndiyo sifa ambazo zinatakiwa.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:- Pamoja na kuhudumia wagonjwa wengi wakiwemo watokao Wilaya ya Kondoa, Chemba, Kiteto, Babati na wakati mwingine hata Hanang’, lakini Hospitali ya Mji wa Kondoa haina gari la wagonjwa (Ambulance) na uhitaji wa huduma za dharura na rufaa umeongezeka sana baada ya kukamilika kwa barabra kuu itokayo Dodoma – Babati:- Je, ni lini Serikali itaipatia gari la wagonjwa hospitali hiyo?

Supplementary Question 5

MHE. AISHAROSE N. MATEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Tatizo lililopo Kondoa Mjini halina tofauti na tatizo lililopo Jimbo la Singida Mjini. Kwa kuwa, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida ndiyo kimbilio la wananchi wengi katika kupata huduma za afya, lakini hospitali hiyo haina kabisa gari la kubebea wagonjwa. Je, ni lini sasa Serikali itapeleka gari la kubebea wagonjwa ili kuokoa vifo vya akinamama na watoto? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, jiografia na maeneo yanatofautiana. Kama hitaji kubwa kwa hospitali ya mkoa ni gari la wagonjwa na kwa sasa halipo, naomba nimtake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Singida ahakikishe miongoni mwa gari zilizopo anateua gari moja itumike kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa wakati Serikali ikijipanga kuja kupeleka gari la wagonjwa. (Makofi)

Name

Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:- Pamoja na kuhudumia wagonjwa wengi wakiwemo watokao Wilaya ya Kondoa, Chemba, Kiteto, Babati na wakati mwingine hata Hanang’, lakini Hospitali ya Mji wa Kondoa haina gari la wagonjwa (Ambulance) na uhitaji wa huduma za dharura na rufaa umeongezeka sana baada ya kukamilika kwa barabra kuu itokayo Dodoma – Babati:- Je, ni lini Serikali itaipatia gari la wagonjwa hospitali hiyo?

Supplementary Question 6

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, nami niulize swali moja dogo la nyongeza. Hospitali ya Wilaya ya Manyoni pamoja na kuhudumia Wilaya ya Manyoni lakini inahudumia Wilaya ya Ikungi, Sikonge, Wilaya ya Bahi, Wilaya ya Chemba imezidiwa sana na haina kabisa gari la wagonjwa. Je, ni lini sasa Serikali itaipatia hospitali hii ya Wilaya gari la wagonjwa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, tutakubaliana Wabunge wote kwamba, nia ya Serikali na jinsi ambavyo inatenda katika kupunguza adha ya wagonjwa kwa maana ya uwepo wa magari sote ni mashuhuda tumeliona. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pale ambapo nafasi ya kifedha itaruhusu tuna kila sababu ya kuhakikisha kwamba maeneo yale yote ambayo yanahitaji kupelekewa gari za wagonjwa tunapeleka na kwa kufuata vigezo kama ambavyo nilivyotangulia kujibu katika swali langu la msingi.