Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 40 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 334 2018-05-30

Name

Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:-
Pamoja na kuhudumia wagonjwa wengi wakiwemo watokao Wilaya ya Kondoa, Chemba, Kiteto, Babati na wakati mwingine hata Hanang’, lakini Hospitali ya Mji wa Kondoa haina gari la wagonjwa (Ambulance) na uhitaji wa huduma za dharura na rufaa umeongezeka sana baada ya kukamilika kwa barabra kuu itokayo Dodoma – Babati:-
Je, ni lini Serikali itaipatia gari la wagonjwa hospitali hiyo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Edwin Mgante Sannda, Mbunge wa Kondoa Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuwa kwa muda mrefu hospitali ya Mji wa Kondoa imekuwa na ukosefu wa gari la wagonjwa hali ambayo imechangiwa na uchakavu wa gari lililokuwepo. Hata hiyo, Halmashauri ya Mji wa Kondoa imepata gari la wagonjwa (Ambulance) iliyotolewa tarehe 16 Machi, 2018 katika mgao wa magari yaliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.