Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA (K.n.y. JOSEPH M. MKUNDI) aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe (Nansio) inakabiliwa na msongamano wa Wagonjwa; Mwaka 2002 Halmashauri ya Wilaya ilitumia zaidi ya shilingi milioni 200 kuanza ujenzi wa Kituo cha Afya Nakutunguru kama njia ya kupunguza msongamano huo. Hata hivyo, ujenzi huu haujakamilika kutokana na ukosefu wa fedha:- Je, Serikali ipo tayari kuondoa upungufu uliopo ili Kituo hicho kianze kutoa huduma?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na jitihada kubwa za Serikali kupitia Wizara yake ya TAMISEMI kuhakikisha inaboresha vituo vingi vya afya kikiwemo na Kituo cha Afya hiki cha Ukerewe, kama Mheshimiwa Waziri anavyofahamu kwamba kumekuwa na changamoto kubwa ya watumishi, vifaa tiba ambavyo kwa kweli vingesaidia zaidi ufanisi na ubora wa utumishi kwenye hospitali hii. Je, ni lini hasa Serikali itahakikisha suala hili linafanyiwa kazi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali dogo la pili, kwa sababu matatizo ya Ukerewe kwa namna fulani yanafafana sana matatizo yaliyoko kwenye hospitali ya Wilaya ya Nyamagana. Ni nini sasa mpango wa Serikali kwa sababu mara kadhaa hospitali ya Wilaya ya Nyamagana imeshaomba kupatiwa vifaa kama ultra sound na ni lini sasa Serikali inaweza kuhakikisha hospitali ya Nyamagana inapata ultra sound pamoja na X-Ray machine?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, anauliza kuhusiana na Kituo cha Afya Nakutunguru kukamilika na hasa kuwepo na vifaa vya kutolea huduma, pamoja na suala zima la watumishi. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba vituo vya afya vyote vinavyokamilika ni pamoja na kuwa na vifaa vya kufanyia kazi ikiwepo X-Ray, ultra sound hayo yote ni muhimu ili kituo cha afya kiweze kukamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili anaulizia hospitali yake ya Wilaya. Kwanza naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Mabula amekuwa akipigania hospitali hii kwa muda mrefu kuhakikisha kwamba inatoa huduma kwa kadri inavyokusudiwa. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba hospitali zote za Wilaya zinakuwa na vifaa vya kutosha ili viweze kutoa huduma inayotakiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ni azma yetu kuhakikisha kwamba hospitali ya Nyamagana ni miongoni mwa hospitali za Wilaya ambazo zitakua kwa viwango vinavyotakiwa ikiwa ni pamoja na kuwa vifaa vyote vinavyotosheleza.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA (K.n.y. JOSEPH M. MKUNDI) aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe (Nansio) inakabiliwa na msongamano wa Wagonjwa; Mwaka 2002 Halmashauri ya Wilaya ilitumia zaidi ya shilingi milioni 200 kuanza ujenzi wa Kituo cha Afya Nakutunguru kama njia ya kupunguza msongamano huo. Hata hivyo, ujenzi huu haujakamilika kutokana na ukosefu wa fedha:- Je, Serikali ipo tayari kuondoa upungufu uliopo ili Kituo hicho kianze kutoa huduma?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwanza, naishukuru sana Serikali kwa kuweza kunipatia fedha za Kituo cha Afya cha Mwese na Kituo cha Afya cha Mishamo. Tatizo ambalo lipo kwenye eneo la Wilaya ya Tanganyika vituo vya afya havina Wahudumu na Madaktari kwa ujumla. Je, ni lini Serikali itapeleka Madaktari ili waweze kufanya kazi iliyokusudiwa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kakoso anafahamu kabisa kwamba sasa hivi Ofisi ya Rais, TAMISEMI imeshatangaza nafasi kwa ajili ya watu wa afya wakiwepo Madaktari, Wahudumu, Manesi. Naomba nimhakikishie katika hawa ambao watakuwa wameajiriwa na naamini kwamba na wengi watakuwa wameomba wakiwa wanatokea maeneo huko ili pale wanapopewa nafasi ya kwenda kufanya kazi wasije wakasema mazingira yale kwao ni mageni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, ni wajibu wa Serikali kuhakikisha Watumishi tunawasambaza ili wakatoe huduma kwa wananchi.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA (K.n.y. JOSEPH M. MKUNDI) aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe (Nansio) inakabiliwa na msongamano wa Wagonjwa; Mwaka 2002 Halmashauri ya Wilaya ilitumia zaidi ya shilingi milioni 200 kuanza ujenzi wa Kituo cha Afya Nakutunguru kama njia ya kupunguza msongamano huo. Hata hivyo, ujenzi huu haujakamilika kutokana na ukosefu wa fedha:- Je, Serikali ipo tayari kuondoa upungufu uliopo ili Kituo hicho kianze kutoa huduma?

Supplementary Question 3

MHE. RASHID A SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Halmashauri ya Lushoto na hospitali ya Wilaya ya Lushoto inahudumia Majimbo matatu na Halmashauri mbili kwa maana ya Lushoto na Bumbuli na inakabiliwa na msongamo mkubwa sana wa wagonjwa. Je ni lini sasa Serikali itaipa fedha ili kupanua huduma hizi za afya katika Wilaya ya Lushoto?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika kwamba Wilaya ambayo Mheshimiwa Mbunge anaitaja ina population kubwa. Pia ni ukweli usiopinga kwamba Halmashauri wanajua uhitaji, naomba kwa kushirikiana na Halmashauri na hasa Mheshimiwa Mbunge akiwa wa kwanza kuelekeza namna iliyo bora ya kuhakikisha maeneo mengi vituo vya afya vinajengwa hasa kwa kushirikisha wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ni vizuri kama ni suala la ujenzi wa vituo vingine ili kuweza kutoa nafasi kwa hospitali ya Wilaya, wazo hilo jema ni vizuri likaanza kwao na sisi Serikali tutaunga mkono jitihada za wananchi.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA (K.n.y. JOSEPH M. MKUNDI) aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe (Nansio) inakabiliwa na msongamano wa Wagonjwa; Mwaka 2002 Halmashauri ya Wilaya ilitumia zaidi ya shilingi milioni 200 kuanza ujenzi wa Kituo cha Afya Nakutunguru kama njia ya kupunguza msongamano huo. Hata hivyo, ujenzi huu haujakamilika kutokana na ukosefu wa fedha:- Je, Serikali ipo tayari kuondoa upungufu uliopo ili Kituo hicho kianze kutoa huduma?

Supplementary Question 4

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza Swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa wananchi wa Wilaya ya Ngorongoro Mkoa wa Arusha hususani Loliondo wamekuwa wakitegemea hospitali ya Waso kwenye matibabu na hali hii inapelekea msongamano mkubwa katika hospitali ya Waso. Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kujenga hospitali ya Wilaya ya Ngorongoro?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Magige ni shuhuda kwamba tumeweza kujenga hospitali ya Wilaya Arusha pale na Vituo vya Afya vingi ikiwepo na Murieti na yeye ni miongoni mwa watu ambao wamekuwa wakipigania suala zima la afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie tumeanza na hospitali 67, tukishamaliza hizo 67 tutaenda maeneo yale ambayo hakuna hospitali za Wilaya ili kupunguza mlundikano kwa wananchi kupata huduma.