Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 40 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 332 2018-05-30

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA (K.n.y. JOSEPH M. MKUNDI) aliuliza:-
Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe (Nansio) inakabiliwa na msongamano wa Wagonjwa; Mwaka 2002 Halmashauri ya Wilaya ilitumia zaidi ya shilingi milioni 200 kuanza ujenzi wa Kituo cha Afya Nakutunguru kama njia ya kupunguza msongamano huo. Hata hivyo, ujenzi huu haujakamilika kutokana na ukosefu wa fedha:-
Je, Serikali ipo tayari kuondoa upungufu uliopo ili Kituo hicho kianze kutoa huduma?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Michael Mkundi, Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Serikali ilitoa fedha kiasi cha shilingi milioni 200 kupitia fedha za Ruzuku ya Maendeleo kwa Serikali za Mitaa yaani (Local Government Development Grant) mwaka 2012 kwa ajili ya kuanza kwa awamu wa kituo cha Afya Nakatunguru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa jengo hilo OPD ulikamilika mwezi Aprili, 2015 na lilizinduliwa rasmi tarehe 18 Februari, 2018 na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa. Mpaka sasa kituo hiki kinafanya kazi kwa kutoa huduma kwa wagonjwa wa nje (OPD) na huduma za Mama, Baba na Mtoto (Reproduction and Child Health (RCH).
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa Fedha 2018/2019, Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe imeidhinishiwa jumla ya shilingi milioni 45 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya watumishi wa Kituo hiki. Kwa sasa Serikali ipo katika awamu ya nne ya utekelezaji wa mpango wa ukarabati wa Vituo vya Afya nchini, hivyo tutakiingiza Kituo cha Afya Nakutunguru katika awamu zijazo ili kuhahakisha kinakamilika na kutoa huduma zote ikiwemo huduma za upasuaji kwa akinamama wajawazito.