Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Katika Jimbo la Tabora Mjini hasa vijiji na kata zilizopo nje ya Manispaa ikiwemo Kata ya Tumbi na vijiji vinavyoizunguka kata hiyo havijajumuishwa katika Mpango wa REA Awamu ya Tatu. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA katika kata na vijiji hivyo?

Supplementary Question 1

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza, nianze kwa kuishukuru hii Wizara ya Nishati chini ya Dkt. Kalemani pamoja na Naibu wake Mheshimiwa Subira kwa kazi nzuri mnayofanya, hongereni sana. Ninaomba niulize maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Manispaa ya Tabora kwa kuitamka inaonekana kama hata vile vijiji vinavyozunguka ni kama vipo karibu sana, lakini vijiji vingi vipo mbali na maeneo ya mjini. Huu mradi ambao unafadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika kwa ajili ya kusambaza umeme unaonekana unasuasua maeneo mengi ya vijiji hivi ambavyo vimetajwa. Kama kuna uwezekano naomba Serikali iangalie uwezekano wa kuingiza vijiji hivyo kwenye mradi huu wa REA III ili viweze kupatiwa umeme haraka, hilo la kwanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, nilipata taarifa kwamba Mheshimiwa Waziri anaweza kufanya ziara Tabora wiki ijayo sehemu za Urambo, kwa kuwa Tumbi hii ninayoizungumzia ipo njiani, anapokuwa Mheshimiwa Waziri anaelekea Urambo lazima atapita Tumbi pale. Je, Waziri yupo tayari kusimama maeneo yale hata kwa dakika chache ili asikilize kero za wananchi pale zinazohusiana na hilo suala la usambazaji umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Mwakasaka, kwanza hilo la pili nipo tayari kusimama, nitasimama na nitafanya kazi pale, Mheshimiwa Mbunge nakupongeza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na vijiji kweli kabisa Jimbo la Tabora kwanza lina kata 29 na kata 15 zipo mjini na kata 14 kimsingi zipo vijijini ingawa ni za Manispaa. Nimpe tu taarifa Mheshimiwa Mbunge kwa niaba ya wananchi wake zile kata 14 ambazo kimsingi zipo vijijini tumezipelekea kwenye miradi ya REA kwenye mpango wa Peri-Urban. Kwa hiyo, wananchi wake wataendelea kupata umeme kama kawaida. (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Katika Jimbo la Tabora Mjini hasa vijiji na kata zilizopo nje ya Manispaa ikiwemo Kata ya Tumbi na vijiji vinavyoizunguka kata hiyo havijajumuishwa katika Mpango wa REA Awamu ya Tatu. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA katika kata na vijiji hivyo?

Supplementary Question 2

MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa niweze kuuliza swali moja la nyongeza.
Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kuweza kupata nafasi ya kuja katika Jimbo langu la Busokelo, lakini nina swali moja tu kwamba ulivyokuja wana Busokelo tulikuomba kwamba vijiji vyote ambavyo vipo kwenye scope ya REA III na kwa bahati mbaya sana hivi vijiji baadhi yao vina nyumba za nyasi lakini hii leo ninavyouliza swali kwako Mheshimiwa Waziri ni kwamba vile vijiji vimerukwa. Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya Vijiji 8 ambavyo vimerukwa kwenye scope ambayo ipo sasa kwa REA III? (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Atupele, tulifanya ziara pamoja katika Jimbo lake na kwa kweli katika Jimbo la Busokelo vijiji takribani 50 vipo katika REA hii ya Awamu ya Tatu na mkandarasi Stag International tulimwelekeza afanye tathmini katika maeneo yote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hyo, naomba nimthibitishie vile vijiji nane ambavyo vipo kati ya vijiji 50 ambavyo vitapatiwa umeme katika REA awamu hii mzunguko wa kwanza tunamwelekeza mkandarasi vyote avifanyie tathmini na kwa kuwa Serikali imeelekeza nyumba yoyote iwe ya tembe au kawaida zote zinapatiwa umeme na tumeshuhudia mara kadhaa tukizindua umeme na nyumba hizi ambazo zimewekewa umeme. Kwa hiyo, nataka niseme hakuna nyumba mbayo itabaguliwa na mkandarasi atavifikia vile vijiji vinane, asante sana. (Makofi)

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Katika Jimbo la Tabora Mjini hasa vijiji na kata zilizopo nje ya Manispaa ikiwemo Kata ya Tumbi na vijiji vinavyoizunguka kata hiyo havijajumuishwa katika Mpango wa REA Awamu ya Tatu. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA katika kata na vijiji hivyo?

Supplementary Question 3

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hangamoto ya umeme iliyopo manispaa ya Tabora inafanana kabisa na ile ya Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga katika Kata ya Tambani, Mwandege na vijiji vyake. Je, ni lini sasa umeme utawaka kwenye Kata hizi ikizingatiwa mradi wa REA I na REA II tayari ulishapita? Ahsante.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza nikiri kwa kweli kwa Mbunge wa Mkuranga, Mheshimiwa Ulega pamoja na Mheshimiwa Mchafu wamekuwa wakifuatilia sana masuala ya nishati ya umeme katika Wilaya ya Mkuranga. Na ninaomba nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge, mkandarasi wa Mkoa wa Pwani Sengerema tumezungumza naye na Jumapili hii atapeleka nguzo kwa ajili ya maeneo hayo ya Tambani, Mwandege ambapo pana ongezeko kubwa la wananchi na hususani Kijiji cha Mlamleni katika Wilaya ya Mkuranga. Nataka nimthibitishie kazi kuanzia Jumamosi hii nguzo zitafika na itaendelea katika Mradi huu wa REA Awamu ya Tatu. Ahsante sana.

Name

Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Katika Jimbo la Tabora Mjini hasa vijiji na kata zilizopo nje ya Manispaa ikiwemo Kata ya Tumbi na vijiji vinavyoizunguka kata hiyo havijajumuishwa katika Mpango wa REA Awamu ya Tatu. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA katika kata na vijiji hivyo?

Supplementary Question 4

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, Jimbo la Mbozi lenye kata 11 kuna kata mbili ambazo karibu vijiji 14 havina umeme kabisa. Sasa naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri, ni lini sasa hizi kata mbili za Magamba na Kata ya Bara zitapatiwa umeme wa REA? Ahsante sana.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme mpango wa Serikali ni kupeleka umeme katika maeneo yote ambayo yamesalia, vijiji 7,873. Kwa hiyo, kwa kuwa swali lake limejielekeza kwenye kata mbili ambazo zina vijiji 14 na hakuna umeme kabisa, nataka nimuarifu kwa kipindi hiki cha 2018/2019 – 2019/2020 Serikali itakamilisha upelekaji wa umeme katika maeneo ya hizo kata mbili na vijiji vyake kwa mradi huu kabambe wa REA Awamu ya Tatu unaoendelea kutekelezwa ndani ya mwaka huu wa fedha na unaoendelea. Ahsante.

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Katika Jimbo la Tabora Mjini hasa vijiji na kata zilizopo nje ya Manispaa ikiwemo Kata ya Tumbi na vijiji vinavyoizunguka kata hiyo havijajumuishwa katika Mpango wa REA Awamu ya Tatu. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA katika kata na vijiji hivyo?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza REA kwa kazi nzuri, lakini hata hivyo katika Wilaya yetu ya Hanang kuna changamoto nyingi ambazo tunaziona, kwa mfano kuna taasisi ambazo hazijapata umeme pale ambapo umeme umeletwa, kuna maeneo yanarukwa njiani wanakwenda kwingine, je, Waziri atakubali kuja kutembelea Hanang ili tuone changamoto hizo ili tuzisahihishe na kama anaweza kumtuma mkandarasi kuja kuona changamoto hizo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru mama yangu, Mheshimiwa Dkt. Nagu na tumekubali huo mwaliko wa kutembelea kwa kuwa sisi Wizara yetu pamoja na Mheshimiwa Waziri na viongozi mbalimbali tumekuwa tukifanya ziara kwa kuwa miradi hii inatekelezwa vijijini. Kwa hiyo, naomba nimuagize pia mkandarasi Angelic, tuliwapa maelekezo wakandarasi wote taasisi muhimu za umma zipatiwe huduma hii ya umeme na maelekezo ya Serikali kupitia Mheshimiwa Rais pia mwenyewe kwamba vijiji visirukwe. Kwa hiyo, naomba nisisitize maelekezo haya yako palepale na tutafanya ziara katika maeneo yote likiwemo Jimbo la Hanang.

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Katika Jimbo la Tabora Mjini hasa vijiji na kata zilizopo nje ya Manispaa ikiwemo Kata ya Tumbi na vijiji vinavyoizunguka kata hiyo havijajumuishwa katika Mpango wa REA Awamu ya Tatu. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA katika kata na vijiji hivyo?

Supplementary Question 6

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana, kwanza nianze kwa kumpongeza Waziri na Naibu Waziri kwa ziara walizozifanya kwenye Halmashauri ya Mbeya. Naibu Waziri alitembelea kata ambazo hazina umeme kabisa lakini zinalizunguka Jiji la Mbeya kama Kata za Swaya na Maendeleo. Je, ni lini hizi kata mbili nazo zitapewa umuhimu wa kupewa umeme?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tukushukuru sana kwa namna ambavyo umetambua mahitaji ya nishati na kuwapa fursa Waheshimiwa Wabunge kuuliza maswali mengi. Umenipa fursa ya kujibu maswali ya Mheshimiwa Njeza, Mheshimiwa Mwamoto pamoja na Mheshimiwa Frank.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Njeza na Mheshimiwa Mwamoto maswali yao yanalingana kwa sababu yamehusisha masuala ya umeme vijijini. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Njeza, tulifanya ziara Mbeya, pamoja na kwamba Jimbo lake ni Mbeya Vijijini, hapa amezisemea kata ambazo zipo ndani ya Jiji la Mbeya, na kama nilivyosema, Serikali imetambua ukuaji wa maeneo katika Miji, Manispaa na Majiji na ndiyo maana tumekuja na mradi huu unaoitwa Peri-Urban. Niliombe Bunge lako tukufu, tutakapowasilisha bajeti yetu ya mwaka 2018/2019 ituunge mkono katika miradi mbalimbali ukiwemo Mradi huu wa Peri- Urban kuupitisha kwa kishindo kisha tufanye kazi ya kupeleka umeme katika maeneo ambayo hayajafikiwa na huduma hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sambamba na hilo, Mheshimiwa Mwamoto, ni kweli tulifanya ziara tena kwa mara ya kwanza Mawaziri wawili, Mheshimiwa Waziri mwenyewe na mimi Naibu Waziri tulikuwa kwenye kata hiyo aliyoitaja. Nataka niseme sisi lengo letu ni kupeleka nishati kwenye maeneo yenye uhitaji ikiwemo mojawapo ya maeneo ambayo kweli yanahitaji nishati ni eneo la viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwapongeze Mheshimiwa Mbunge na vijana hao kwa kutenga eneo la viwanda vidogo vidogo na kwa gharama za Serikali umeme utafika katika maeneo hayo na nitoe rai tu wao waendelee kujipanga kuunganisha lakini umeme utafika kama ambavyo tumeahidi katika ule mkutano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la mwisho la Mheshimiwa Frank, ni kweli Mji wa Tunduma ni mji ambao umekuwa na upo mpakani. Nataka niseme Mji wa Tunduma upo katika Mkoa mpya wa Songwe na wakati huo umeme katika Mkoa wa Songwe ulikuwa unatoka katika njia ya kusafirisha umeme ni ndefu kutoka Mbeya. Serikali ina mpango wa kujenga sub-station palepale Tunduma kwa ajili ya kuufanya Mkoa mzima wa Songwe upate nishati ya uhakika na wakati wote. Kwa hiyo, nimthibitishe Mjumbe kwa kuwa yeye Mheshimiwa Mbunge ni Mjumbe wa Kamati yetu ya Nishati na yeye pia atuunge mkono katika bajeti yetu ili mradi huu wa ujenzi wa sub-station pamoja na line ambayo inatoka Mbeya inayoenda Sumbawanga - Mpanda – Kigoma - Nyakanazi ya KV 400 ambayo yote kwa pamoja itachangia kwa upatikanaji wa umeme wa uhakika. Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana, ahsante sana.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Katika Jimbo la Tabora Mjini hasa vijiji na kata zilizopo nje ya Manispaa ikiwemo Kata ya Tumbi na vijiji vinavyoizunguka kata hiyo havijajumuishwa katika Mpango wa REA Awamu ya Tatu. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA katika kata na vijiji hivyo?

Supplementary Question 7

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii, kwa kuwa Mheshimiwa Waziri alifika Kilolo, tena Kijiji cha Kihesa Mgagao, Kata ya Ng’uruwe, na kuwaahidi vizuri wananchi wa Kilolo kuhusu umeme; na kwa kuwa sasa baadhi ya vijana wameshatenga maeneo kwa ajili ya viwanda vidogo vidogo. Je, ni nani haswa anayepaswa kusogeza umeme kwenye maeneo ambayo vijana tayari wameshatengewa maeneo, ni gharama za nani? (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tukushukuru sana kwa namna ambavyo umetambua mahitaji ya nishati na kuwapa fursa Waheshimiwa Wabunge kuuliza maswali mengi. Umenipa fursa ya kujibu maswali ya Mheshimiwa Njeza, Mheshimiwa Mwamoto pamoja na Mheshimiwa Frank.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Njeza na Mheshimiwa Mwamoto maswali yao yanalingana kwa sababu yamehusisha masuala ya umeme vijijini. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Njeza, tulifanya ziara Mbeya, pamoja na kwamba Jimbo lake ni Mbeya Vijijini, hapa amezisemea kata ambazo zipo ndani ya Jiji la Mbeya, na kama nilivyosema, Serikali imetambua ukuaji wa maeneo katika Miji, Manispaa na Majiji na ndiyo maana tumekuja na mradi huu unaoitwa Peri-Urban. Niliombe Bunge lako tukufu, tutakapowasilisha bajeti yetu ya mwaka 2018/2019 ituunge mkono katika miradi mbalimbali ukiwemo Mradi huu wa Peri- Urban kuupitisha kwa kishindo kisha tufanye kazi ya kupeleka umeme katika maeneo ambayo hayajafikiwa na huduma hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sambamba na hilo, Mheshimiwa Mwamoto, ni kweli tulifanya ziara tena kwa mara ya kwanza Mawaziri wawili, Mheshimiwa Waziri mwenyewe na mimi Naibu Waziri tulikuwa kwenye kata hiyo aliyoitaja. Nataka niseme sisi lengo letu ni kupeleka nishati kwenye maeneo yenye uhitaji ikiwemo mojawapo ya maeneo ambayo kweli yanahitaji nishati ni eneo la viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwapongeze Mheshimiwa Mbunge na vijana hao kwa kutenga eneo la viwanda vidogo vidogo na kwa gharama za Serikali umeme utafika katika maeneo hayo na nitoe rai tu wao waendelee kujipanga kuunganisha lakini umeme utafika kama ambavyo tumeahidi katika ule mkutano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la mwisho la Mheshimiwa Frank, ni kweli Mji wa Tunduma ni mji ambao umekuwa na upo mpakani. Nataka niseme Mji wa Tunduma upo katika Mkoa mpya wa Songwe na wakati huo umeme katika Mkoa wa Songwe ulikuwa unatoka katika njia ya kusafirisha umeme ni ndefu kutoka Mbeya. Serikali ina mpango wa kujenga sub-station palepale Tunduma kwa ajili ya kuufanya Mkoa mzima wa Songwe upate nishati ya uhakika na wakati wote. Kwa hiyo, nimthibitishe Mjumbe kwa kuwa yeye Mheshimiwa Mbunge ni Mjumbe wa Kamati yetu ya Nishati na yeye pia atuunge mkono katika bajeti yetu ili mradi huu wa ujenzi wa sub-station pamoja na line ambayo inatoka Mbeya inayoenda Sumbawanga - Mpanda – Kigoma - Nyakanazi ya KV 400 ambayo yote kwa pamoja itachangia kwa upatikanaji wa umeme wa uhakika. Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana, ahsante sana.

Name

Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Katika Jimbo la Tabora Mjini hasa vijiji na kata zilizopo nje ya Manispaa ikiwemo Kata ya Tumbi na vijiji vinavyoizunguka kata hiyo havijajumuishwa katika Mpango wa REA Awamu ya Tatu. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA katika kata na vijiji hivyo?

Supplementary Question 8

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Tunduma uko mpakani mwa Zambia na Tanzania na ni mji ambao unapokea wageni wengi wanaotoka nchi za Kusini mwa Afrika lakini huduma ya umeme kwenye Mji wa Tunduma ni haba sana na umeme unakatikakatika mara kwa mara na kusababisha usalama wa wageni na wananchi wa Tunduma kuwa hatarini. Je, ni lini Serikali itahakikisha kwamba inaweka umeme wa uhakika katika Mji wa Tunduma?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tukushukuru sana kwa namna ambavyo umetambua mahitaji ya nishati na kuwapa fursa Waheshimiwa Wabunge kuuliza maswali mengi. Umenipa fursa ya kujibu maswali ya Mheshimiwa Njeza, Mheshimiwa Mwamoto pamoja na Mheshimiwa Frank.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Njeza na Mheshimiwa Mwamoto maswali yao yanalingana kwa sababu yamehusisha masuala ya umeme vijijini. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Njeza, tulifanya ziara Mbeya, pamoja na kwamba Jimbo lake ni Mbeya Vijijini, hapa amezisemea kata ambazo zipo ndani ya Jiji la Mbeya, na kama nilivyosema, Serikali imetambua ukuaji wa maeneo katika Miji, Manispaa na Majiji na ndiyo maana tumekuja na mradi huu unaoitwa Peri-Urban. Niliombe Bunge lako tukufu, tutakapowasilisha bajeti yetu ya mwaka 2018/2019 ituunge mkono katika miradi mbalimbali ukiwemo Mradi huu wa Peri- Urban kuupitisha kwa kishindo kisha tufanye kazi ya kupeleka umeme katika maeneo ambayo hayajafikiwa na huduma hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sambamba na hilo, Mheshimiwa Mwamoto, ni kweli tulifanya ziara tena kwa mara ya kwanza Mawaziri wawili, Mheshimiwa Waziri mwenyewe na mimi Naibu Waziri tulikuwa kwenye kata hiyo aliyoitaja. Nataka niseme sisi lengo letu ni kupeleka nishati kwenye maeneo yenye uhitaji ikiwemo mojawapo ya maeneo ambayo kweli yanahitaji nishati ni eneo la viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwapongeze Mheshimiwa Mbunge na vijana hao kwa kutenga eneo la viwanda vidogo vidogo na kwa gharama za Serikali umeme utafika katika maeneo hayo na nitoe rai tu wao waendelee kujipanga kuunganisha lakini umeme utafika kama ambavyo tumeahidi katika ule mkutano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la mwisho la Mheshimiwa Frank, ni kweli Mji wa Tunduma ni mji ambao umekuwa na upo mpakani. Nataka niseme Mji wa Tunduma upo katika Mkoa mpya wa Songwe na wakati huo umeme katika Mkoa wa Songwe ulikuwa unatoka katika njia ya kusafirisha umeme ni ndefu kutoka Mbeya. Serikali ina mpango wa kujenga sub-station palepale Tunduma kwa ajili ya kuufanya Mkoa mzima wa Songwe upate nishati ya uhakika na wakati wote. Kwa hiyo, nimthibitishe Mjumbe kwa kuwa yeye Mheshimiwa Mbunge ni Mjumbe wa Kamati yetu ya Nishati na yeye pia atuunge mkono katika bajeti yetu ili mradi huu wa ujenzi wa sub-station pamoja na line ambayo inatoka Mbeya inayoenda Sumbawanga - Mpanda – Kigoma - Nyakanazi ya KV 400 ambayo yote kwa pamoja itachangia kwa upatikanaji wa umeme wa uhakika. Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana, ahsante sana.