Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 9 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 73 2018-04-13

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:-
Katika Jimbo la Tabora Mjini hasa vijiji na kata zilizopo nje ya Manispaa ikiwemo Kata ya Tumbi na vijiji vinavyoizunguka kata hiyo havijajumuishwa katika Mpango wa REA Awamu ya Tatu.
Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA katika kata na vijiji hivyo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Emanuel Adamson Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli vijiji vilivyopo nje ya Manispaa ya Tabora ikiwemo Kata ya Tumbi havikujumuishwa katika utekelezaji wa mradi wa REA III mzunguko wa kwanza. Sehemu ya vijiji katika Kata ya Tumbi ilipatiwa umeme mwaka 2006 kupitia mradi wa umeme chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden. Kwa kuwa baadhi ya vijiji vya Jimbo la Tabora Mjini viko ndani ya Manispaa ya Tabora, Serikali kupitia mradi wa Urban Electrification itaendelea kuyapelekea umeme maeneo yaliyomo katika Mamlaka za Miji, Manispaa na Majiji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mipango ya Serikali ni kuipatia umeme Kata ya Tumbi na Vijiji vilivyoizunguka Kata hiyo katika Manispaa ya Tabora kupitia mradi wa Urban Electrification. Aidha, mradi wa Urban Electrification unaofadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika utepeleka umeme katika vijiji na shule za Makunga, Mkinga, Mayeye, Shalua, Mtakuja, Chang’ombe, Itetemia, Itaga na Umanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi mwingine unaotarajiwa kutekelezwa ni densification kwa nia ya kuongeza wigo wa usambazaji umeme katika vijiji ambavyo vimefikiwa na miundombinu ya umeme. Maandalizi ya awamu ya pili ya mradi huu yanaendelea na unatarajiwa kutekelezwa kwatika mwaka wa fedha 2018/2019. Nakushukuru. (Makofi)