Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. GRACE V. TENDEGA) aliuliza:- Kesi za dawa za kulevya na upelelezi vimekuwa vikichukua muda mrefu sana na kusababisha wakati mwingine ushahidi kupotea na watuhumiwa kuachwa huru baada ya upelelezi kukamilika:- Je, kwa nini Serikali isianzishe Mahakama za Dawa za Kulevya kwenye Viwanja vya Ndege, Bandari na mipakani ili watuhumiwa wafikishwe Mahakamani punde tu ushahidi ukiwa mikononi kama zifanyavyo nchi nyingine ikiwemo India?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzetu katika nchi za nyingine Afrika Mashariki wako makini sana katika jambo hili na mashauri mengi yamekuwa yakiamuliwa kwa haraka tofauti na sisi. Kucheleweshwa kwa maamuzi ya mashauri haya kunaweza kukapelekea fikra kwamba rushwa inatumika zaidi katika kuamua haya mashauri. Sasa, je, ni lini Serikali itakamilisha huo mchakato wa kuongea na wadau ili maamuzi haya yaweze kufanyika haraka iwezekanavyo kunusuru maisha ya watoto wetu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, sheria inataka mali za watuhumiwa wa madawa ya kulevya zitaifishwe. Uwezekano wa kuzitaifisha ndani ya nchi upo, lakini ni utaratibu gani unaotumika kutaifisha mali hizi kama ziko nje ya nchi? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema katika majibu ya msingi, kinachofanyika hivi sasa ni wadau wa haki jinai ambao ni mhimili wa mahakama na pamoja na sisi upande wa Serikali kutafuta namna bora ya kuanza utekelezaji wa shughuli ya kushughulikia masuala ya kesi za madawa ya kulevya katika maeneo ya viwanja vya ndege na mipaka ya nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu jambo hilo ni la kisheria tunalifanya kwa umakini mkubwa. Hivi sasa ninavyozungumza tayari Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Dawa za Kulevya na Jaji Kiongozi Feleshi wameshaanza mazungumzo ya kuja na namna bora ya kuweza kuwa na mahakama hizi ambazo zitakuwa tembezi, ili inapotokea kwamba kuna mhalifu yeyote amekamatwa na madawa ya kulevya basi aweze kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa utaratibu ambao unakuja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ugumu unakuja kwa sababu ukiangalia kesi hizi nyingi za madawa ya kulevya zina masharti yake pia kwa maana ya kisheria. Kwa sababu ni kesi ambazo zinatakiwa zipitie hatua moja mpaka nyingine; kwa maana zinakwenda Mahakama Kuu na zikienda Mahakama Kuu maana yake ni kesi ambazo utaratibu umewekwa kwa mujibu wa sheria zianzie katika Mahakama za Mwanzo. Kwa hiyo si rahisi sana kufanya maamuzi hayo ya kiharaka, ndiyo maana tukasema kwamba kupitia utaratibu huu utarahisisha sana mashauri haya yaweze kusikilizwa kwa wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kumalizia tu nimpe taarifa Mheshimiwa Mbunge, imeanzishwa Mahakama ya Mafisadi kwa mujibu wa marekebisho ya Sheria Na.3 ya Mwaka 2016 ambayo imeonesha tija sana na mpaka hivi sasa ninapozungumza tayari kesi 7,517 zimeshaamuliwa kwa uharaka sana na tunaamini kabisa zoezi hili likikamilika basi tutaweza kuwahudumia Watanzania kwa kuhakikisha kwamba wale wahalifu wote wanakamatwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, ameuliza kuhusu namna ya utaifishaji wa hizi mali nje ya nchi. Nchi yetu imesaini makubaliano na tulishirikiana na baadhi ya nchi na tumekuwa na ushirikiano mzuri na nchi nyingi ambazo kupitia utaratibu wa makubaliano hayo, ikitokea suala la namna hiyo basi mamlaka zote mbili zinafanya kazi kuhakikisha kwamba mhusika ambaye mali zake ziko nje ya nchi pia utaratibu ufuatwe wa kisheria ili ziweze kutaifishwa.

Name

Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. GRACE V. TENDEGA) aliuliza:- Kesi za dawa za kulevya na upelelezi vimekuwa vikichukua muda mrefu sana na kusababisha wakati mwingine ushahidi kupotea na watuhumiwa kuachwa huru baada ya upelelezi kukamilika:- Je, kwa nini Serikali isianzishe Mahakama za Dawa za Kulevya kwenye Viwanja vya Ndege, Bandari na mipakani ili watuhumiwa wafikishwe Mahakamani punde tu ushahidi ukiwa mikononi kama zifanyavyo nchi nyingine ikiwemo India?

Supplementary Question 2

MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kuchelewesha haki ni kunyima haki na si kesi za madawa ya kulevya pekee kuna mashtaka ambayo watuhumiwa wakipelekwa kule ni kama wanasahauliwa. Kuna kesi za ugaidi na kuna kesi …
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujua ni kwa nini mashtaka ya kesi aina hii zinachukua muda mrefu kupelekwa mahakamani na kuhukumiwa?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA): Mheshimiwa Mwenyekiti, katika utaratibu wa makosa yote ya kijinai na kwa mujibu wa Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, Sura ya 20 umewekwa utaratibu wa namna gani kesi hizi zishughulikiwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kesi hizi zinahitaji umakini mkubwa sana, si rahisi kwa namna yoyote ile kuziharakisha pasipokuwa uchunguzi wake umekamilika. Ndiyo maana nawaomba Waheshimiwa Wabunge waendelee kuvuta subira mamlaka zetu zinafanya kazi sasa hivi kuhakikisha kwamba kesi zinapungua na Mahakama imeweka utaratibu wa kuhakikisha kwamba kesi nyingi zinasikilizwa kwa wakati ili haki ionekane imetendeka.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. GRACE V. TENDEGA) aliuliza:- Kesi za dawa za kulevya na upelelezi vimekuwa vikichukua muda mrefu sana na kusababisha wakati mwingine ushahidi kupotea na watuhumiwa kuachwa huru baada ya upelelezi kukamilika:- Je, kwa nini Serikali isianzishe Mahakama za Dawa za Kulevya kwenye Viwanja vya Ndege, Bandari na mipakani ili watuhumiwa wafikishwe Mahakamani punde tu ushahidi ukiwa mikononi kama zifanyavyo nchi nyingine ikiwemo India?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Diwani wa Kata ya Mihingo Mheshimiwa Nyambula Nyamhanga yuko lockup miezi sita sasa kwa kosa la uchochezi. Naomba kupata ufafanuzi wa Serikali, ni njia gani tuitumie huyu Diwani apate dhamana, kwa hiyo kesi ya uchochezi kwa sababu ana miezi sita yuko gerezani bila kupata dhamana? (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu jambo alilolisemea Mheshimiwa Mbunge ni mahsusi na kwa mujibu wa sheria kuna makosa yenye dhamana na kuna makosa yasiyo na dhamana; nimwombe tu Mheshimiwa Mbunge tuje tuliongee. Pia nimpongeze kwa kufuatilia sana masuala ya wapiga kura wake. Kama ni jambo ambalo lina dhamana maana yake taratibu tu za dhamana zitafuata ili ziweze kukamilika na Mheshimiwa Diwani aweze kupata dhamana. Mara zote yale makosa yasiyo na … (Makofi)

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. GRACE V. TENDEGA) aliuliza:- Kesi za dawa za kulevya na upelelezi vimekuwa vikichukua muda mrefu sana na kusababisha wakati mwingine ushahidi kupotea na watuhumiwa kuachwa huru baada ya upelelezi kukamilika:- Je, kwa nini Serikali isianzishe Mahakama za Dawa za Kulevya kwenye Viwanja vya Ndege, Bandari na mipakani ili watuhumiwa wafikishwe Mahakamani punde tu ushahidi ukiwa mikononi kama zifanyavyo nchi nyingine ikiwemo India?

Supplementary Question 4

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa miongoni mwa sababu zinazochangia kuchelewa kwa kesi hizi ni vidhibiti kutopelekwa maabara kwa Mkemia Mkuu haraka ili kuthibitisha. Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto hii?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa marekebisho ya sheria yaliyofanyika mwaka 2017, hivi sasa Sheria ya Udhibiti wa Dawa za Kulevya Kifungu cha 4(n) ambacho kimeongezewa baada ya marekebisho kimeweka utaratibu wa kwamba hivi sasa kwa kuzingatia kwamba kuna mashauri mengi ambayo yanasimama kwa kusubiri vidhibiti kutoka katika Ofisi ya Mkemia Mkuu, sasa kupitia sheria hii imeanzishwa laboratory katika Ofisi ya Kamishna Jenerali ili kuhakikisha kwamba mamlaka pia nayo iwe na wajibu huo wa kuchunguza na kutoa taarifa ili kujaribu kusaidia expedite kesi hizi zisichukue muda mrefu sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimwondolee hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ilichukua hatua kwa marekebisho hayo ya sheria na hivi sasa ukiacha Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Jeshi la Polisi lakini... kazi hiyo pia.