Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 60 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 509 2018-06-28

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. GRACE V. TENDEGA) aliuliza:-
Kesi za dawa za kulevya na upelelezi vimekuwa vikichukua muda mrefu sana na kusababisha wakati mwingine ushahidi kupotea na watuhumiwa kuachwa huru baada ya upelelezi kukamilika:-
Je, kwa nini Serikali isianzishe Mahakama za Dawa za Kulevya kwenye Viwanja vya Ndege, Bandari na mipakani ili watuhumiwa wafikishwe Mahakamani punde tu ushahidi ukiwa mikononi kama zifanyavyo nchi nyingine ikiwemo India?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Katiba wa Sheria, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Grace Victor Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la uanzishwaji wa mahakama katika kushughulikia aina fulani ya makosa, ni suala la kisheria linalohitaji ushirikishwaji mkubwa wa wadau wote husika wa haki jinai (criminal justice). Kwa kutambua hilo, Serikali imeshaanza mazungumzo ya awali na wadau hao wa haki jinai, ukiwemo mhimili wa Mahakama ili kuona uwezekano wa kusikiliza mashauri ya watuhumiwa wa dawa za kulevya wanaokamatwa katika maeneo ya viwanja vya ndege, bandarini na maeneo mengine ya mipaka ya nchi, kwa kutumia Mahakama zinazotembea (mobile courts).
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, nawaomba Waheshimiwa Wabunge wawe na subira wakati Serikali ikijadiliana na wadau wa haki jinai kuhusiana na suala hilo.