Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vedasto Edgar Ngombale Mwiru

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. VEDASTO EDGA NGOMBALE (KILWA KASKAZINI) aliuliza:- Kupata habari ni moja ya haki za Kiraia, TBC ni chombo pekee cha habari kwa sasa kinachowafikia wananchi wengi hususan wale wanaoishi vijijini lakini kwa muda mrefu sasa chombo hicho hakisikiki vizuri katika maeneo mengi ya vijijini vya Jimbo la Kilwa Kaskazini na Wilaya ya Kilwa kwa ujumla. Je, ni tatizo gani linalosababisha chombo hiki kisisikike vizuri katika maeneo mengi ya vijijini?

Supplementary Question 1

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kwa kuwapongeza community redio ya Mashujaa FM kwa kufanya coverage kwa niaba ya TBC.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa katika bajeti ya mwaka 2016/2017 Serikali ilitenga hiyo bajeti ya kujenga mtambo Nangurukuru, mwaka 2017/2018 na hii 2018/2019 imerudia kuwa inaendelea kutenga bajeti bila ya utekelezaji. Sasa nini commitment ya Serikali katika bajeti ya mwaka huu kwa sababu inaonekana kana kwamba Serikali haina nia thabiti ya kujenga mtambo huo?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa TBC ndio chombo cha Taifa na kina jukumu la kutoa mawasiliano kwa wananchi, kutokana na kusua sua kwake Mheshimiwa Waziri haoni kwamba wanawakosesha haki wananchi wa Kilwa kupata habari? Lakini pia…

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza ameonesha wasiwasi kwamba TBC inasuasua katika utekelezaji wa usikivu hususan katika Wilaya yake ya Kilwa. Kwanza napenda kutumia nafasi hii kumtoa hofu Mheshimiwa Mbunge kwa sababu zifuatazo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, sababu ya kwanza, wote tunafahamu kwamba katika bajeti ya fedha ya mwaka WA 2017/2018 Serikali ilitenga shilingi bilioni tatu kwa ajili ya kuboresha usikivu wa TBC na fedha hiyo ilishatolewa yote. Katika bajeti ya mwaka huu wa fedha 2018/2019 Serikali imetenga bajeti ya shilingi bilioni tano. Kwa hiyo tuna imani kabisa fedha hiyo itatolewa yote kwa sababu imekuwa ni mpango wa Serikali na tumeona kabisa Serikali ina commitment na ndiyo maana katika fedha zote ambazo zinatengwa zimeendelea kutolewa kama inavyotakiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili, kwamba TBC kusuasua kwake kunawakosesha haki wananchi, nimtoe hofu kama ambavyo tumejibu katika jibu letu la msingi, kwamba katika mwaka huu wa fedha wa 2018/2019 Serikali kupita shirika lake la TBC imejipanga kujenga mnara mpya wa kurushia matangazo yake katika eneo la Nangurukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tunaamini kabisa na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge mimi kama Naibu Waziri pamoja na Waziri wangu tutawasimamia katika mwaka huu wa fedha kuhakikisha kwamba mtambo huo unajengwa, ili basi wananchi wa Kilwa waweze kupata haki yao ya kuweza kupata habari, ahsante.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. VEDASTO EDGA NGOMBALE (KILWA KASKAZINI) aliuliza:- Kupata habari ni moja ya haki za Kiraia, TBC ni chombo pekee cha habari kwa sasa kinachowafikia wananchi wengi hususan wale wanaoishi vijijini lakini kwa muda mrefu sasa chombo hicho hakisikiki vizuri katika maeneo mengi ya vijijini vya Jimbo la Kilwa Kaskazini na Wilaya ya Kilwa kwa ujumla. Je, ni tatizo gani linalosababisha chombo hiki kisisikike vizuri katika maeneo mengi ya vijijini?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza nitoe shukurani kwa Wizara hii kwa sababu wametujengea mtambo katika eneo letu la Kwemashai kule Lushoto; lakini bado usikivu haupo vizuri. Sasa, je, ni lini Serikali itahakikisha kwamba usikivu wa TBC katika Wilaya ya Lushoto na leo wenyewe wapo hapa wamekuja kufuatilia jambo hili utakuwa na usikivu unaoeleweka?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa napenda kumpongeza Mheshimiwa Rashid Shangazi kwa sababu yeye amekuwa ni mdau mkubwa wa TBC ndani ya Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania. Hata hivyo, kama ambavyo ametoa pongezi na mimi kwa niaba ya Serikali napenda kupokea pongezi hizo, kwamba TBC sasa hivi tumekwisha kuweza kujenga Mtambo katika Wilaya yake ya Lushoto.
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto kubwa ambayo ipo katika Wilaya hiyo ya Lushoto ambayo inasababisha usikivu kutokuwa mzuri ni kwamba mitambo hii inapofungwa lazima kuwe kuna muda kidogo wa kuweza kufanyia maboresho. Kwa hiyo, nichukue nafasi hii kuweza kumhakikishia Mheshimiwa Shangazi, pamoja na wananchi wote wa Wilaya ya Lushoto ambao wapo ndani ya Bunge hili, kwamba ndani ya miezi miwili nilishaongea na Mkurugenzi wa TBC ameniahidi kwamba atatuma timu yake ya wataalam kwenda kufanya maboresho katika mtambo huo ili basi usikivu wa TBC uwe mzuri. Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. VEDASTO EDGA NGOMBALE (KILWA KASKAZINI) aliuliza:- Kupata habari ni moja ya haki za Kiraia, TBC ni chombo pekee cha habari kwa sasa kinachowafikia wananchi wengi hususan wale wanaoishi vijijini lakini kwa muda mrefu sasa chombo hicho hakisikiki vizuri katika maeneo mengi ya vijijini vya Jimbo la Kilwa Kaskazini na Wilaya ya Kilwa kwa ujumla. Je, ni tatizo gani linalosababisha chombo hiki kisisikike vizuri katika maeneo mengi ya vijijini?

Supplementary Question 3

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Swali kama hili ambalo Mheshimiwa Ngombale leo ameuliza, nililiuliza mimi 2016 na majibu yalikuwa haya haya. Sasa Mheshimiwa Naibu Waziri Mkoa wa Lindi usikivu wa TBC ni tatizo sana, naomba commitment ya Mheshimiwa Naibu Waziri kama alivyotoa wakati anajibu kwa Mheshimiwa Ngombale; kwamba katika mwaka huu wa fedha huo mnara aliosema utajengwa ili Watanzania wanaomsikia wajue kwamba Serikali imeji-commit ndani ya Bunge.

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA HABARI UTAMADUNI SANAA NA MICHEZO:
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Naibu Waziri kwa majibu mazuri aliyoyatoa ambayo ameyatoa kwa maswali aliyoulizwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kumjibu Mheshimiwa Bobali kwamba, kwanza si sahihi kusema kwamba eti majibu tuliyotoa sasa ndio majibu tuliyotoa kipindi kilichopita miaka miwili iliyopita wakati kuna miradi tayari tumeitekeleza mwaka huu na mwaka jana. Ni kichekesho, sasa sisi tumekuwa waganga wa kienyeji kwamba tumetekeleza hayo mambo mwaka huu..
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge awe na imani na Serikali yetu, kwamba tumehakikisha kwamba katika mwaka 2018/2019 mradi wa kujenga mtambo wa FM kurusha matangazo eneo la Nangurukuru utatekelezwa.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. VEDASTO EDGA NGOMBALE (KILWA KASKAZINI) aliuliza:- Kupata habari ni moja ya haki za Kiraia, TBC ni chombo pekee cha habari kwa sasa kinachowafikia wananchi wengi hususan wale wanaoishi vijijini lakini kwa muda mrefu sasa chombo hicho hakisikiki vizuri katika maeneo mengi ya vijijini vya Jimbo la Kilwa Kaskazini na Wilaya ya Kilwa kwa ujumla. Je, ni tatizo gani linalosababisha chombo hiki kisisikike vizuri katika maeneo mengi ya vijijini?

Supplementary Question 4

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Mkoa wa Katavi usikivu wa TBC sio mzuri kabisa na baadhi ya maeneo hawasikii matangazo ya aina yoyote na hutumia matangazo ya nchi jirani. Je, ni lini Serikali italeta mtambo kwenye Mkoa wa Katavi ili wananchi waweze kupata huduma ya TBC?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 ipo mikoa mitano ambayo ipo kwenye bajeti. Mikoa hiyo ni mikoa mipya ukiwemo Mkoa wa Songwe, Mkoa wa Simiyu, Mkoa wa Katavi, Zanzibar pamoja na Mkoa wa Njombe. Kwa hiyo nichukue nafasi hii kuweza kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mwaka huu wa fedha 2018/2019, Mkoa wa Katavi upo kwenye mpango na tunamhakikishia kwamba usikivu wa TBC katika Mkoa wake utaboreshwa. Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. VEDASTO EDGA NGOMBALE (KILWA KASKAZINI) aliuliza:- Kupata habari ni moja ya haki za Kiraia, TBC ni chombo pekee cha habari kwa sasa kinachowafikia wananchi wengi hususan wale wanaoishi vijijini lakini kwa muda mrefu sasa chombo hicho hakisikiki vizuri katika maeneo mengi ya vijijini vya Jimbo la Kilwa Kaskazini na Wilaya ya Kilwa kwa ujumla. Je, ni tatizo gani linalosababisha chombo hiki kisisikike vizuri katika maeneo mengi ya vijijini?

Supplementary Question 5

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Ludewa kijiogrofia ni tambarare, milima na mabonde na kwa maeneo mengi inayosikika inasikika Redio Malawi. Je, ni lini TBC itasikika maeneo ya Ludewa yote?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimeshajibu kwamba, katika mwaka wa fedha 2018/2019 TBC imetengewa bajeti ya shilingi bilioni tano. Kati ya mikoa ambayo itashughulikiwa ni Mkoa wa Njombe. Kwa sababu natambua kabisa kwamba Wilaya ya Ludewa ipo ndani ya Mkoa wa Njombe, kwa hiyo, ni hakika kabisa kwamba TBC ndani ya mwaka huu wa fedha itaweza kusikika na maboresho makubwa yatafanyika katika Wilaya hiyo ya Ludewa pamoja na Mkoa mzima wa Njombe.