Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 59 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 501 2018-06-27

Name

Vedasto Edgar Ngombale Mwiru

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. VEDASTO EDGA NGOMBALE (KILWA KASKAZINI)
aliuliza:-
Kupata habari ni moja ya haki za Kiraia, TBC ni chombo pekee cha habari kwa sasa kinachowafikia wananchi wengi hususan wale wanaoishi vijijini lakini kwa muda mrefu sasa chombo hicho hakisikiki vizuri katika maeneo mengi ya vijijini vya Jimbo la Kilwa Kaskazini na Wilaya ya Kilwa kwa ujumla.
Je, ni tatizo gani linalosababisha chombo hiki kisisikike vizuri katika maeneo mengi ya vijijini?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Vedasto Edga Ngombale, Mbunge wa Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeshaanza kuchukua hatua mahsusi za kuboresha usikivu wa Redio katika Mikoa ya Lindi pamoja na Mtwara, ikiwemo Wilaya ya Kilwa kama ifuatavyo:-
(a) Mitambo ya kurushia matangazo iliyoko Nachingwea ya TBC Taifa imeongezewa nguvu kutoka watt 250 hadi watt 1,000 na ile ya TBC FM toka watt 150 hadi watt 1,000. Matokeo yake ni usikivu bora wa redio maeneo mengi ya Nachingwea, Ruangwa na sehemu za Wilaya ya Masasi.
(b) Mitambo miwili ya kurushia matangazo ya TBC Taifa na TBC FM imejengwa Mtwara, kila mmoja una ukubwa wa watt 1,000 na kuwezesha matangazo ya redio kuwafikia wananchi Mtwara Vijijini, Tandahimba pamoja na Lindi Vijijini.
(c) Hatua ya tatu ni ndani ya mwaka wa fedha 2018/2019 tuna mradi wa kujenga Mtambo mpya wa FM wa kurusha matangazo eneo la Nangurukuru ambao utaimarisha usikivu wa redio maeneo ya milima yaliyobaki.