Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO aliuliza:- Katika Wilayani Tunduru kulikuwa na Kambi ya Jeshi ambayo pamoja na mambo mengine ilishughulika na ulinzi katika Vijiji vya Wenje na Makande vilivyopo mpakani na Nchi ya Msumbiji:- i. Je, Serikali halioni haja ya kurudisha Kambi hiyo ya Jeshi Wilayani Tunduru? ii. Kambi iliyokuwepo ilikuwa na hekta za ardhi zisizopungua 18,000, je, Serikali ina mpango gani wa kuendeleza maeneo hayo ambayo sasa yamekuwa vichaka?

Supplementary Question 1

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Jeshi la Wananchi liliweka kambi katika Vijiji vya Wenje na Makande kwa ajili ya kuimarisha ulinzi katika mipaka yetu na kama inavyofahamika kwamba Wilaya ya Tunduru ni miongoni mwa Wilaya zilizoko mpakani mwa Msumbiji. Je, Serikali haioni sasa wakati umefika wa kurudisha kambi katika maeneo yale ili kuendeleza ulinzi kama ilivyokusudiwa awali?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, hivi karibuni Serikali imetangaza halmashauri ya mji katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru; kutangaza halmashauri ya mji ni wazi kwamba tunaongeza maeneo ya utawala. Kuongeza maeneo ya utawala ni wazi pia kwamba idadi ya watu inaongezeka. Je, nini sasa kauli ya Serikali katika kuandaa mpango huo rasmi wa kukabidhi maeneo yale ya Kitanda katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ili wananchi sasa wapate kuyaendeleza maeneo yale? Ahsante sana.

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI (K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kuwa anafuatilia sana jambo hili. Niseme tu Mikoa ya Kusini ikiwemo Mtwara na Ruvuma, Kamati za Ulinzi na Usalama zilishafanya maombi ya uimarishwaji wa masuala ya kiulinzi mpakani. Kwa kuwa wamefanya maombi hayo, mawasiliano yanaendelea kufanyika kuona namna bora ya kuimarisha ulinzi huko mipakani. Jambo litakalokuwa limeamuliwa Kamati za Ulinzi na Usalama pamoja na Waheshimiwa Wabunge kwa kuwa wanafuatilia wataweza kujulishwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili aliloliuliza, nisema tu kama ambavyo nimejibu kwenye jibu la msingi kwamba Jeshi la Kujenga Taifa pamoja na Jeshi la Wananchi watatuma timu ya wataalam. Wakishamaliza kufanyia vipimo kwa kushirikiana na halmashauri wataweka matumizi bora ya ardhi na kuweza kukidhi kile alichokisemea kuhusu ongezeko la watu pamoja na uwepo wa halmashauri ya mji.

Name

Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO aliuliza:- Katika Wilayani Tunduru kulikuwa na Kambi ya Jeshi ambayo pamoja na mambo mengine ilishughulika na ulinzi katika Vijiji vya Wenje na Makande vilivyopo mpakani na Nchi ya Msumbiji:- i. Je, Serikali halioni haja ya kurudisha Kambi hiyo ya Jeshi Wilayani Tunduru? ii. Kambi iliyokuwepo ilikuwa na hekta za ardhi zisizopungua 18,000, je, Serikali ina mpango gani wa kuendeleza maeneo hayo ambayo sasa yamekuwa vichaka?

Supplementary Question 2

MHE. ALHAJ ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kutokana na swali la msingi naomba kuuliza Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, wananchi wa Makoko katika mji wa Musoma waliachia eneo wananchi 95 mwaka 1982 mpaka leo ni miaka 36 hawajalipwa haki yao ya bilioni 1.4 Serikali inatoa tamko gani kwa wananchi hao? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI (K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Bulembo kwa sababu amelisemea jambo mahususi ambalo linahusu fidia, niseme tu nimelipokea na nitalishughulikia kujua status yake kwa maana ya jambo ambalo linahusisha fidia ili kuweza kujua kama tathmini na masuala yote ya uhakiki yalishafanyika na kama inastahili kutakiwa kulipwa.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO aliuliza:- Katika Wilayani Tunduru kulikuwa na Kambi ya Jeshi ambayo pamoja na mambo mengine ilishughulika na ulinzi katika Vijiji vya Wenje na Makande vilivyopo mpakani na Nchi ya Msumbiji:- i. Je, Serikali halioni haja ya kurudisha Kambi hiyo ya Jeshi Wilayani Tunduru? ii. Kambi iliyokuwepo ilikuwa na hekta za ardhi zisizopungua 18,000, je, Serikali ina mpango gani wa kuendeleza maeneo hayo ambayo sasa yamekuwa vichaka?

Supplementary Question 3

MHE. SUSAN A. LYMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa mwaka 1994 Serikali ilifuta ile kwenda jeshini watoto wanaomaliza kidato cha sita kwa lazima na moja ya sababu hiyo ilikuwa ni pamoja na ukosefu wa fedha. Sasa hivi nchi yetu ina fedha na nikikukumbuka maneno ya Mheshimiwa Profesa Kabudi alisema nyumba yenye fedha ndio inaingiliwa na wezi. Sasa je, Serikali haioni kwa kuwa sasa tuna fedha nyingi, fedha hizo zitumike kupeleka wanafunzi wote wanaomaliza kidato cha sita kwenda jeshini ili kuwajengea ujasiri, ukakamavu na uzalendo?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI (K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo aliloliuliza Mheshimiwa Mbunge hata sasa linafanyika mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sharia yalisharejeshwa na hivi ambavyo yanafanyika kufuatana na utaratibu wa kwenye makambi ambayo yanaendesha mafunzo hayo. Kutokana na bajeti zilivyotengwa idadi ya wanafunzi na wale wanaoenda kwa mujibu pamoja na wale wanaoenda kujitolea itaendelea kuongezea mwaka hadi mwaka. (Makofi)

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO aliuliza:- Katika Wilayani Tunduru kulikuwa na Kambi ya Jeshi ambayo pamoja na mambo mengine ilishughulika na ulinzi katika Vijiji vya Wenje na Makande vilivyopo mpakani na Nchi ya Msumbiji:- i. Je, Serikali halioni haja ya kurudisha Kambi hiyo ya Jeshi Wilayani Tunduru? ii. Kambi iliyokuwepo ilikuwa na hekta za ardhi zisizopungua 18,000, je, Serikali ina mpango gani wa kuendeleza maeneo hayo ambayo sasa yamekuwa vichaka?

Supplementary Question 4

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali moja la nyongeza. Bajeti inayomalizika hivi sasa ya 2017/2018, kulikuwa na tathmini ya fidia juu ya maeneo ambayo ya jeshi yalichukuliwa kwa wananchi, bilioni 27 na eneo mahususi Jimbo la kilwa masoko la Mheshimiwa Bwege na linaloitwa Rasi Mshindo, Mtaa wa Mpala ni eneo muhimu nyeti ambalo Jeshi wanataka kufanyia kazi kwa ajili ya shughuli zao. Je, nini mkakati wa Serikali kuweza kulipa kwa dharura eneo la Rasi Mshindo, Mtaa wa Mpala, Kilwa Masoko? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI (K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Masoud ni mjumbe Veterani kwenye Kamati inayosimamia Wizara hizi. Mapendekezo yaliyoletwa na Mheshimiwa Waziri yalikubaliwa na Bunge hili bila hata shilingi moja kushikwa. Niseme tu kwa sababu ndio tunamaliza bajeti tumpe tu Mheshimiwa Waziri muda wa kwenda kuyatekeleza hayo na haya yote ambayo ya kipaumbele kama ambavyo Mjumbe wa Kamati amesema yatapewa uzito unaostahili.