Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 56 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 475 2018-06-22

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO aliuliza:-
Katika Wilayani Tunduru kulikuwa na Kambi ya Jeshi ambayo pamoja na mambo mengine ilishughulika na ulinzi katika Vijiji vya Wenje na Makande vilivyopo mpakani na Nchi ya Msumbiji:-
i. Je, Serikali halioni haja ya kurudisha Kambi hiyo ya Jeshi Wilayani Tunduru?
ii. Kambi iliyokuwepo ilikuwa na hekta za ardhi zisizopungua 18,000, je, Serikali ina mpango gani wa kuendeleza maeneo hayo ambayo sasa yamekuwa vichaka?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI (K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Wziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sikudhani Chikambo kama ifautavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Ulinzi wananchi wa Tanzania liliweka kituo cha ulinzi cha Kombania ya sita ya 691 kikosi cha Jeshi (06/691 KJ) katika eneo la Chitanda, Wilayani Tunduru. Kutokana na sababu ambazo zilikuwa za msingi kwa wakati huo kituo hicho kilifungwa na eneo hilo likarudishwa rasmi kwa uongozi wa Serikali ya Wilaya ya Tunduru mwaka 1998. Aidha, mwaka 2006 eneo hilo liliombwa upya na JWTZ kwa uongozi wa Mkoa wa Ruvuma kwa ajili ya kuendelea kulitumia katika kuimarisha ulinzi na usalama wa nchi yetu katika eneo hilo.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa pamoja na Makao Makuu ya Jeshi linaandaa mpango kwa kutumia wataalam wake kuwatuma kwenda Wilayani Tunduru kwa kushirikiana na uongozi wa Wilaya ya Tunduru kutathmini na kulipima upya eneo hilo na kulifanyia mchakato wa kulimiliki kwa misingi ya sheria za ardhi zilizopo.