Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Mkoa wa Tabora ni moja kati ya mikoa inayokabiliwa na tatizo kubwa la ndoa za utotoni na kusababisha watoto wengi wa kike kushindwa kumaliza elimu ya msingi au ya sekondari. Aidha, hivi karibuni Serikali ilikata rufaa juu ya ndoa za utotoni ikitaka iruhusiwe watoto wa kike kuolewa na umri kuanzia miaka 14 ambapo hii ni kinyume cha Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009:- Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia watoto wa kike wa Mkoa wa Tabora angalau wengi waweze kwenda kupata elimu ya msingi na sekondari kwa kupunguza ndoa za utotoni?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru Serikali imetoa majibu kwamba na wamekiri kwamba kweli sheria ya mtoto ya kuolewa kwa maiaka 15 ipo na inaendelea kuwepo na wanasema kwamba wanataka kumlinda mtoto huyu asiolewe akiwa na umri huo wakati sheria inasema kwamba anaweza kuolewa akiwa na umri huo. Mkoa wa Tabora ni moja kati ya mikoa ambayo ndoa nyingi za utotoni na watoto kujifungua watoto wenzao wakiwa na umri mdogo na kusababisha vifo vingi vya watoto. Serikali ina mpango gani wa kuibadilisha sheria hii ili watoto hawa waweze kuendelea na masomo yao kisheria? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, asilimia 63 ya wanaoathirika na ndoa za utotoni ni watoto wa kike, kesi nyingi zimekuwepo mahakamani kuhusiana na suala hili, lakini kutokana na sheria kuwepo ya watoto kuolewa na umri wa miaka 15 wanaofanya makosa hayo wamekuwa hawaadhibiwi kwa sababu sheria haisemi ni adhabu gani wanaweza wakapatiwa, Serikali inasemaje kuhusiana na suala hili ili kunusuru watoto wetu wanaolewa wakiwa na umri mdogo? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA) : Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali la kwanza amezungumza kuhusu mkinzano na kuitaka Serikali kubadilisha sheria. Suala hili limekwishazungumzwa sana na Serikali mkishatoa maelezo yake na ikumbukwe kwamba yalitolewa maamuzi ya kesi Na.5 ya mwaka 2016 ambayo ni kesi kati ya Rebeka Jumi dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Serikali imekata rufaa, kwa hiyo tunasubiri maamuzi ya kesi hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa uchache anachokisema Mheshimiwa Mbunge kama mkinzano, mkinzano huu haupo kwa sababu suala la umri, umri wa mtoto unatafsiri katika sheria tofauti na katika maeneo tofauti. Kuna umri biological, kuna umri contextual na kuna umri situational.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndio maana tunasema hapa katika sheria zetu hizi sheria ambayo anahisi yeye inakinzana hakuna upinzani wowote, Kwa sababu mwanafunzi yoyote ambaye yuko shuleni ambaye akipata ujauzito pale Hatuangalii biological age yake tunaangalia umri wa muktadha, ndio maana tunasema hata kama akiwa yupo form six ana miaka 18 akipewa ujauzito sheria ambayo tulifanya wenyewe marekebisho hapa Bungeni ukienda kwenye Sheria ya Elimu ya mwaka 1978 kifungu imeongezwa kifungu cha 60A imeweka adhabu ya kwamba mtu anayefanya akosa hilo adhabu yake ni miaka 30. Kwa hiyo hakuna mkinzano katika eneo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la pili, Mheshimiwa Mbunge amezungumza kuhusu Serikali ifute sheria na amesema kwa sababu ndio sehemu pekee ya kuweza kulinda haki ya mtoto wa kike hasa katika eneo ambalo ametokea yeye kutokana na kwamba kulikuwa na idadi kubwa sana ya watoto ambao wanapata ujauzito na akasema ni sheria gani ambayo inamchukulia hatua mtu huyu ambaye anafanya kosa hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria hii imesema dhahiri kabisa ukienda kwenye Sheria Na. 21 ya mwaka 2009, sheria ambayo inalinda haki ya mtoto imezungumza juu ya kosa hilo la mtu yoyote ambaye anatenda kosa la kuzuia haki ya mtoto, baadaye sheria hiyo inaweza kuchukua mkondo na kuhakikisha kwamba mtu huyo anatiwa katika mikono ya sheria. Kwa hiyo, nimwondoe hofu Mheshimiwa kwamba si kweli kwamba Serikali hatu fahamu na hatulindi haki za mtoto na ndio maana tumechukua hatua mbalimbali kuhakikisha kwamba tunalinda haki ya mtoto na watupe muda tuendelee kufanyia kazi suala hili. (Makofi)

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Mkoa wa Tabora ni moja kati ya mikoa inayokabiliwa na tatizo kubwa la ndoa za utotoni na kusababisha watoto wengi wa kike kushindwa kumaliza elimu ya msingi au ya sekondari. Aidha, hivi karibuni Serikali ilikata rufaa juu ya ndoa za utotoni ikitaka iruhusiwe watoto wa kike kuolewa na umri kuanzia miaka 14 ambapo hii ni kinyume cha Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009:- Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia watoto wa kike wa Mkoa wa Tabora angalau wengi waweze kwenda kupata elimu ya msingi na sekondari kwa kupunguza ndoa za utotoni?

Supplementary Question 2

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, Nimemsikiliza vizuri Mheshimiwa Naibu wakati akijibu swali nilikuwa nataka nimuulize tu ikitokea mwanafunzi wa kiume akamchukua Mwalimu wa kike sheria inasemaje?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Sheria ya Elimu ya Mwaka 1978 na kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002, Sura ya 353 imezungumza katika kifungu cha 60A(2) kwamba ni kosa pia kwa mtoto wa kiume yeyote ambaye yuko shule kuoa. Kwa hiyo, kosa linabaki pale pale na kwa upande wa wanaume imezungumza kama ni kosa, kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge Mheshimiwa Ndassa bado inabaki pale pale mtoto wa kiume pia na yeye akioa akiwa bado yuko shuleni ni kosa pia.

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Mkoa wa Tabora ni moja kati ya mikoa inayokabiliwa na tatizo kubwa la ndoa za utotoni na kusababisha watoto wengi wa kike kushindwa kumaliza elimu ya msingi au ya sekondari. Aidha, hivi karibuni Serikali ilikata rufaa juu ya ndoa za utotoni ikitaka iruhusiwe watoto wa kike kuolewa na umri kuanzia miaka 14 ambapo hii ni kinyume cha Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009:- Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia watoto wa kike wa Mkoa wa Tabora angalau wengi waweze kwenda kupata elimu ya msingi na sekondari kwa kupunguza ndoa za utotoni?

Supplementary Question 3

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Watoto wakike wengi wanaoshindwa kuendelea na masomo baada ya kumaliza kidato cha nne na cha sita wanaolewa kwa kukosa fursa ya kujifunza katika vyuo vyetu vya ufundi. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuanzisha kambi la vijana ili hawa watoto wanaomaliza kidato cha nne wakiwa wadogo na hawaruhusiwi wakiwa chini ya miaka 14 au wakiwa na miaka 14 wakajifunze shughuli za ufundi, ufugaji bora wakajifunze ujasiriamali na mambo mengine?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA) : Mheshimiwa Mwenyekiti, ofisi ya Waziri Mkuu ina program ya ukuzaji ujuzi nchini ambao lengo lake kubwa ni kuhakikisha tunaisadia nguvu kazi yetu hasa vijana wengi kupata fursa ya kujifunza kwa vitendo hasa katika mafunzo mbalimbali ya ufundi. Program hii inaendelea na mpaka ninavyozungumza hivi sasa takribani vijana 22,000 nchi nzima wameshawasilisha maombi. Kwa hiyo, ni program ambayo inawagusa watu tofauti tofauti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba ni program endelevu mpaka mwaka 2021 tutaendelea kuwachukua watoto wengi hasa wa kike kuingia kwenye program hii kujifunza ili waweze kujitegemea. (Makofi)

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Mkoa wa Tabora ni moja kati ya mikoa inayokabiliwa na tatizo kubwa la ndoa za utotoni na kusababisha watoto wengi wa kike kushindwa kumaliza elimu ya msingi au ya sekondari. Aidha, hivi karibuni Serikali ilikata rufaa juu ya ndoa za utotoni ikitaka iruhusiwe watoto wa kike kuolewa na umri kuanzia miaka 14 ambapo hii ni kinyume cha Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009:- Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia watoto wa kike wa Mkoa wa Tabora angalau wengi waweze kwenda kupata elimu ya msingi na sekondari kwa kupunguza ndoa za utotoni?

Supplementary Question 4

MHE. MARYAM S. MSABAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kumuuliza Naibu Waziri suala dogo la nyongeza. Kwa kuwa kuna watu wazima ambao wana akili zao timamu na wana kazi zao, lakini wamekuwa wakikiuka maadili na kuwachukua hawa mabinti wakiwa katika umri mdogo na sana kuwazalisha watoto na kuongeza ongezeko la watoto wa mitaani. Je, Serikali ina mikakati gani kuchukua sheria na mikakati ili kuhakikisha tunakomesha vitendo hivi na hawa watoto wa kike kupata haki zao stahiki?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA) : Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa sheria imeeleza vyema ni katika mazingira gani mtoto wa kike anaweza kuolewa na kinyume chake maana yake ni kosa linatengenezwa. Kwa hiyo, kwa wale wote ambao wanafanya vitendo hivyo vya kukiuka sheria, sheria zetu zipo, watachukuliwa hatua na kupelekwa kwenye vyombo vya sheria ili haki ionekane imetendeka kwa mtoto huyu ambaye anakuwa amekatishwa shughuli mbalimbali ikiwemo masomo.