Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:- Shule za Sekondari za Farkwa na Msakwalo zilizoko Wilayani Chemba zimepandishwa hadhi kuwa za A – level na idadi ya wanafunzi imeongezeka katika shule hizo:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuzipatia maji ya uhakika shule hizo ili kuwaondolea wanafunzi adha ya kutafuta maji badala ya masomo?

Supplementary Question 1

MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Serikali, nina swali moja tu la nyongeza. Kwanza nitumie fursa hii kumpongeza sana Waziri wa Elimu, Profesa Ndalichako, Naibu wake na watendaji wote wa Wizara kwa juhudi walizochukua za kuhakikisha kwamba shule hizi za Msakwalo na Farkwa zinapata maji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu ni moja tu kwamba katika Shule za Sekondari za Mondo na Soya ambazo nazo ni shule za A-Level zilizopo katika Wilaya ya Chemba, wanafunzi wanatembea umbali mrefu kutafuta maji. Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba wanafunzi na walimu wa shule hizi wanapata maji ya uhakika?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI, kaka yangu Mheshimiwa Kakunda kwa majibu mazuri, lakini sisi Wizara ya Maji tunatambua umuhimu wa elimu. Kupitia elimu mtoto wa mama ntilie anaweza kuwa Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Sisi kama Wizara ya Maji katika bajeti hii tumewatengea Chemba Sh.1,468,000,000. Labda nimuagize Mhandisi wa Maji wa Chemba aone umuhimu sasa kwa shule ambazo ameziorodhesha Mheshimiwa Mbunge wa kuhakikisha wanapata maji safi, salama na yenye kuwatosheleza.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:- Shule za Sekondari za Farkwa na Msakwalo zilizoko Wilayani Chemba zimepandishwa hadhi kuwa za A – level na idadi ya wanafunzi imeongezeka katika shule hizo:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuzipatia maji ya uhakika shule hizo ili kuwaondolea wanafunzi adha ya kutafuta maji badala ya masomo?

Supplementary Question 2

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, hali ilivyo Chemba inafanana vilevile na kule Mkinga. Tunaishukuru Serikali katika kipindi hiki imetuwezesha kuanzisha sekondari za kidato cha tano na sita kwa Shule ya Mkinga Leo na Maramba Sekondari. Shule hizi zinakabiliwa na tatizo kubwa sana la maji na kukamilika kwa vyumba vya madarasa na mabweni. Je, nini kauli ya Serikali kuwezesha kukamilika kwa nia njema hii ya kuwa na sekondari za A-Level ili ziweze kutoa elimu stahiki kama walivyokusudia?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda sana nimpongeze Mheshimiwa Jumaa Aweso kwa majibu yake mazuri. Pengine hakumalizia tu kwamba Wizara ya Maji na Umwagiliaji inakamilisha mchakato wa mwisho kabisa wa kupata dola milioni 350 ambazo ndani yake kuna programu nzuri sana ya kupeleka huduma za maji katika shule za sekondari na za msingi zote nchini ambazo hazina huduma ya maji, pamoja na hizo alizotaja Mheshimiwa Kitandula, Shule za Maramba ambayo ni shule ya zamani sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nimhakikishie kwamba tumeshatoa agizo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri wote akiwemo Mkurugenzi wake, kuhakikisha kwamba shule ambazo wamezipangia kwamba zitaombewa kibali ziwe kidato cha tano na sita wanaweka kipaumbele cha haraka ili kusudi miundombinu yake iweze kukamilika, maombi yake yaweze kufikishwa Wizara ya Elimu ili zipate kibali ili angalau mwakani ziweze kuanza kuchukua vijana wa kidato cha tano na sita.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:- Shule za Sekondari za Farkwa na Msakwalo zilizoko Wilayani Chemba zimepandishwa hadhi kuwa za A – level na idadi ya wanafunzi imeongezeka katika shule hizo:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuzipatia maji ya uhakika shule hizo ili kuwaondolea wanafunzi adha ya kutafuta maji badala ya masomo?

Supplementary Question 3

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Tatizo la maji katika shule za sekondari pamoja na shule za misingi lipo Tanzania nzima na nimemsikia Mheshimiwa Naibu Waziri hapa wakati anajibu anasema tatizo hilo litatatuliwa katika shule zote za sekondari.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nataka nifahamu jambo hilo litatekelezwa lini kwa kuwa tumeshapitisha bajeti na hakuna fedha yoyote iliyopitishwa kwa ajili ya kupeleka maji katika shule za sekondari. Upi ni mpango ambao utasaidia kupeleka maji shule za sekondari na shule za msingi Tanzania nzima ikiwemo Momba? Ahsante.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa David Silinde, Mbunge kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kitandula, nimetoa ufafanuzi kwamba tunakamilisha mchakato wa mwisho wa kupata hizi fedha ambao ni mkopo nafuu kutoka Benki ya Dunia, dola milioni 350 si hela ndogo, ni hela ndefu. Kwa hiyo, mchakato huu unaweza ukakamilika vizuri kabisa 2018/2019 na fedha hizo zikaanza kutumika 2019/2020 kwa ajili ya kuhakikisha kwamba shule zetu zote zinaondolewa matatizo kabisa ya kukosa huduma ya maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini katika bajeti ambayo tumeipitisha Bungeni hapa ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji na fedha nyingine chache tulizipitisha katika kasma yetu ya TAMISEMI ambazo zote sasa tutazipeleka Wizara ya Maji ili ziweze kusimamiwa vizuri zaidi, zipo bajeti ambazo si kubwa sana kwa ajili ya kuhakikisha tumepeleka huduma za maji katika baadhi ya shule. Ahsante sana.

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Napenda kuongezea kidogo majibu mazuri ambayo yametolewa na Mheshimiwa Naibu Waziri kulifahamisha Bunge lako Tukufu kwamba kupitia Mradi wa SWASH kuna kiasi cha shilingi bilioni 16 ambazo zimetengwa kwa ajili ya kuimarisha miundombinu ya maji shuleni. Kwa hiyo, mimi hiyo naona si hela kidogo, tayari Serikali imeonesha commitment, shilingi bilioni 16 zipo kwa ajili ya kuimarisha miundombinu ya maji shuleni kwa mwaka wa Fedha 2018/2019. Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:- Shule za Sekondari za Farkwa na Msakwalo zilizoko Wilayani Chemba zimepandishwa hadhi kuwa za A – level na idadi ya wanafunzi imeongezeka katika shule hizo:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuzipatia maji ya uhakika shule hizo ili kuwaondolea wanafunzi adha ya kutafuta maji badala ya masomo?

Supplementary Question 4

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Singida Mjini tumeanza programu ya kupandisha hadhi shule zetu za sekondari kuwa kidato cha tano na sita ikiwemo Shule ya Sekondari ya Mungumaji. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kutusaidia kukamilisha programu hii?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mussa Ramadhan Sima, Mbunge wa Singida Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, nikirejea majibu yangu ya awali ambayo nimeyatoa, kwanza yeye kama mwalimu namsifu kwa juhudi zake za kuendeleza sekta ya elimu katika jimbo lake lakini vilevile kutoa mawazo mazuri kwa ajili ya nchi nzima. Napenda kusisitiza kwamba maagizo ambayo tumeyatoa kwa Wakurugenzi wa Halmashauri ambao wanasimamiwa na Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa ni kwamba kipaumbele lazima waendelee kukiweka katika shule zote ambazo wameziteua kwa ajili ya kuzipandisha hadhi kuwa za kidato cha tano na sita kwa maana hizo zitakuwa ni shule za nchi. Waweke kipaumbele kuhakikisha kwamba miundombinu inayohitajika yote kwa mujibu wa vigezo vilivyotolewa na Wizara ya Elimu inakamilika mapema iwezekanavyo ili kusudi shule hizo ziweze kutusaidia kupokea watoto wengi zaidi au vijana wengi zaidi wa kidato cha tano na sita.

Name

Justin Joseph Monko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:- Shule za Sekondari za Farkwa na Msakwalo zilizoko Wilayani Chemba zimepandishwa hadhi kuwa za A – level na idadi ya wanafunzi imeongezeka katika shule hizo:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuzipatia maji ya uhakika shule hizo ili kuwaondolea wanafunzi adha ya kutafuta maji badala ya masomo?

Supplementary Question 5

MHE. JUSTIN J. MONKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniona. Katika Jimbo langu la Singida Kaskazini tunazo sekondari tatu ambazo zilipandishwa hadhi ikiwepo katika Tarafa ya Mgori Mwanamema, Ilongero pamoja na Mtinku. Shule hizi bado zina changamoto zikiwepo za vitanda, magodoro na kadhalika na zingine zimeshindwa hata kupangiwa wanafunzi katika mwaka huu kwa sababu hazijakidhi vigezo. Je, Serikali itatusaidiaje ili kukamilisha vigezo hivyo na shule hizo zianze kutoa huduma kama ilivyokusudiwa?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA):
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Justin Monko, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, amezitaja shule tatu katika jimbo lake ambazo zimepandishwa hadhi, lakini kati ya shule tatu Shule ya Mwanamema Shein kama ilivyo jina lake ni shule ambayo imeboreshwa kwa kiasi kikubwa na sasa hivi wamepangwa vijana kupelekwa pale. Wengine walikuwa wanakuja ofisini kwangu kusema bwana hii Shule ya Mwanamema Shein sisi hatuitambui tunaomba tuhamishe watoto, nimewaambia hatuwezi kuhamisha watoto pale. Watoto waende wakasome pale Shule ya Mwanamema Shein na watapata elimu nzuri, tumepeleka walimu wazuri pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nimhakikishie Mheshimiwa Monko pamoja na Waheshimiwa Wabunge wote kwamba zile shule ambazo zina usajili wa Wizara ya Elimu lakini zinatakiwa kuongezewa miundombinu kidogo tu ili kusudi ziweze kuchukua vijana wengi zaidi kuliko capacity yao ya sasa hivi, wiki ijayo Wizara ya Fedha itapeleka fedha kwenye hizo shule, kama walikuwa wanakosa bwalo watajengewa bwalo, kama walikuwa wanakosa darasa moja watajengewa darasa moja ili kusudi mpaka mwezi wa nane vijana wa second selection waweze kuripoti shuleni.