Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 55 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 467 2018-05-21

Name

Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:-
Shule za Sekondari za Farkwa na Msakwalo zilizoko Wilayani Chemba zimepandishwa hadhi kuwa za A – level na idadi ya wanafunzi imeongezeka katika shule hizo:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuzipatia maji ya uhakika shule hizo ili kuwaondolea wanafunzi adha ya kutafuta maji badala ya masomo?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Juma Selemani Nkamia, Mbunge wa Chemba kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Shule ya Sekondari Msakwalo ilikuwa ikitumia maji ya bomba kutoka katika kisima cha kijiji na Shule ya Sekondari Farkwa ilikuwa inatumia miundombinu ya kuvuna maji ya mvua na pia ilikuwa ikitumia maji ya bomba kutoka katika kisima cha kijiji. Visima hivi pamoja na uchakavu wa miundombinu havikuwa na uwezo wa kuzalisha maji ya kutosha kwa matumizi ya vijiji pamoja na shule. Hivyo, shule hizo kushindwa kupata maji ya kutosheleza kwa mwaka mzima.
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kutatua tatizo la maji katika Shule za Sekondari Msalikwa na Farkwa, Serikali katika mwaka wa fedha 2017/2018, ilitoa jumla ya shilingi milioni 104 kwa Shule ya Sekondari Msalikwa na shilingi milioni 87 kwa Shule ya Sekondari Farkwa kwa ajili ya kuchimba visima na kufanya ukarabati wa miundombinu ya mfumo wa bomba kwenye shule hizo. Kazi ya uchimbaji wa visima na ukarabati wa miundombinu ya mabomba katika shule hizo imekamilika na wanafunzi kwa sasa wanapata maji ya kutosha.