Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. MARY P. CHATANDA - (K.n.y MHE. STEPHEN H. NGONYANI) aliuliza:- Serikali ilitenga shilingi bilioni 13 kwa ajili ya ujenzi wa Bwawa la Mkomazi lakini baadaye Serikali ilihamishia fedha hizo mkoa mwingine:- Je, Serikali ina mpango gani wa kurudisha fedha hizo ili bwawa lililokusudiwa lijengwe?

Supplementary Question 1

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru na nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa Serikali ilikuwa bado haijaupa kipaumbele mradi huu na sasa wanasema walishaliweka katika vipaumbele vya kutekeleza mradi huu kama mradi kabambe wa umwagiliaji. Je, sasa Waziri atakuwa tayari kufuatana na Mbunge wa Jimbo ndugu yangu Stephen Ngonyani baada ya Bunge hili ili kwenda kuwaeleza wananchi wa Mkomazi kutokana na mradi huu kuwa unasuasua kwa muda mrefu?
La pili, kwa kuwa atakapokuwa anapita kwenda Mkomazi, kwa kuwa kauli mbiu ya Rais wetu mpendwa ni Hapa Kazi tu, je, atakuwa tayari kupita Korogwe Mjini kwenye mradi wa kwa Mgumi wa umwagiliaji ili aweze kwenda kuuona na hatimaye kuweza kuufanyia kazi kutokana na matatizo walionayo? (Makofi). Mheshimimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, natambua kazi nzuri sana inayofanywa na Mheshimiwa Mbunge Hillary Ngonyani, Maji Marefu, kaka yangu, nataka nimhakikishie kwamba striker haogopi back. Kama Mbunge wa Jimbo la Pangani na Naibu Waziri wa Maji nipo tayari kwenda kuzungumza na wananchi wa Korogwe katika kuwahakikishia kwamba kilimo cha umwagiliaji kitafanyika katika eneo lake.
Mheshimiwa Spika, lingine nimhakikishie Mheshimiwa mama yangu Mary Chatanda tumekwisha kubaliana baada ya Bunge hili nitapita Kateshi, nitapitia Mkoa wa Tanga kufanya ziara yangu kuhakikisha wananchi wa Mkoa wangu wa Tanga wanapata maji safi, salama na yenye kuwatosheleza.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. MARY P. CHATANDA - (K.n.y MHE. STEPHEN H. NGONYANI) aliuliza:- Serikali ilitenga shilingi bilioni 13 kwa ajili ya ujenzi wa Bwawa la Mkomazi lakini baadaye Serikali ilihamishia fedha hizo mkoa mwingine:- Je, Serikali ina mpango gani wa kurudisha fedha hizo ili bwawa lililokusudiwa lijengwe?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza. Kwa kuwa katika Wilaya ya Mpwapwa na Kongwa kuna skimu za umwagiliaji ambazo zilijengwa sasa ni miaka 10 hazijafanyiwa ukarabati, katika Kijiji cha Chamkoroma, Mseta, Tumbugwe, Mlembule, Boli na Injovu. Hakuna hata mtaalam mmoja ambaye amepitia kuziona skimu zile. Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kwenda kukagua skimu za umwagiliaji katika maeneo haya?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, kwa kutambua sasa hivi tunaelekea katika uchumi wa viwanda na uchumi wa viwanda unategemeana kabisa na kilimo cha umwagiliaji. Nipo tayari Mheshimiwa Mbunge kuongozana na yeye katika kuhakikisha tunakwenda kuziangalia skimu zile zake za umwagiliaji.

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. MARY P. CHATANDA - (K.n.y MHE. STEPHEN H. NGONYANI) aliuliza:- Serikali ilitenga shilingi bilioni 13 kwa ajili ya ujenzi wa Bwawa la Mkomazi lakini baadaye Serikali ilihamishia fedha hizo mkoa mwingine:- Je, Serikali ina mpango gani wa kurudisha fedha hizo ili bwawa lililokusudiwa lijengwe?

Supplementary Question 3

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kupata nafasi hii. Kwa kuwa Kata ya Mkomazi ni jirani sana na Kata Ndungu na kwa kuwa pale kwenye Kata Ndungu kuna skimu kubwa sana ya umwagiliaji ambayo inasaidia kilimo kikubwa cha mpunga. Skimu ile sasa imeonekana kwamba imechoka sana na maisha ya wananchi wa Kata ya Ndungu, Kihurio mpaka Kalemawe yapo hatarini; je, Mheshimiwa Waziri atakapotoka Korogwe pale Mkomazi kwa sababu Ndungu ni jirani anatuambia nini, atakuja kuona skimu ile?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, naomba nirudie tena ukisoma Tenzi za Rohoni inasema unapotembea na kuzuru wengine naomba usinipite Mwokozi, sitompita Mheshimiwa mama Anne Kilango katika kuhakikisha wananchi wake wanapata maji. (Makofi/Kicheko)