Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Zahanati ya Migungumalo, Kata ya Usagari Uyui ilijengwa kwa maandalizi ya kuwa Kituo cha Afya na kufunguliwa na Rais wa Awamu ya Tatu, Mheshimiwa Benjamin William Mkapa tarehe 25/11/1997 na kuahidi kuwa zahanati hiyo itakuwa Kituo cha Afya cha Kanda ya Magharibi. (a) Je, Serikali ina mipango gani ya kuikuza zahanati hiyo ili iwe Kituo cha Afya kutokana na mahitaji na huduma zinazotolewa kuwa juu ya uwezo wa zahanati? (b) Kwa kuenzi kazi na juhudi za Rais Mstaafu Mheshimiwa Benjamin William Mkapa, kufika mpaka Usagari kufungua zahanati; je, Waziri yuko tayari kumwomba Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano kuja kuzindua Kituo cha Afya baada ya kuipandisha hadhi Zahanati hiyo ya Migungumano?

Supplementary Question 1

MHE. ALMAS. A MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naipongeza sana Serikali kwa fedha ambazo imetupatia kwa ajili ya Kituo cha Upuge na fedha ambazo zinapelekwa kwenye zahanati hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo naomba niseme ukweli kwamba methali ya kwamba mzigo mzito mpe Mnyamwezi, hatuitaki tena kwa sababu inatukandamiza. Tunasema mzigo mzito punguza, beba mwenyewe. Kwa sababu tumegundua kwamba kumbe mzigo mzito ni kutokuwa na vituo vya afya, kutokuwa na barabara huko kwetu, hatutaki tena.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunataka Bunge hili lielewe kwamba Wilaya yote ya Uyui ina kituo kimoja tu cha afya, sidhani kama kuna Wilaya nyingine hapa Tanzania iko namna hiyo, lakini vilevile hakuna tena hospitali ya Wilaya katika Wilaya nzima. Kwa hiyo, vituo vya afya vilivyopo, zahanati hizi ndiyo tunazoomba zipanuliwe ziweze kuwa vituo vya afya. Kwa hiyo, wananchi wa Kata ya Usagari, wamechanga shilingi milioni 50 wakiwa na lengo la kupanua kituo kile kiwe kituo cha afya na maeneo yapo. Tunaona ni bora kuongezea kuliko kujenga upya…
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali, je, Serikali iko tayari kubadili msimamo wake ili hela za wananchi, shilingi milioni 50 na Mfuko wa Jimbo wa shilingi milioni 10 watuongezee tupanue kituo kile kiwe kituo cha afya? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, samani swali langu la pili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; kwa kujua hali ilivyo kule Jimboni kwangu kwamba hakuna kituo cha afya, hakuna zahanati bora zaidi ya hiyo ya Migungumalo; je, Serikali iko tayari kutusaidia kujenga kupandisha Zahanati za Ilolanguru na Ufuluma ili vitumike kwa muda kama vituo vya afya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la mtani wangu Mnyamwezi wa Tabora kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepata maombi yake Mheshimiwa Maige. Hata hivyo naomba nikiri wazi kwamba Mbunge huyu amekuwa mpiganaji sana wa eneo lake. Hata siyo muda kwa kazi kubwa anayofanya, hata jina la Halmashauri yake muda si mrefu sana litabadilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nafahamu kwamba kutokana na changamoto, ndiyo maana tuliwapa fedha kuimarisha Kituo cha Afya cha Upuge ambacho sasa hivi kinaenda vizuri, lakini hata katika bajeti ya mwaka 2018/2019 kutokana na shida kubwa waliyokuwa nayo tumewapa takriban shilingi bilioni 1.5 watajenga Hospitali ya Wilaya. Vilevile kabla ya tarehe 15 mwezi wa saba katika Jimbo la Igalula tutapeleka fedha nyingine kwa ajili kuimarisha kituo cha afya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimhakikishie kwamba wananchi wa jimboni kwako tutafanya kila liwezekanalo ili kama kuna vituo ambavyo vinatakiwa tuvipe hadhi, tutaangalia nini tufanye, lengo letu kubwa kama Serikali ni kuhakikisha kwamba Wanyamwezi wa Tabora wanapata huduma ya afya vizuri kama wengine. (Makofi)

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Zahanati ya Migungumalo, Kata ya Usagari Uyui ilijengwa kwa maandalizi ya kuwa Kituo cha Afya na kufunguliwa na Rais wa Awamu ya Tatu, Mheshimiwa Benjamin William Mkapa tarehe 25/11/1997 na kuahidi kuwa zahanati hiyo itakuwa Kituo cha Afya cha Kanda ya Magharibi. (a) Je, Serikali ina mipango gani ya kuikuza zahanati hiyo ili iwe Kituo cha Afya kutokana na mahitaji na huduma zinazotolewa kuwa juu ya uwezo wa zahanati? (b) Kwa kuenzi kazi na juhudi za Rais Mstaafu Mheshimiwa Benjamin William Mkapa, kufika mpaka Usagari kufungua zahanati; je, Waziri yuko tayari kumwomba Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano kuja kuzindua Kituo cha Afya baada ya kuipandisha hadhi Zahanati hiyo ya Migungumano?

Supplementary Question 2

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwanza kabisa naishukuru Serikali kwa kutupatia fedha milioni mia tano kujenga Kituo cha Afya cha Ihalula, lakini naomba kuiuliza Serikali; je, lini sasa watatupatia fedha kwa ajili kukarabati Hospitali ya Halmashauri ya Mji Njombe Kibena?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Mwalongo kwa sababu juzi nilienda kukagua kituo kile wamejenga vizuri sana. Nilipokuwa Mkoani Njombe nilitembelea vituo mbalimbali, miongoni mwa kituo ambacho wametumia taaluma vizuri ya Force Account, Mheshimiwa Mwalongo mmefanya vizuri. Hata hivyo tunafahamu katika ujenzi, hasa changamoto ya miundombinu, kama Serikali, tunachukua hili tunaweka katika mipango yetu. Lengo kubwa ni kwamba isiwe kwa hospitali yako peke yake, lakini hospitali mbalimbali za Wilaya ambazo zinachangamoto lazima tulirekebishe ili wananchi wapate huduma vizuri. (Makofi)

Name

Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Zahanati ya Migungumalo, Kata ya Usagari Uyui ilijengwa kwa maandalizi ya kuwa Kituo cha Afya na kufunguliwa na Rais wa Awamu ya Tatu, Mheshimiwa Benjamin William Mkapa tarehe 25/11/1997 na kuahidi kuwa zahanati hiyo itakuwa Kituo cha Afya cha Kanda ya Magharibi. (a) Je, Serikali ina mipango gani ya kuikuza zahanati hiyo ili iwe Kituo cha Afya kutokana na mahitaji na huduma zinazotolewa kuwa juu ya uwezo wa zahanati? (b) Kwa kuenzi kazi na juhudi za Rais Mstaafu Mheshimiwa Benjamin William Mkapa, kufika mpaka Usagari kufungua zahanati; je, Waziri yuko tayari kumwomba Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano kuja kuzindua Kituo cha Afya baada ya kuipandisha hadhi Zahanati hiyo ya Migungumano?

Supplementary Question 3

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naipongeza sana Serikali katika kuhakikisha inaboresha miundombinu ya sekta ya afya. Hata hivyo, je, Serikali iko tayari kwenda sambamba na uongezaji wa watumishi katika maeneo hayo? Kwa sababu sasa hivi changamoto kubwa sana ni watumishi katika zahanati zetu na vituo vya afya pamoja na hospitali.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tumemsikia Mheshimiwa Hawa Ghasia, ninafahamu kwamba siyo muda mrefu tutaimarisha kituo chake cha Mahulunga pale katika Jimbo lake ambalo najua kwamba changamoto ya watumishi itakuwa kubwa. kwa bahati nzuri Naibu Waziri alishasema awali kwamba tunaajiri watumishi 6,180.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutawapa kipaumbele katika miundombinu hii wananchi waweze kupata huduma ya afya katika Jimbo la Mtwara DC.

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Zahanati ya Migungumalo, Kata ya Usagari Uyui ilijengwa kwa maandalizi ya kuwa Kituo cha Afya na kufunguliwa na Rais wa Awamu ya Tatu, Mheshimiwa Benjamin William Mkapa tarehe 25/11/1997 na kuahidi kuwa zahanati hiyo itakuwa Kituo cha Afya cha Kanda ya Magharibi. (a) Je, Serikali ina mipango gani ya kuikuza zahanati hiyo ili iwe Kituo cha Afya kutokana na mahitaji na huduma zinazotolewa kuwa juu ya uwezo wa zahanati? (b) Kwa kuenzi kazi na juhudi za Rais Mstaafu Mheshimiwa Benjamin William Mkapa, kufika mpaka Usagari kufungua zahanati; je, Waziri yuko tayari kumwomba Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano kuja kuzindua Kituo cha Afya baada ya kuipandisha hadhi Zahanati hiyo ya Migungumano?

Supplementary Question 4

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kituo cha Afya Endabash katika Tarafa ya Endabash inahudumia kata nne, lakini kituo hicho kina upungufu mkubwa ikiwemo jengo la mama na mtoto, maabara na mortuary. Ni lini Serikali itatoa fedha ili miundombinu hiyo iliyobaki ikamilike ili kituo hicho kitoe huduma stahiki?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninafahamu Endabash ni sehemu yenye changamoto kubwa. Tukijua wazi kwamba Wilaya yetu ya Karatu ni center kubwa ya watalii, ndiyo maana katika mipango mikakati yetu kwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI tunataka kuangalia tuone ni jinsi gani tutafanya tu upgrade kituo kimoja. Mimi naamini kwamba kwa sababu ya ajenda kubwa ya utalii, jukumu langu kubwa ni kuhakikisha unajipanga vizuri na watu wako, ikifika kabla ya mwezi Disemba kituo hicho kiwe kimekamilika kwa ajili ya kuwatumikiwa wananchi wa eneo hilo.

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Zahanati ya Migungumalo, Kata ya Usagari Uyui ilijengwa kwa maandalizi ya kuwa Kituo cha Afya na kufunguliwa na Rais wa Awamu ya Tatu, Mheshimiwa Benjamin William Mkapa tarehe 25/11/1997 na kuahidi kuwa zahanati hiyo itakuwa Kituo cha Afya cha Kanda ya Magharibi. (a) Je, Serikali ina mipango gani ya kuikuza zahanati hiyo ili iwe Kituo cha Afya kutokana na mahitaji na huduma zinazotolewa kuwa juu ya uwezo wa zahanati? (b) Kwa kuenzi kazi na juhudi za Rais Mstaafu Mheshimiwa Benjamin William Mkapa, kufika mpaka Usagari kufungua zahanati; je, Waziri yuko tayari kumwomba Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano kuja kuzindua Kituo cha Afya baada ya kuipandisha hadhi Zahanati hiyo ya Migungumano?

Supplementary Question 5

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi nami niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya ya Wanging’ombe kuna Kituo cha Afya cha Makoga. Kituo hiki ni cha kimkakati, kinahudumia wananchi wa Tarafa ya Imalinyi na Mdandu. Tuseme ni theluthi mbili ya wananchi wa Wilaya ya Wanging’ombe wanapata huduma katika Kituo cha Afya hicho cha Makoga, lakini hali yake ya miundombinu ni mibaya sana. Je, ni lini Serikali itatoa pesa ili kuweza kukarabati Kituo kile cha Afya cha Makoga?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumpongeza Mheshimiwa Neema Mgaya na Wabunge wa Njombe wote kwa ujumla wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi tulikuwepo kule tukifanya harambee na tulipata shilingi milioni mia moja na thelathini na saba. Namshukuru Mheshimiwa Neema, Mheshimiwa Lwenge na Waheshimiwa Wabunge wote. Hii tulifanyia pale Makoga na kweli changamoto yake ni kubwa. Hata hivyo tulitembelea Kituo kingine cha Afya cha Palangawano ambacho kinajengwa. Kwa hiyo, kama Serikali tumeweka kipaumbele katika maeneo haya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini kabla ya mwezi wa 12 kati ya vituo hivyo viwili tutaweza kukiboresha kituo kimojawapo. Hata hivyo priority ya Makoga na Palangawale lazima tuikamilishe kwa ajili ya wananchi wa Wanging’ombe waweze kupata huduma vizuri. (Makofi)