Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE (K.n.y. MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI) aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Nne iliahidi kuanzisha Mkoa mpya wa Selous. a) Je, ahadi hiyo itatekelezwa lini? b) Je, Serikali haioni kuwa mpaka wa Kusini wenye urefu wa zaidi ya kilometa 600 na wenye mikoa miwili tu sio salama kiulinzi?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri wa TAMISEMI, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kwa kuwa eneo la Sasawala ndiyo eneo ambalo linategemewa kuanzisha Wilaya Mpya na Makao Makuu yake kuwa Lusewa; je, ni kwa nini Serikali isianzishe Jimbo jipya la Uchaguzi katika eneo hilo la Sasawala?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ilifuata utaratibu wote wa kuanzisha Wilaya mbili, kwa maana Wilaya ya Tunduru Kusini na Tunduru iliyopo sasa na kwa kuwa Halmashauri hiyo iliendesha vikao vya kuanzisha miji midogo miwili, katika Vijiji vya Nalasi na Mchoteka; je, Serikali haioni haja kwa sasa kuanzisha miji midogo katika eneo la Nalasi na Mchoteka? Ahsante. (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, majibu yangu katika maswali yake mawili ya nyongeza, hayawezi kutofautiana sana na jibu langu la swali la msingi. Kuhusu kuanzisha Jimbo jipya, utaratibu wake uko tofauti kidogo na utaratibu wa kuanzisha maeneo mapya ya utawala.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kuanzisha Jimbo jipya linahusisha sana Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Tume ya Taifa ya Uchaguzi kabla ya michakato yoyote ya mikutano haijaanza, inatakiwa itangaze nia ya kuanzisha Jimbo jipya katika eneo fulani, baada ya hapo ndiyo vikao viridhie na baadae Mheshimiwa Rais aridhie. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili kwamba michakato ya kuanzisha Wilaya mbili kutoka katika Wilaya moja ya Tunduru, kwa maana Tunduru na Tunduru Kusini na miji aliyoitaja kwamba iwe miji midogo, utaratibu wake ni sawasawa na jibu langu kwenye swali la msingi kwamba hii miji midogo ni maeneo mapya ya utawala, kwa maana kwamba ukishakuwa na mji mdogo utakuwa na Halmashauri ya Mji, Mkurugenzi na utakuwa na vikao vinavyohusika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, maeneo hayo yote ya utawala yamesitishiwa kuanzishwa hadi hapo tutakapoimarisha zaidi maeneo tuliyonayo sasa hivi. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE (K.n.y. MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI) aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Nne iliahidi kuanzisha Mkoa mpya wa Selous. a) Je, ahadi hiyo itatekelezwa lini? b) Je, Serikali haioni kuwa mpaka wa Kusini wenye urefu wa zaidi ya kilometa 600 na wenye mikoa miwili tu sio salama kiulinzi?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Jimbo la Mpanda Vijijini ni kubwa lenye kilometa za mraba 16,900. Jimbo hili limekuwa vigumu sana kurahisisha shughuli za kiutendaji kwa sababu ya ukubwa.
Je, ni lini Serikali itafikiria kuligawa Jimbo hili ili kupeleka huduma kwa wananchi kuwa karibu?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba hapa nchini yako maeneo ambako Majimbo yake ni makubwa sana pamoja na hili Jimbo ambalo Mheshimiwa Kakoso amelitaja.
Sasa utaratibu wake hautofautiani sana na maelezo ambayo nimeyatoa hapo awali kwamba namuomba Mheshimiwa Mbunge tushirikiane, lakini hasa yeye kuwasiliana na Tume ya Taifa ya Uchaguzi ili waingize kwenye orodha ya maeneo ambayo watayataja kwamba yanahitajika kugawanywa kuwa Majimbo mawili. Kwa hiyo, naomba sana tushirikiane baada ya hapa pengine tuonane ili tupeane maelezo zaidi.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE (K.n.y. MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI) aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Nne iliahidi kuanzisha Mkoa mpya wa Selous. a) Je, ahadi hiyo itatekelezwa lini? b) Je, Serikali haioni kuwa mpaka wa Kusini wenye urefu wa zaidi ya kilometa 600 na wenye mikoa miwili tu sio salama kiulinzi?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Kusini unaozungumzwa ilikuwa uchangiwe pamoja na Wilaya ya Liwale, Nachingwea na Masasi kutokana na mikoa hii kuwa mbali na Makao Makuu ya Mikoa. Serikali kusitisha uanzishwaji wa Mkoa huu wa Selous, huoni kwamba ni kuwanyima haki ya kimsingi wananchi wanaokaa maeneo haya ambao wako mbali sana na Makao Makuu ya Mkoa? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza katika swali lake ameongeza maeneo ambayo hayajawahi kujadiliwa; yapo maeneo aliyoyaongeza hapa kama Liwale na wengine wanazungumza Nanyumbu kwamba iwe katika sehemu ya Mkoa mpya wa Selous.
Katika majadiliano yaliyofanyika, maeneo hayo hayakutajwa kwamba ni sehemu ya mapendekezo ya Mkoa mpya. Sasa kwa sababu ni mapya basi naomba sana Mheshimiwa Kuchauka ayapeleke kwenye Mkoa wake wa Mtwara ili waweze kuyajadili kuanzia huko. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE (K.n.y. MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI) aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Nne iliahidi kuanzisha Mkoa mpya wa Selous. a) Je, ahadi hiyo itatekelezwa lini? b) Je, Serikali haioni kuwa mpaka wa Kusini wenye urefu wa zaidi ya kilometa 600 na wenye mikoa miwili tu sio salama kiulinzi?

Supplementary Question 4

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijaanza kuuliza swali, naomba nimpongeze Mheshimiwa Rais kwa kugawa tablets kwa walimu wakuu wa shule za msingi ili kuboresha elimu na ufundishaji. Mheshimiwa Rais aliahidi na ameanza kutekeleza, angalau ni kawaida yake kuahidi na kutekeleza, tunampongeza sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa taratibu zote za kuugawa Mkoa wa Tabora zilishakamilika na Serikali iliahidi kutimiza kuugawa mkoa huo ambao una Wilaya saba na una wakazi wengi na kuwasababishia wakazi wa mkoa huo kukosa huduma za msingi kama inavyostahili.
Je, ni lini sasa Serikali itaugawa Mkoa Tabora kama ilivyogawa Mkoa wa Mbeya kuwa Songwe na kama ilivyogawa Shinyanga na Simiyu ili wananchi wa Tabora nao waweze kupata haki zao za msingi?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitoe maelezo kwamba sisi katika Mkoa wa Tabora tunajivunia sana utendaji kazi wa Mheshimiwa Munde Tambwe Abdallah kwa jinsi ambavyo anafuatilia masuala mbalimbali kwenye Mkoa wa Tabora. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimkumbushe kwamba Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli alipotembelea Mkoa wa Tabora mwaka 2017 na kufanya mkutano wa hadhara pale Nzega lilijitokeza swali hili la ombi la kuugawa Mkoa wa Tabora kwamba tuwe na Mkoa mpya wa Nzega.
Mheshimiwa Mwenyekiti, majibu yake katika mkutano ule ndiyo ambayo yamejenga mwongozo wa kitaifa kwa sasa kwamba kuna haja kwanza kuimairisha miundombinu na mahitaji mengine katika Mikoa, Wilaya na Halmashauri mpya ambazo zilishaanzishwa tangu zamani ili tukikamilisha uimarishaji huo ndiyo tuje kwenye mikoa mpya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Mkoa wa Nzega limeshajadiliwa RCC na vikao vyote vimekamilika, tutakapokuwa tumeimarisha maeneo haya mapya yaliyopo, Mkoa huo mpya wa Nzega, naomba sana watu wa Nzega wasiendelee kubishana tena, utatangazwa mara moja na utapewa kipaumbele.