Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 47 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 397 2018-06-08

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE (K.n.y. MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI) aliuliza:-
Serikali ya Awamu ya Nne iliahidi kuanzisha Mkoa mpya wa Selous.
a) Je, ahadi hiyo itatekelezwa lini?
b) Je, Serikali haioni kuwa mpaka wa Kusini wenye urefu wa zaidi ya kilometa 600 na wenye mikoa miwili tu sio salama kiulinzi?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Edwin Amandus Ngonyani, Mbunge wa Namtumbo, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, mnamo tarehe 15 Julai, 2013 Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa ziarani Wilayani Tunduru alikutana na wazee wa Tunduru walioomba mkoa mpya wa Selous. Katika majibu yake alielekeza taratibu zifuatwe kisheria, kwa maana hiyo, hakuahidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maelekezo hayo, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma imeratibu vikao kadhaa vya kisheria kikiwemo Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Ruvuma cha tarehe 28 Novemba, 2017 kilichosisitiza ombi la kuundwa kwa mkoa mpya wa Selous wenye Wilaya nne za Tunduru, Tunduru Kusini, Namtumbo na Sasawala, Tarafa 10, Kata 53 na Vijiji 212 kwenye eneo lenye kilometa za mraba 38,988 na idadi ya watu 499,913 kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imetafakari kwa kina maombi hayo na kuyaona kuwa ni ya msingi. Hata hivyo, kutokana na changamoto ya kuimarisha kwanza miundombinu kama majengo ya Ofisi na nyumba za Watumishi na mahitaji mengine kama vifaa ya Ofisi, Watumishi wa kutosha na vyombo vya usafiri kwenye maeneo mapya ya utawala yaliyoanzishwa tangu mwaka 2010 na 2012, Serikali imesitisha uanzishwaji wa maeneo mapya ya utawala hadi maeneo mapya yaliyopo yaimarishwe kikamilifu.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ulinzi na usalama katika mpaka wa Kusini, ipo mikakati ya pamoja baina ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Msumbiji kuhakikisha kuwa mpaka huo upo salama. Nawaomba wananchi waendelee na shughuli zao bila wasiwasi wowote.