Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Gereza la Kilimo la Mng’aro ni miongoni mwa magereza kongwe hapa nchini, lakini gereza hili limekuwa na miundombinu chakavu kutokana na umri wake:- Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kulifanyia ukarabati mkubwa gereza hili pamoja na kuongeza uwezo wa kuchukua wafungwa wengi zaidi?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Swali langu lilikuwa very specific kwa Gereza la Mng’aro, lakini naona Waziri ananijibu na magereza mengine nchini. Sasa gereza hili limejengwa kwa miti pamoja na udongo na linahatarisha hata usalama wa wafungwa ambao wako pale. Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kuhakikisha kwamba, badala ya kusubiri changamoto za nchi nzima, kuwa na mpango wa muda mfupi wa kukarabati gereza hili?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa, gereza hili ni la kilimo na liko katika Skimu ya Kilimo ya Mng’aro ambayo ni kilimo cha mpunga na lilikuwa na uwezo wa kulisha magereza yote ya Mkoa wa Tanga. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kulipa zana bora za kilimo ili liweze kuzalisha zaidi na kuweza kulisha magereza yote ya Mkoa wa Tanga?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge, mara nyingi amekuwa akifuatilia sana maendeleo ya vyombo hivi vya usalama vilivyopo chini ya Wizara yetu ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Leo hili swali lake lake linaonesha msingi wa dhamira yake hiyo ya dhati.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusiana na swali lake la kwanza ambalo ametaka kujua kuhusu mpango mahususi wa ukarabati wa Gereza la Mng’aro; naomba nijibu swali hili pamoja na swali la pili kwa sababu yanaingiliana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Shangazi na Waheshimiwa Wabunge wengine, kwamba tumekuwa tukifanya jitihada mbalimbali ambazo zinasaidia kuboresha magereza yetu ambayo yako katika hali mbaya, ukiachilia mbali jitihada za Serikali kupitia bajeti kuu ambayo hata mwaka huu wa fedha tumetenga fedha hizo. Mifano iko mingi tu ambayo mimi binafsi nimefanya ziara maeneo kadhaa na tumeweza kushirikiana katika kuhakikisha kwamba tunafanya ukarabati kwa kutumia rasilimali katika maeneo husika. Naomba nichukue fursa hii kwa kutumia mfano huohuo ambao nimeweza kuona kwamba, umefanya kazi katika maeneo mengine ili tuupeleke Mlalo.
Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri hivi karibuni nilipofanya ziara katika Mkoa wa Lindi, watu wa Magereza wa Mkoa wa Lindi waliniambia kwamba, wangekuwa wamepata mashine za kufyatulia matofali ingerahisisha huu mchakato ambao tunauzungumza hapa. Nichukue fursa hii kumpa pongezi sana Kaimu Mkurugenzi wa National Housing Corporation ambaye baada ya kutoka Lindi nilimwandikia barua kumwomba mashine hizo na ametupatia mashine 10 kwa kuanzia ambazo nitazipeleka Lindi, lakini nitatumia mamlaka niliyokuwanayo kuchukua mashine moja ile kuipeleka kwa Mheshimiwa Shangazi, Mlalo, tukafanye kazi ile ya kuweza kuanza kufanya kazi ya ukarabati wa gereza letu lile kwa kutumia rasilimali za pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hiyo itasaidia vile vile kuhamasisha ujenzi wa mabweni ya ziada, kwa sababu suala la kilimo, kama swali lake la pili ambalo amelizungumza, linategemea vile vile nguvukazi ya wafungwa; ambapo kwa kiwango cha wafungwa waliopo Mng’aro sasa hivi na aina ya ukubwa wa shamba lile la karibu ekari nadhani zaidi ya 300 wafungwa wale hawatatosheleza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tutafanya jitihada za kuongeza mabweni, ili tupate wafungwa zaidi na wakati huohuo nimuahidi pia Mheshimiwa Shangazi kwamba tuna mpango vile vile wa kupata matrekta sita mapya ambayo tutayagawa katika magereza ambayo ni ya kilimo makubwa. Vile vile kule kuna matrekta ambayo ni chakavu, kwa hiyo tutachukua trekta moja chakavu tutalitengeneza vizuri tuweze kulipeleka Mng’aro. Tukifanya hayo tutakuwa tumetatua matatizo yote mawili kwa pamoja, tutakuwa tumeimarisha miundombinu wakati huohuo suala la kilimo cha mpunga katika eneo lile litakuwa limepatiwa ufumbuzi.

Name

Martin Alexander Mtonda Msuha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Gereza la Kilimo la Mng’aro ni miongoni mwa magereza kongwe hapa nchini, lakini gereza hili limekuwa na miundombinu chakavu kutokana na umri wake:- Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kulifanyia ukarabati mkubwa gereza hili pamoja na kuongeza uwezo wa kuchukua wafungwa wengi zaidi?

Supplementary Question 2

MHE.MARTIN M. MSUHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Gereza la Kitai lililopo Wilayani Mbinga ni moja ya magereza kongwe nchini. Gereza hili linakabiliwa na ukachavu wa miundombinu yake ikiwemo uchakavu wa lango kuu la kuingilia gerezani, bwalo la kulia chakula la wafungwa, lakini pia uzio wa kuzunguka gereza hilo umechakaa na unahatarisha usalama wa Maafisa Magereza wanaolinda wafungwa hao. Je, ni lini Serikali itakwenda kukarabati miundombinu katika gereza hilo la Kitai?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Naibu Spika, jibu la swali hili halitatofautiana sana na jibu ambalo nimejibu katika swali la msingi la Mheshimiwa Shangazi. Kitakachokuwa tofauti ni kwa sababu lilikuwa ni swali la msingi. Inawezekana pengine bahati ile ambayo Mheshimiwa Shangazi ameipata isiende sambamba na gereza la Kitai kwa maana ya kupata ile mashine, lakini ni kutokana na uchache wa hizo mashine zenyewe na changamoto tulizokuwa nazo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo nichukue fursa hii kumwomba Mheshimiwa Mbunge kwamba tushirikiane kutumia dhana ile ile ambayo nimeizungumza katika jibu langu la msingi; kwamba tunaweza haya matatizo madogo madogo ya kukarabati magereza yetu tukayafanya kwa kutumia rasilimali za maeneo husika bila kutengemea bajeti ya Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, Bajeti ya Serikali imetengwa lakini changamoto ni nyingi. Hivyo, kwa mambo madogo madogo kama haya tunaweza tukakaa tukashirikiana na Mheshimiwa Mbunge tukakae, baadaye tuandae utaratibu ikiwezekana hata mimi niende kwenye ziara kwenye jimbo lake ili nikapeleke uzoefu ambao nimeupata katika maeneo mengine uliosaidia kufanya marekebisho na ukarabati wa magereza ya maeneo mbalimbali nchini.

Name

John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Gereza la Kilimo la Mng’aro ni miongoni mwa magereza kongwe hapa nchini, lakini gereza hili limekuwa na miundombinu chakavu kutokana na umri wake:- Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kulifanyia ukarabati mkubwa gereza hili pamoja na kuongeza uwezo wa kuchukua wafungwa wengi zaidi?

Supplementary Question 3

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Suala la uchakavu na wingi wa mahabusu na wafungwa kwenye magereza, yaani kwa maana kwamba magereza kuzidiwa. Kwa mfano Gereza la Tarime lilijengwa mwaka 1947 kwa ajili ya kuchukua wafungwa 140 tu. Hivi tunavyoozungumza kuna watu mpaka 700. Je, Serikali ya CCM haioni kwamba kubeba watu wengi ndani ya magereza ni kukiuka haki za binadamu na kuwaumiza watu ndani ya magereza haya?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Naibu Spika, wingi wa watu magerezani si ukiukwaji wa haki za binadamu kwa sababu wako magerezani kwa mujibu wa sheria. Kitu ambacho nadhani ningemshauri Mheshimiwa Mbunge ni kwamba aendelee kuwa balozi mzuri wa wananchi wa Tarime kuhakikisha kwamba wanafuata sheria na wasifanye uhalifu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itajitahidi kupunguza msongamano pale ambapo inawezekana na tunafanya hivyo. Nachukua fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, amekuwa akifanya kazi nzuri ya kuona kwamba atumie mamlaka yake ya Kikatiba aliyokuwa nayo kusamehe wafungwa wale ambao amekidhi vigezo.

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Gereza la Kilimo la Mng’aro ni miongoni mwa magereza kongwe hapa nchini, lakini gereza hili limekuwa na miundombinu chakavu kutokana na umri wake:- Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kulifanyia ukarabati mkubwa gereza hili pamoja na kuongeza uwezo wa kuchukua wafungwa wengi zaidi?

Supplementary Question 4

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa gereza la Uyui Mkoa wa Tabora ni kongwe linafanana na gereza la Mng’aro. Kawaida ya gereza lile lilitakiwa kuchukua wafungwa 1,360 lakini mpaka ninavyosema hivi sasa lina wafungwa 1,860. Je, Serikali ina mpango gani wa kupanua gereza au kuwapunguza wafungwa waende sehemu nyingine?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la msongamano wa wafungwa ni suala pana na niseme bora nizungumze kwanza kwa ujumla wake kabla sijaenda specifically kwenye gereza la Uyui kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge ameuliza, maana yake naona masuala yote yanaingiliana katika hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, imsingi suala hili nimekuwa nikilijbu mara kadhaa katika kipindi cha nyuma kwamba tunaweza tukatatua tatizo la msongamano wa wafungwa kama ambavyo Serikali tunavyofanya kwa kufanya mambo yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, moja, tunapanga bajeti ya kuongeza mabweni yetu na kazi hiyo inaendelea kadri ya hali ya uwezo wa kibajeti utaporuhusu. Katika kipindi cha miaka mitano tumefanya hivyo katika magereza, nadhani takribani mawili kama sikosei.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo tunatumia sheri zetu zile tatu ama nne, Sheria ile ya Parole, Sheria ile ya Community Services pamoja na kutumia vile vile mamlaka ya kikatiba ya Mheshimiwa Rais. Kwa hiyo haya ni mambo ambayo tunayafanya kimsingi kupunguza msongamano wa wafungwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, lingine kubwa zaidi ni kuhakikisha kwamba tunafanya kila linalowezekana kupitia vyombo vingine vya dola kusimamia sheria. Ndiyo maana jeshi letu la polisi sasa hivi linafanya kazi kubwa ya kutoa elimu kwa wananchi ili kuepukana kufanya makosa ambayo yanaweza kuepukika ili kuweza kupunguza msongamano katika magereza yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, specifically kuhusiana na kwenye gereza la Uyui, nimwombe Mheshimiwa Mbunge kwamba kama ambavyo nimezungumza kwenye majibu yangu mengine haya mawili utaratibu ndio huo huo tu, aidha bajeti ya Serikali au utaratibu wa kuweza kutumia rasilimali za eneo husika kuweza kufanya marekebisho madogo madogo.

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Gereza la Kilimo la Mng’aro ni miongoni mwa magereza kongwe hapa nchini, lakini gereza hili limekuwa na miundombinu chakavu kutokana na umri wake:- Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kulifanyia ukarabati mkubwa gereza hili pamoja na kuongeza uwezo wa kuchukua wafungwa wengi zaidi?

Supplementary Question 5

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Swali langu, je, ni lini Serikali itaamisha gereza la Songwe ili kupisha mradi wa mgodi wa niobium ambao una thamani ya zaidi ya dola bilioni 6.8 ambayo ni sawa na shilingi bilioni 15. Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lake linauliza ni lini, nadhani sitaweza kujibu kwa lini sasa hivi hapa kabla ya kuweza kulifanyia utafiti. Ningeomba anipatie muda nilifanyie utafiti jambo lake hili nijue hasa undani wa hili tatizo lake lilivyo ili niweze baadaye kukaa nizungumze naye pembeni kuweza kumfahamisha kama ni lini litahamishwa au kama kuna mipango mingine ambayo ipo ya kuweza kukabiliana na tatizo ambazo amelizungumza.