Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 46 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 394 2018-06-07

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:-
Gereza la Kilimo la Mng’aro ni miongoni mwa magereza kongwe hapa nchini, lakini gereza hili limekuwa na miundombinu chakavu kutokana na umri wake:-
Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kulifanyia ukarabati mkubwa gereza hili pamoja na kuongeza uwezo wa kuchukua wafungwa wengi zaidi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Rashid Shangazi, Mbunge wa Mlalo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuwa Gereza la Kilimo la Mng’aro miundombinu yake ni chakavu kutokana na gereza hilo kuwa la muda mrefu, tangu mwaka 1977 hali ambayo inasababisha gereza hilo pamoja na miundombinu yake kuwa chakavu.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kukabiliana na changamoto hiyo Serikali linatekeleza mpango wa muda mrefu kwa nchi nzima wa kuboresha majengo hayo kwa kuyafanyia ukarabati mkubwa, ikiwemo Gereza la Mng’aro ili kuimarisha, kuyaboresha na kuyafanyia upanuzi.