Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Serikali iliahidi vijiji vingi vya Jimbo la Mbulu Vijijini umeme wa REA III. Je, ni lini sasa umeme utafika katika vijiji vya Endahargadat, Endahagichani, Qamtananat, Mewadan, Endalat, Gidbiyo na Manghay?

Supplementary Question 1

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nitoe ombi, Hospitali ya Haydom umeme unakatika mara nyingi sana. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Waziri atafute namna mbadala ya kusaidia umeme wa Haydom.
Swali sasa kwanza, nimshukuru Mheshimiwa Waziri alifika katika Jimbo la Mbulu Vijijini na kuahidi kwamba umeme utafika Endagichan Masieda, Endagichan Endamila, Yaeda Chini na Eshkeshi; je, ahadi hiyo bado ipo na umeme utafika vijiji hivyo?
Swali la pili; kwa kuwa Hospitali ya Haydom inatumia shilingi milioni 12 kwa ajili ya jenereta za dizeli kwenye vyanzo vya maji, je, Serikali ina mpango gani wa haraka ili kuisaidia hospitali ile kujihudumia vizuri kwa umeme kufika pale katika vyanzo vya maji?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini.
Kwa kweli nampongeza kufuatia ziara aliyofanya Mheshimiwa Waziri katika Jimbo lake tarehe 9 Mei, 2018 na kama mwenyewe alivyosema Mheshimiwa Waziri alipofika katika Jimbo lake alitoa ahadi ya kuongezeka kwa vijiji 22 kwa kuwa Jimbo hili lina vijiji vingi. Kwa hiyo, namthibitishia Mheshimiwa Mbunge, vijiji alivyovitaja ni miongoni mwa vijiji ambayo Mheshimiwa Waziri aliahidi na tumeshaviwasilisha REA kwa ajili ya taratibu za awali za upembuzi yakinifu.
Swali lake la pili kuhusu Hospitali ya Haydom, Mheshimiwa Waziri kupitia ziara yake ya tarehe 9 Mei, 2018 alitoa maelekezo kwa TANESCO kukamilisha ukarabati wa miundombinu ili wananchi wa Mkoa wa Manyara wapate umeme wa uhakika kwa wakati wote. Kwa hiyo, naomba niwahimize TANESCO wakamilishe hiyo kazi mwisho wa mwezi huu. Ahsante.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Serikali iliahidi vijiji vingi vya Jimbo la Mbulu Vijijini umeme wa REA III. Je, ni lini sasa umeme utafika katika vijiji vya Endahargadat, Endahagichani, Qamtananat, Mewadan, Endalat, Gidbiyo na Manghay?

Supplementary Question 2

MHE. AISHAROSE N. MATEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo lililopo Mbulu Vijijini Iinafanana kabisa na tatizo lililopo Iramba Mgharibi. Vijiji 13 vya Jimbo la Iramba Magharibi hadi sasa havijapatiwa umeme. Baadhi ya vijiji hivyo ni Kisua, Tieme B, Kisonso, Makunda, Twinke, Tulya, Meli na Kisiriri.
Je, ni lini sasa Serikali itapeleka umeme katika vijiji hivyo ili kuyawezesha makundi ya wanawake na vijana kujiajiri?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Aisharose Matembe kuhusu masuala ya REA katika vijiji vyake 13. Kwanza naomba nimtaarifu Mheshimiwa Mkoa wake wa Singida umepata vijiji 150 kwa REA hii Awamu ya Tatu, mzunguko wa kwanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, vijiji hivi kama ambavyo nimekuwa nikirejea kwenye majibu ya msingi, mpango wa Serikali ni kupeleka vijiji vyote umeme. Kwa hiyo, vijiji 13 vipo katika mpango wa REA mzunguko wa kwanza na ninawaomba Waheshimiwa Wabunge wote wafanye ufuatiliaji wa karibu na kwa kweli nafarijika kuona Wabunge wa Viti Maalum wanachangamkia miradi hii ya REA. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Lucy Thomas Mayenga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Serikali iliahidi vijiji vingi vya Jimbo la Mbulu Vijijini umeme wa REA III. Je, ni lini sasa umeme utafika katika vijiji vya Endahargadat, Endahagichani, Qamtananat, Mewadan, Endalat, Gidbiyo na Manghay?

Supplementary Question 3

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Wizara hii imekuwa ikijitahidi sana kwenye suala zima la usambazaji wa umeme katika maeneo mbalimbali kupitia miradi ya REA pamoja na taratibu nyingine.
Je, Wizara hii iko tayari sasa kuweza kuwasaidia wananchi wetu wa Wilaya ya Shinyanga Mjini na hasa Jimbo langu la Shinyanga ambako natoka ambapo tunakabiliwa na tatizo kubwa sana la kukatika sana sana kwa umeme; kwa taarifa nilizonazo ni kwamba kituo cha kusambazia umeme cha Ibadakuli kimezidiwa nguvu.
Je, Serikali ipo tayari sasa kuweza kusaidia kituo hiki kukiongezea nguvu ili umeme wa uhakika uweze kupatikana? Ahsante sana.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii. Ni kweli kufuatia utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa msongo wa KV 400 kutoka Iringa mpaka Shinyanga, mradi ule una taratibu za upanuzi wa vituo vya kupokea na kupoozea umeme kimojawapo ikiwa ni Ibadakuli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kituo kile pamoja na kuzidiwa, mradi huu wa kukikarabati na kukiwezesha kutoka kwenye KV 220 na kufika KV 400 utakwenda kutatua tatizo la wananchi wake wa Shinyanga ambako amekuwa akifuatilia sana mahitaji wa umeme. Ahsante.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Serikali iliahidi vijiji vingi vya Jimbo la Mbulu Vijijini umeme wa REA III. Je, ni lini sasa umeme utafika katika vijiji vya Endahargadat, Endahagichani, Qamtananat, Mewadan, Endalat, Gidbiyo na Manghay?

Supplementary Question 4

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniruhusu nami niulize swali la nyongeza kuhusu REA. REA haikupita kabisa katika vijiji vya Kanyenye, Majengo, Ikongolo, Kiwembe, Zumbuka na Igulawima, tukategemea kwamba REA Namba Tatu itatusaidia hilo, lakini sasa mkandarasi haonekani. Lini mkandarasi ataonekana katika vijiji hivyo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Almas juu ya lini Mkandarasi atafika katika maeneo yake kutekeleza mradi katika vijiji alivyotaja?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme, kwa kweli Wakandarasi kwa sasa hivi wako site na kwa kuwa kupitia Bunge lako na kupitia Wizara ya Fedha na Benki Kuu kwamba zile pesa shilingi bilioni 268 Letter of Credit zimefunguliwa pamoja na dola milioni 52. Kwa hiyo, nataka niseme wakandarasi wote hawana kisingizio tena waende site, wafanye kazi ili miradi hii ikamilike kwa wakati na hakutakuwa na msalie Mtume. Ahsante. (Makofi)

Name

Martha Jachi Umbulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Serikali iliahidi vijiji vingi vya Jimbo la Mbulu Vijijini umeme wa REA III. Je, ni lini sasa umeme utafika katika vijiji vya Endahargadat, Endahagichani, Qamtananat, Mewadan, Endalat, Gidbiyo na Manghay?

Supplementary Question 5

MHE. MARTHA J. UMBULLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi. Kwanza na mimi nampongeza sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kazi nzuri anayoifanya na kwa majibu yake mazuri.
Kwa kuwa umeme wa REA kwa sehemu kubwa inapopita katika Wilaya zetu za Mkoa wa Manyara zikiwepo Mbulu vijijini, zinapita katika barabara kuu na kuacha pembeni taasisi muhimu kama shule, zahanati na nyinginezo:-
Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba umeme huu sasa ujaribu kwenda vijijini zaidi ili iweze kunufaisha shule za sekondari, zahanati na taasisi nyingine muhimu na huko ambako kuna wananchi walio wengi zaidi?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Umbulla ambapo kwa kweli ameuliza swali la msingi, lakini tangu mwanzo baada ya kubaini changamoto ya REA I na REA II tumetoa maelekezo. REA Awamu ya Tatu taasisi zote za Umma alizozitaja ziwe zipaumbele. Kwa hiyo, naomba niendelee kusisitiza kwa wakandarasi, wasimamizi wa miradi yote, Mikoa na Wilaya walitekeleze hilo kwa wakati na kwa usimamizi wa hali ya juu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili ili Wabunge wasiendelee kuuliza swali kama hili, ni kwamba densifications awamu ya pili inaanza hivi karibuni katika mikoa 11. Densification hii maana yake ni ujazilizi, yale maeneo ambayo yamerukwa yatapatiwa umeme katika awamu inayoanza mwaka 2018/2019. Nawashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa sababu mmeshapitisha bajeti, msiwe na wasiwasi.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Serikali iliahidi vijiji vingi vya Jimbo la Mbulu Vijijini umeme wa REA III. Je, ni lini sasa umeme utafika katika vijiji vya Endahargadat, Endahagichani, Qamtananat, Mewadan, Endalat, Gidbiyo na Manghay?

Supplementary Question 6

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto katika utekelezaji wa mradi wa REA pia ni upatikanaji wa nguzo. Katika Jimbo la Bunda Mjini ni lini sasa nguzo zitafika katika maeneo ya Bunda Store, Nyamswa, ambapo katika Kitongoji cha Zanzibar pamoja na Nyabeu Sazila ili wananchi wahakikishiwe kupata umeme wa uhakika kwa sababu tatizo kubwa la maeneo hayo ni nguzo? Ahsante sana.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Bunda Mjini, Mheshimiwa Esther Bulaya, juu ya masuala ya upatikanaji wa nguzo katika maeneo ambayo ameainisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme Mkandarasi DEM yuko site anaendelea na kazi. Kama changamoto ilikuwa ufunguaji wa Letter of Credit kwa ajili ya kuagiza vifaa kwa wingi, tumeshawafungulia Wakandarasi wote; na kwa kuwa pia viwanda vya kuzalisha nguzo ambavyo viko ndani ya nchi, tumekutana navyo na nguzo zipo. Kwa mfano, hapo Kuwaya Iringa, Saw Mill Iringa na tumefanya uhakiki kwamba nguzo za kutosha zipo. Rai yangu kwa wakandarasi wote, waagize hivyo vifaa kwa wakati ili kusiwe na visingizio. Nakushukuru.

Name

John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Serikali iliahidi vijiji vingi vya Jimbo la Mbulu Vijijini umeme wa REA III. Je, ni lini sasa umeme utafika katika vijiji vya Endahargadat, Endahagichani, Qamtananat, Mewadan, Endalat, Gidbiyo na Manghay?

Supplementary Question 7

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Waziri hizi pesa za REA ni pesa ambazo ziko ring fenced, lakini mpaka sasa ninavyozungumza kwenye Jimbo langu mradi wa densification haujafanyika hata mmoja kwenye maeneo ya Nyamorege, Nyabitocho, Kyoruba, Pemba na Matongo ambayo ni maeneo makubwa yenye watu wengi. Kwa mfano, Nyamorege ina watu zaidi ya 20,000 wenye uwezo wa kutumia umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nauliza, ni lini mkandarasi atakwenda pale? Kwa sababu mnasema pesa zipo, lakini yeye anasema hajalipwa pesa; lini anakwenda kuwekea watu wa Tarime umeme hasa Kata ya Susuni ambayo haina umeme kabisa kata nzima na ina watu wengi? (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Heche ameeleza kwamba kuna mradi wa densification, haoni maendeleo yoyote. Nataka niseme hii miradi iko tofauti. Densification kwa kweli hela zake zipo na unafadhiliwa na Serikali ya Norway pamoja na Serikali ya Tanzania na ni shilingi bilioni 62. Sasa labda baada ya kipindi hiki cha maswali na majibu, namwomba Mheshimiwa Mbunge tukutane ili tuongee na mkandarasi nijue tatizo lake ni nini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa densification hauna matatizo kabisa na kwa kuwa Mkoa wa Mara uko katika mikoa ile nane ya awali na sasa hivi matarajio yetu ni mwezi Mei miradi yote ya densification iwe imekamilika ili tuanze na densification awamu ya pili. Kwa hiyo, namuomba Mheshimiwa Mbunge tuwasiliane baada ya hapa ili tuweze kuona tatizo ni nini ili niweze kulishughulikia.

Name

Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Serikali iliahidi vijiji vingi vya Jimbo la Mbulu Vijijini umeme wa REA III. Je, ni lini sasa umeme utafika katika vijiji vya Endahargadat, Endahagichani, Qamtananat, Mewadan, Endalat, Gidbiyo na Manghay?

Supplementary Question 8

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi.
Naomba niulize swali moja la nyongeza. Tarafa ya Wampembe yenye Kata nne za Kala, Wampembe, Kizumbi na Ninde iko kwenye mpango wa REA. Ninavyosema hivi, hakuna harakati zozote zinazoendelea katika kupeleka umeme katika maeneo haya. Je, ni lini Serikali itapelekea wananchi umeme katika maeneo haya?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mipata juu ya lini Serikali itapeleka umeme katika Tarafa ya Mwampembe; na ameainisha kwamba iko katika mpango wa REA. Napenda nimthibitishie kwamba Mkandarasi Nakuroi Investment yupo anafanya kazi katika Mkoa wa Rukwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimwelekeze Mkandarasi na tumetoa maelekezo kwamba wasifanye kazi kujielekeza kwenye eneo moja. Kwa kuwa hakuna changamoto nyingine ya kuagiza vifaa, nawaomba Wakandarasi wote wa miradi ya REA wawe na magenge ya kutosha katika Majimbo yote na Wilaya zote ili kazi zitekelezeke kwa wakati na kwa speed ambayo tunaitarajia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tatizo ni hilo, nitaongea na Wakandarasi wote nchi nzima. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.