Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 45 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 385 2018-06-06

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-
Serikali iliahidi vijiji vingi vya Jimbo la Mbulu Vijijini umeme wa REA III.
Je, ni lini sasa umeme utafika katika vijiji vya Endahargadat, Endahagichani, Qamtananat, Mewadan, Endalat, Gidbiyo na Manghay?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Gregory Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nia ya Serikali ni kufikisha umeme katika vijiji vyote Tanzania Bara visivyokuwa na miundombinu ya umeme ifikapo mwezi Juni, 2021. Jimbo la Mbulu vijijini lina vijiji vipatavyo 76, kati ya vijiji hivyo 12 vimepatiwa umeme. Vijiji 13 vya Qaloda, Getesh, Endesh, Labay, Maretadu, Hayderer, Endanachan (Haydom), Muslur, Dirim, Simha, Yaeda Ampa, Endoji na Gidhim vimejumuishwa katika mradi wa REA awamu ya tatu mzunguko wa kwanza. Mkandarasi Kampuni ya Angelique International Limited kutoka India ameshaanza utekelezaji wa mradi na anatarajia kukamilisha kazi hiyo mwezi Juni, 2019. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi za mradi zinahusisha ujenzi wa kilometa 45.87 za njia ya umeme wa msongo wa Kilovolt 33 na kilometa 35 za nja ya umeme wa msongo wa 0.4 kilovolt, ufungaji wa transfoma 16 na uunganishwaji wa wateja wa awali 347. Gharama za mradi ni shilingi bilioni 2.6. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji vilivyobaki vitapatiwa umeme kupitia mradi wa REA awamu ya tatu mzunguko wa pili utakaoanza kutekelezwa Julai, 2019 hadi mwezi Juni, 2021. Nakushukuru. (Makofi)