Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:- Mjasiliamali au mtu yeyote anapokata mti anatakiwa achukue 70% ya kile anachokilipia:- • Je, ni lini recovery rate ya 30% ya mbao ilifanyiwa utafiti? • Je, ni taasisi gani ilifanya utafiti huo?

Supplementary Question 1

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize maswali madogo mawili ya nyongeza pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, tofauti ya majibu haya kwamba kuna asilimia 60 na 70 na kuna asilimia 30, wadau hawa wanapita katika njia moja na wanachukua vibali sehemu moja na wakaguzi wa vizuia, wanakagua bila kujua huyu katoka kwenye mashine ya kisasa au mashine ya kizamani. Kwa mpango huo, inamaanisha kwamba kuna mwanya mkubwa sana wa rushwa, kuna mtu atatoka na asilimia 60 na mwingine asilimia 30. Je, sasa Serikali inakuja na mkakati gani uliobora kabisa kuepusha watumishi ambao sio waaminifu kufanya kazi ambayo imenyooka kwa dhamira iliyopo sasa ya Awamu hii ya Tano kwamba tunataka wananchi watendewe haki?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni lini sasa Serikali itaona njia bora zaidi ya kusaidia wadau hawa wajasiriamali, wale ambao wana mashine za kizamani waweze kuwezeshwa na kupata mashine hizi za kisasa ili kuondoa mkanganyiko huu ambao unasababisha mwanya mkubwa wa rushwa?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Omary Massare, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza kwa sababu yeye ni mdau mkubwa sana wa mazao yatokanayo na misitu na kwa kweli amekuwa akifanya kazi nzuri sana na amekuwa mshauri mzuri sana katika masuaa mbalimbali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mkakati ambao Wizara imeweka, Serikali kwa kweli imeweka mkakati mkubwa wa kuhakikisha tunawahamasisha wananchi wote wahakikishe wanapata teknolojia za kisasa, mashine ambazo ni bora kwa sababu hizi mashine zingine kwa kweli zinafanya upotevu mkubwa sana na hasara ni kubwa. Katika suala hilo ndiyo maana tumeweka mkazo kwamba wale wote ambao wanakuwa na zile mashine ambazo zinapoteza sana kwa kweli hawaruhusiwi. Pale ambapo itabainika kwamba baadhi ya watumishi wetu katika maeneo kadhaa wanaruhusu hizo mashine zitumike kwa rushwa basi tunaomba mtusaidie kututajia majina ili hatua kali ziweze kuchukuliwa kwa watumishi wa aina hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu namna ya kuwasaidia Watanzania hawa, kwa kweli ziko njia nyingi za kuwasaidia Watanzania lakini nitumie nafasi hii kuwahamasisha kwamba wajaribu kutafuta mikopo ya aina mbalimbali. Kuna aina nyingi za mikopo sasa hivi, kuna ile mikopo inayotolewa na Halmashauri, kuna mifuko mingi inatoa mikopo basi wachukue mikopo ili waweze kupata mashine ambazo ni bora ambazo zitawafanya wapate mazao mengi zaidi kuliko mashine ambazo ziko hivi sasa. (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:- Mjasiliamali au mtu yeyote anapokata mti anatakiwa achukue 70% ya kile anachokilipia:- • Je, ni lini recovery rate ya 30% ya mbao ilifanyiwa utafiti? • Je, ni taasisi gani ilifanya utafiti huo?

Supplementary Question 2

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kumekuwa na kauli ya Serikali kwamba kila Halmashauri wapande miti 1,500,000 kwa ajili ya kuhifadhi mazingira yetu. Nafahamu Wizara hii, Wizara ya TAMISEMI pamoja na Mazingira wanahusika na hawa wana mbegu za miti mbalimbali. Kwa nini msione umuhimu wa kutoa miti katika Halmashauri zetu hiyo 1,500,000 ili tuipande na kuhifadhi mazingira kwa sababu mkitegemea Halmashauri watoe fedha, wanunue hiyo miti Halmashauri zetu hazina fedha, kwa nini msitupe hiyo miti 1,500,000 tupande?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Pauline Gekul, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa ni sera ya Serikali kuhakikisha kwamba Halmashauri zote nchini zinapanda miti angalau kila Halmashauri 1,500,000 lakini kumekuwa na upungufu wa miche ya kupanda. Hivi sasa kama Serikali tumechukua hatua kwa kutumia Wakala wetu wa Misitu kuhakikisha kwamba wanashirikiana na Halmashauri kwanza kwa kuwapatia mengi lakini katika maeneo mengi kuwapa miche ile ambayo tayari tumeshaiotesha ili kusudi zile Halmashauri ziende kufanya kazi ile ya kupanda katika maeneo mbalimbali. Siyo tu suala la kupanda lakini baada ya kupanda pia Halmashauri zihakikishe kwamba zinailinda ile miti na kuhakikisha kwamba kweli inakua sio tu inapandwa halafu inaachwa.