Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 9 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 119 2018-09-14

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:-
Mjasiliamali au mtu yeyote anapokata mti anatakiwa achukue 70% ya kile anachokilipia:-
• Je, ni lini recovery rate ya 30% ya mbao ilifanyiwa utafiti?
• Je, ni taasisi gani ilifanya utafiti huo?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni Magharibi, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, mauzo ya miti ya Serikali kwa ajili ya kuvuna hufanyika baada ya kufanya tathmini ya ujazo wa miti kwa kupima unene na urefu wa miti inayotarajiwa kuuzwa. Ujazo huu hauhusishi ujazo wa matawi, majani na mizizi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tafiti zilizowahi kufanywa na wataalam wetu wa misitu kati ya mwaka 1996 hadi 1999 wakati wa kutekeleza Mradi wa FRMP (Forest Resource Management Programme), zilibainisha kuwa mteja anaweza kupata mbao kati ya asilimia 60 – 70 ya ujazo wa mti uliopimwa kama atachakata magogo hayo kwa kutumia mashine zenye ufanisi wa kiwango cha juu ambazo ni frame saw au band saw. Mashine hizi hupatikana kwenye viwanda vikubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika viwanda vidogo vidogo na vya kati ambavyo hutumia mashine zenye ubora wa chini kiwango cha uzalishaji ni kati ya asilimia 20 - 43 ambapo wastani ni asilimia 30 ya ujazo wa mti. Utafiti huu ulifanywa kati ya mwaka 2005 na 2007 na wataalam kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) na Chuo cha Viwanda vya Misitu cha Moshi (FITI). Teknolojia duni, uelewa mdogo na usimamizi hafifu ndiyo chanzo cha kuwa na ufanisi huo mdogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuzingatia utafiti huo na ufanisi wa teknolojia iliyopo sasa ya msumeno wa mkono na msumeno wa duara (circular saw) hauwezi kuzalisha mbao zenye ujazo wa zaidi ya asilimia 30 ya ujazo wa mti uliopimwa. Kiwango cha asilimia 30 kitaalam tunakiita recovery rate.