Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:- Je, ni lini Jeshi la Kujenga Taifa litakuja na mkakati wa kuwa na miradi itakayounganishwa na jitihada za vijana wasiokuwa na ajira Wilayani Biharamulo na kwingineko kwa namna isiyohitaji uwekezaji mkubwa wa kujenga Kambi za Kijeshi?

Supplementary Question 1

MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa kuwa Serikali imeonesha nia ya kufanyia kazi wazo hili na kwa kuwa Biharamulo tuko tayari, Mheshimiwa Waziri uko tayari kwa hivi karibuni tuje mimi na Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi kwa ajili ya kuanza mazungumzo na wataalam wako wa Jeshi la Kujenga Taifa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, Mheshimiwa Waziri uko tayari kututembelea ili kabla ya maongezi haya hayajaanza uone fursa zilizopo ili maongezi yawe yamesheheni ushahidi na mambo ambayo tumeyaona kwa pamoja?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kutembelea niko tayari kufanya ziara katika eneo hilo ili kutambua fursa ambazo zinaweza zikashughulikiwa ili kutoa ajira kwa vijana hao.
Kuhusu mazungumzo na wataalamu wake nina shauri nipate fursa kwanza ya kujadiliana suala hili na wataalam wa JKT ili kuona uwezekano wake na watakapokuwa wao tayari kuja basi wenzao hawa wawe tayari kwa ajili ya mazungumzo haya.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:- Je, ni lini Jeshi la Kujenga Taifa litakuja na mkakati wa kuwa na miradi itakayounganishwa na jitihada za vijana wasiokuwa na ajira Wilayani Biharamulo na kwingineko kwa namna isiyohitaji uwekezaji mkubwa wa kujenga Kambi za Kijeshi?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwanza niwapongeze vijana wote wa JKT wanaoendelea kujitolea. Kumekuwa na malalamiko ya kubaguliwa katika upande mzima wa suala la kupewa ajira kwa vijana wanaomaliza JKT hasa ajira ambazo zimetokea kwenye Jeshi la Polisi na hasa katika Operesheni ya Jakaya Kikwete.
Sasa swali langu, nini tamko la Serikali kuhusiana na tabia hii ya kibaguzi, na wapo vijana wa jimboni kwangu?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Ester Bulaya kwa kuamua kwa makusudi kujiunga na Mfunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa akiwa hapa Bungeni, pamoja na Waheshimiwa Wabunge wengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la malalamiko ya ubaguzi wakati wa ajira, nataka nimfahamishe kwamba mara zote kuna kuwa kuna uhaba wa idadi ya vijana wanaoajiriwa ukilinganisha na wale walioko kwenye kambi. Kwa mfano katika kipindi kilichopita jeshi la Ulinzi liliajiri vijana 2,000 kati ya vijana 9,000 waliokuwepo kule; bila shaka wale 7,000 wataona kwamba wamepaguliwa, lakini ukweli ni kwamba nafasi zinakuwa chache wakati wao wako wengi. Ni kweli hivi karibuni Jeshi la Polisi lilitoa ajira, lakini vile vile idadi ya vijana walioajiriwa ni chache sana ukilinganisha na vijana waliokuwepo katika Kambi za JKT.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa wakati mwingine vigezo vya ajira vinaweza vikafanana lakini kwa sababu ya idadi imekuwa ndogo basi kuna wengine bilashaka wataachwa ndiyo hayo yanasababisha malalamiko.

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:- Je, ni lini Jeshi la Kujenga Taifa litakuja na mkakati wa kuwa na miradi itakayounganishwa na jitihada za vijana wasiokuwa na ajira Wilayani Biharamulo na kwingineko kwa namna isiyohitaji uwekezaji mkubwa wa kujenga Kambi za Kijeshi?

Supplementary Question 3

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru; nina swali moja la dogo la nyongeza.
Serikali au JKT inatoa stadi za kazi ikiwemo suala zima la ushonaji; na Serikali kwa mara kadhaa kwa miaka mingi imesema ina mkakati kabambe wa kuongeza viwanda vya ushonaji nguo na hasa sare zile za jeshi, lakini imeonekana kwamba…
: ...inaonekana
kwamba kunakuwepo na kusua sua kwenye shughuli hizi, swali, je, Serikali ina mkakati gani wa ziada kuona kwamba ahadi yake ya muda mrefu ya kuongeza viwanda vya ushonaji nguo sambamba na Tangamsino mbali ya Kamesuma?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba tunao mkakati wa kuongeza idadi ya viwanda vya kuzalisha nguo katika jeshi letu na tunavozungumza tuna viwanda viwili tayari, kimoja kiko pale katika Kambi ya Mgulani na kingine kipo katika Kambi ya Ruvu. Vinafanya kazi na lengo ni kuviboresha kwanza hivi kabla hatujaanzisha vingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo ukifika pale kwenye kambi ya Mgulani utaona kwa macho yako kwamba kwa kweli juhudi kubwa zimefanyika. Sasa hivi nguo za kombati kwa mfano hatuagizi kutoka nje zina vitambaa vinanunuliwa hapa na zinashonwa hapa. Kwa hiyo, tumeanza na juhudi hiyo na hatua kubwa imepigwa na tutaendelea kuendeleza juhudi hizo. (Makofi)