Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 6 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 73 2018-09-11

Name

Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:-
Je, ni lini Jeshi la Kujenga Taifa litakuja na mkakati wa kuwa na miradi itakayounganishwa na jitihada za vijana wasiokuwa na ajira Wilayani Biharamulo na kwingineko kwa namna isiyohitaji uwekezaji mkubwa wa kujenga Kambi za Kijeshi?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Oscar Mukasa, Mbunge wa Biharamulo Magharibi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua hitaji kubwa la kuanzishwa Kambi za JKT kwenye Mikoa na Wilaya ambazo hazina Kambi za JKT ikiwemo Biharamulo. Jeshi la Kujenga Taifa limeeleka nguvu kwenye vikosi vilivyoanzishwa awali na baadaye kusitisha shughuli za kuchukua vijana mwaka 1994. Aidha, JKT inaanzisha kambi mpya katika maeneo mbalimbali kwa awamu kwa kadri bajeti yake itakavyoruhusu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa Jeshi la Kujenga Taifa limejikita katika kutoa mafunzo ya stadi za kazi kwa vijana waliojiunga na JKT kwa kujitolea. Lengo ni kuwa endapo vijana hawa watakosa ajira katika vyombo vya Ulinzi na Usalama waweze kujiajiriwa na taasisi nyingine za Serikali, sekta binafsi au wajiajiri wenyewe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa vijana wanaopata fursa hii ya kujiunga na JKT kwa kujitolea ni wachache kulingana na mahitaji; wazo la Mheshimiwa la kulitaka Jeshi la Kujenga Taifa kuanzisha miradi iliyohitaji uwekezaji mkubwa na kuwashirikisha vijana wasio na ajira katika maeneo mbalimbali yasiyokuwa na kambi za JKT ikiwemo Biharamulo ni wazo zuri ambalo tunalipokea na tunaahidi kulifanyia kazi ili kuona uwezekano wa kulitekeleza.