Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- Nkwenda I ni kata ya kibiashara yenye wakazi wengi, na Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, wakati wa kampeni katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 aliahidi kujenga barabara kwa kiwango cha lami. Je, Serikali haioni ni wakati muafaka kujenga kilometa kadhaa za lami ili kupunguza adha wanazopata wafanyabiashara hao?

Supplementary Question 1

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niweke rekodi sahihi; swali langu halijajibiwa, nimeuliza kilometa tano za lami zilizoahidiwa na Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni katika Kata ya Kyerwa. Hii ni kata ya mjini, ina wafanyabiashara wengi, ina shughuli nyingi za kibiashara lakini watu wanateseka na adha ya vumbi inayosababisha ajali mbalimbali za mabasi, boda boda na magari mengine.
Swali ni lini kilometa tano alizoahidi Mheshimiwa Rais katika Kata ya Nkwenda – kata ya kibiashara – zitajengwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; tumeshuhudia taharuki na bomoa bomoa katika Kata hii ya Nkwenda ambayo hatuoni kama imetengewa bajeti lakini bomoa bomoa na X zinaendelea. Swali, wale wanaowekewa X na kubomolewa nyumba zao watapewa fidia kwa kuwa hakukuwa na ramani ya mpangomji na ramani sasa inawafuata watu wakiwepo pale; watapewa fidia katika maeneo yao ambayo yanakwenda kupitiwa na bomoa bomoa ya ujenzi wa barabara?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimejibu katika majibu yangu ya msingi, unapoanza kujenga kilometa tano ukaanza na kilometa moja tayari ulishaanza ujenzi kuelekea kilometa tano ambazo Mheshimiwa Rais ilikuwa ahadi yake. Kwa hiyo, nimemhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba ahadi ya Mheshimiwa Rais ambayo wajibu wake ni kutekelezwa ndani ya miaka mitano na kuhakikisha kwamba ahadi hizo zinatekelezwa ndiyo maana tunaanza na kilometa moja. Ukijenga kilometa moja katika tano zinakuwa zimebaki kilometa nne.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia anauliza juu ya wananchi kulipwa fidia. Sheria iko wazi, kwa wale wananchi ambao wameifuata barabara ambayo; hatuwezi wakati huo huo tukataka maendeleo na wakati huo huo tukataka tubaki katika hali ile kabla ya maendeleo. Kwa hiyo, kwa wale ambao wameifuata barabara hawatalipwa na wale ambao barabara imewafuata watalipwa kwa mujibu wa sheria.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- Nkwenda I ni kata ya kibiashara yenye wakazi wengi, na Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, wakati wa kampeni katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 aliahidi kujenga barabara kwa kiwango cha lami. Je, Serikali haioni ni wakati muafaka kujenga kilometa kadhaa za lami ili kupunguza adha wanazopata wafanyabiashara hao?

Supplementary Question 2

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona na kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mheshimiwa Rais, mgombea wakati ule 2015 aliahidi Makambako Mjini kutupatia kilometa sita za lami; na kwa kuwa Serikali tayari imeanza kutupatia mita 150 ambazo tayari zimeshajengwa na mkandarasi ameondoka; na tayari tena atakuja kujenga mita 150. Kwa nini sasa mkandarasi huyu amekuwa akija mita 150 gharama itakuwa ni kubwa, kwa nini asianze kujenga kilometa sita zote kwa pamoja ili kukwepesha gharama ya Serikali isiwe kubwa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jah People (Mheshimiwa Deo Sanga), Mbunge wa Makambako, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimejibu katika jibu langu la msingi, ahadi ambazo zilitolewa na Mheshimiwa Rais wakati akiomba kura kwa Watanzania ziko nyingi, na ziko za aina tofautitofauti. Zile ambazo zinahitaji fedha nyingi zinaratibiwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu na zile nyingine ambazo ni idadi ndogo ya kilometa ambazo zinajengwa zinaratibiwa kupitia Ofisi ya Rais, TAMISEMI na ndiyo kama hiyo ya Makambako.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika kwamba kama ilikuwa ni kilometa sita na Mheshimiwa Mbunge anasema kwamba tayari tulishajenga mita 150 na nyingine 150, naomba nimhakikishie kwamba kabla ya miaka mitano kukamilika ahadi ya Mheshimiwa Rais kwa kilometa sita tutakuwa tumekamilisha.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- Nkwenda I ni kata ya kibiashara yenye wakazi wengi, na Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, wakati wa kampeni katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 aliahidi kujenga barabara kwa kiwango cha lami. Je, Serikali haioni ni wakati muafaka kujenga kilometa kadhaa za lami ili kupunguza adha wanazopata wafanyabiashara hao?

Supplementary Question 3

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, huu ni mwaka wangu wa nane nikiuliza swali la ahadi ya viongozi wetu ambao wamefika katika Jimbo la Nyang’hwale.
Mwaka 2010, Rais wa Awamu ya Nne alikuja akaahidi katika kampeni zake barabara ya lami kutoka Kahama – Nyang’olongo – Busolwa – Karumwa hadi Busisi, Sengerema kujengwa kwa kiwango cha lami. Mwaka 2015 pia Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli alikuja akaahidi vilevile.
Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hii ya ujenzi wa barabara ya lami kutoka Kahama – Nyang’hwale mpaka Busisi? (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaendelea kuratibu ahadi za viongozi wakuu, kama Mheshimiwa Mbunge alivyosema. Tayari tunaendelea kufanya uchambuzi ili kuendelea sasa kujenga katika kiwango cha lami. Hata hivyo, kwa barabara hii Mheshimiwa Mbunge anayoitaja kuja Kahama ni barabara ambayo kwenye mpango mkakati tumeiweka. Tuwasiliane tu uone namna tulivyojipanga kwa sababu tunaendelea kupata fedha kidogo kidogo ili uweze kuona na wakati mwingine uweze kuwapa taarifa wananchi wa Nyang’hwale kwamba ni lini sasa ujenzi utakuwa umeanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini zile hatua za awali tumeshaanza, tunatambua umuhimu wa barabara hii kuiunganisha kutoka Sengerema kuja Kahama. Pia wananchi wajue kwamba eneo la jirani kabisa kutoka Kahama Mjini kwenda Geita, Bunge limepitisha fedha za kutosha, tutaanza ujenzi wa barabara hii ya lami. Kwa maana hiyo tunatambua umuhimu wa kutekeleza ahadi za viongozi pamoja na Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge niwahakikishie tu kwamba tunaendelea kuhakikisha kwamba ujenzi wa barabara unafanyika.

Name

Magdalena Hamis Sakaya

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Kaliua

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- Nkwenda I ni kata ya kibiashara yenye wakazi wengi, na Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, wakati wa kampeni katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 aliahidi kujenga barabara kwa kiwango cha lami. Je, Serikali haioni ni wakati muafaka kujenga kilometa kadhaa za lami ili kupunguza adha wanazopata wafanyabiashara hao?

Supplementary Question 4

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nakushukuru sana kwa kuniona; naomba niulize swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kaliua Mjini pale Mheshimiwa Rais aliahidi kilometa tano za lami ndani ya Mji wa Kaliua, na mwaka jana wakati amekuja kwenye ziara yake pia tulimkumbusha akasisitiza kwamba ahadi hiyo itekelezwe kwa wakati. Naomba kujua Serikali itaanza lini utekelezaji wa kilometa tano za lami ndani ya Mji wa Kaliua Center? Ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu katika majibu yangu ya msingi, ahadi zote za viongozi wakuu wa Kitaifa zitatekelezwa. Kwa kuanzia naomba niwaagize TARURA mkoani kwake na hasa Wilaya ya Kaliua wahakikishe kwamba wanatenga katika mwaka wa fedha 2018/2019 ili ahadi ya Mheshimiwa Rais ya Ujenzi wa kilometa tano ianze kutekelezwa mara moja.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- Nkwenda I ni kata ya kibiashara yenye wakazi wengi, na Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, wakati wa kampeni katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 aliahidi kujenga barabara kwa kiwango cha lami. Je, Serikali haioni ni wakati muafaka kujenga kilometa kadhaa za lami ili kupunguza adha wanazopata wafanyabiashara hao?

Supplementary Question 5

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kule Kilolo kuna barabara ambayo inaunganisha na Mkoa wa Morogoro, swali hili nimeshaliuliza zaidi ya mara tatu na ahadi ya Serikali ilikuwepo. Hivi leo ninavyozungumza wananchi wa Kimala, Itonya, Muhanga, Idete na Idunda wanafanya kazi kwa mikono, na mimi kama Mbunge nimechangia na wananchi wengine wamechangia.
Je, sasa Serikali itakuwa tayari na yenyewe kuchangia ili wale wananchi wa Kilolo kwa nguvu zao waweze kupasua barabara kuelekea Morogoro ambako naunganishwa na Jimbo la Mheshimiwa Susan Kiwanga?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZU NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua umuhimu wa kuunganisha Mikoa. Kwa Mkoa wa Iringa tunao mpango wa kuunganisha eneo hili la Kilolo kuja Mkoa wa Morogoro kupitia Mlimba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo nimpongeze tu Mheshimiwa Mwamoto kwa sababu amekuwa mfuatiliaji mzuri na mwenyewe anafahamu hii barabara kutoka Iringa kuja Kilolo na sehemu ambayo ilikuwa inasumbua kwa maana ule mpango wa Halmashauri kufanya marekebisho ya maana alignment ya ile barabara; tumetoa maelekezo ili waweze kurekebisha ili wananchi ambao walikuwa wamepata usumbufu tatizo lao litakuwa limeondoka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nikuhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge hii eneo hili tunalolizungumza ni kilomita chache sana, lakini kwa sababu ya nature ya eneo tunalifanyia kazi ili tuweze kukuunganisha na eneo la Mlimba.