Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 71 2018-09-11

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:-
Nkwenda I ni kata ya kibiashara yenye wakazi wengi, na Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, wakati wa kampeni katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 aliahidi kujenga barabara kwa kiwango cha lami.
Je, Serikali haioni ni wakati muafaka kujenga kilometa kadhaa za lami ili kupunguza adha wanazopata wafanyabiashara hao?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anatropia Lwehikila Theonest, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, aliahidi kujenga barabara yenye urefu wa kilometa tano katika Wilaya ya Kyerwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jitihada za kutekeleza ahadi hii zimekwishaanza na katika mwaka wa fedha 2018/2019, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) imetenga shilingi milioni mia tatu hamsini kwa ajili ya ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa moja kwa kiwango cha lami Makao Makuu ya Wilaya ya Kyerwa (Rubwera). Ujenzi huu unatarajiwa kuanza mwezi Oktoba, 2018. Serikali itaendelea kujenga barabara za lami Wilaya ya Kyerwa kwa awamu ili kutimiza ahadi hiyo ya Mheshimiwa Rais.