Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MGENI JADI KADIKA aliuliza:- Vituo vingi vya Polisi havina miundombinu mizuri na vingine ni vibovu na vichakavu:- Je, ni lini Serikali itakifanyia maboresho Kituo cha Polisi Konde?

Supplementary Question 1

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza bado sijaridhika na majibu aliyotoa kwa sababu hayo ni majibu ya kila siku. Baada ya hapo, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa miundombinu ya Kituo cha Konde ni mibaya sana hasa wakati wa mvua mpaka askari avue viatu ndiyo aweze kuingia kwenye kituo kutokana na maji yanayopita mbele ya kituo. Je, hili nalo linahitaji fedha za bajeti?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, Kituo hicho cha Konde pamoja na nyumba za askari ni mbovu kabisa hazikaliki. Waziri amenijibu kuwa anasubiri fedha ni mwaka gani huo, mwaka huu au miaka kumi ijayo? Nataka kupata jibu. (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba arejee swali la kwanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza halijasikika vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu kwa pamoja maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mgeni Kadika, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo hicho cha Konde ni kweli kinahitaji marekebisho na sisi tuna mpango wa kurekebisha pale ambapo tutakapopata fedha na azma hii ipo palepale. Hata hivyo, Mheshimiwa Mbunge pia ana nafasi kwa yale mambo ambayo yanaonekana kwamba ni ya dharura, ni mambo madogo madogo ambayo Mbunge hayamshindi kama mabati, anaweza akachangia jitihada hizo kurekebisha mambo hayo lakini sisi kwa upande wetu kama Serikali tuna mambo mengi tunafanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala lake la pili kuhusiana na changamoto za nyumba za askari, nadhani Mkoa wa Kaskazini Pemba ni miongoni mwa mikoa ambayo inafaidika na ujenzi wa nyumba za askari takribani nyumba 12 na Mheshimiwa Rais ametoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba nyingine 400 vilevile Mkoa wa Kaskazini Pemba tutajenga. Kwa hiyo, hiyo ni katika jitihada ambazo Serikali tunafanya na vilevile tunapokea msaada kutoka kwa Waheshimiwa Wabunge au wadau wowote katika kusaidia jitihada za Serikali kupunguza changamoto hii kubwa ya vituo vya polisi pamoja na makazi ya askari hapa nchini.

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. MGENI JADI KADIKA aliuliza:- Vituo vingi vya Polisi havina miundombinu mizuri na vingine ni vibovu na vichakavu:- Je, ni lini Serikali itakifanyia maboresho Kituo cha Polisi Konde?

Supplementary Question 2

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Itakumbukwa kwamba kuna vituo vya polisi ambavyo walijenga wakoloni, mkarithi lakini mmeshindwa kuviendeleza. Hivi karibuni kuna vifaa ambavyo mmepeleka Kisiwani Pemba viko Wilaya ya Mkoani.
Swali, je, vifaa hivyo ndiyo vinaenda kujenga Kituo cha Kengeja ambapo ni muda wa miaka 16 unaahidi lakini hutekelezi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Masoud, Mbunge wa Mtambile, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, vifaa ambavyo tumepeleka si kwa ajili ya kujenga Kituo cha Polisi cha Kengeja bali ni kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za Askari Polisi katika Mkoa wa Kusini na Kaskazini Pemba.

Name

Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. MGENI JADI KADIKA aliuliza:- Vituo vingi vya Polisi havina miundombinu mizuri na vingine ni vibovu na vichakavu:- Je, ni lini Serikali itakifanyia maboresho Kituo cha Polisi Konde?

Supplementary Question 3

MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunitendea haki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri atakubaliana na mimi kwamba Jimbo la Konde na Mji wa Konde ndiyo uliokuwa Makao Makuu ya Wilaya kabla ya mabadiliko yaliyofanyika na kupelekwa katika Jimbo la Micheweni lakini haikuondoa uhalisia kwamba Mji wa Konde ndiyo Mji Mkuu katika Wilaya ya Micheweni hilo analielewa. Pamoja na hilo, bado Mahakama ya Wilaya ya Micheweni…
Mheshimiwa Mwenyekiti, bado ipo katika Jimbo la Konde na miundombinu hii miaka yote, Mheshimiwa Waziri jibu lake ni hili kwamba Serikali mpaka ipate pesa ndiyo ifanyie marekebisho. Serikali hii hii...
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini hasa Waziri atachukua juhudi za kufanya marekebisho katika Kituo cha Polisi cha Konde ili askari wetu wapate uhakika wa maisha yao?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Khatib, Mbunge wa Konde, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, jibu linakuwa linafanafana lakini na mabadiliko yanaonekana, maana mwaka jana tulizungumza kwamba tukipata fedha na utaona kwamba mwaka huu tumepata fedha za kurekebisha baadhi ya changamoto hizi za Askari wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusiana na eneo hilo kama ambavyo nimemjibu Mheshimiwa Kadika kwamba dhamira ya Serikali ipo palepale na hatua ambazo tunapiga za kupunguza changamoto hizi nchi nzima, hatua kwa hatua na awamu kwa awamu tunazipokea jitihada za Wabunge ikiwemo hata Mheshimiwa Mbunge kama ataamua Mfuko wake Jimbo atoe kidogo fedha kwa ajili ya kukarabati hicho kituo tutamkaribisha sana.

Name

Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. MGENI JADI KADIKA aliuliza:- Vituo vingi vya Polisi havina miundombinu mizuri na vingine ni vibovu na vichakavu:- Je, ni lini Serikali itakifanyia maboresho Kituo cha Polisi Konde?

Supplementary Question 4

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Wananchi wa Kondoa Mjini walikusanya nguvu sana wakajenga Kituo cha Polisi kidogo pale Mjini Stand. Kituo hiki sasa kina zaidi ya mwaka kimefungwa kutokana na upungufu na ukosefu wa askari. Je, ni lini sasa Serikali itatuletea askari kituo kile kifunguliwe na kifanye kazi iliyokusudiwa? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Edwin Sannda, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ni kweli sababu hasa ni askari peke yake tunatarajia kuajiri askari 1,500 hivi karibuni, tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kutupatia kibali cha kuajiri askari hao, tunaamini kwamba itasaidia kupunguza changamoto ya askari. Nimwombe Mheshimiwa Mbunge, mimi na yeye tupange utaratibu hata weekend moja twende hapo tukaangalie ili kama changamoto tu ni hiyo na kwa sababu tunahamasisha wananchi washiriki ujenzi wa vituo haikubaliki hata siku moja kuona kituo kimekamilika halafu hakitumiki. Mimi nataka nimuahidi kwamba kama itakuwa ni changamoto tu ya askari mimi na yeye tutashirikiana kulikamilisha hilo na tutakizindua kituo hicho ili kiweze kufanya kazi.