Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 39 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 324 2018-05-29

Name

Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MGENI JADI KADIKA aliuliza:-
Vituo vingi vya Polisi havina miundombinu mizuri na vingine ni vibovu na vichakavu:-
Je, ni lini Serikali itakifanyia maboresho Kituo cha Polisi Konde?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mgeni Jadi Kadika, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuwa miundombinu ya Kituo cha Polisi Konde ni mibovu na imechakaa kama ilivyo katika maeneo mengine nchini. Serikali kupitia Jeshi la Polisi itaendelea kufanya ukarabati wa vituo hivyo kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukarabati wa Kituo cha Polisi Konde, utafanyika mara fedha zitakapopatikana ili kuboresha mazingira ya kazi kwa askari wetu na kuwawezesha kutoa huduma bora kwa wananchi.