Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zainabu Nuhu Mwamwindi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINABU N. MWAMWINDI aliuliza:- Shule ya Msingi Kipela, Wilayani ya Iringa, inahudumia wanafunzi wenye mahitaji maalum (albinism) lakini haina miundombinu rafiki, watumishi wa kutosha, huduma za afya stahiki na umeme:- Je, lini Serikali itarekebisha mapungufu hayo?

Supplementary Question 1

MHE. ZAINABU N. MWAMWINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa mahitaji ni walimu 17, kwa sasa wapo walimu 7, je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha ikama ya walimu inakamilika katika Shule ya Msingi Kipela? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, watumishi wasio walimu wapo 7, mahitaji ya shule ile ni watumishi 13. Je, Serikali haioni wakati sasa umefika wa kuhakikisha idadi ya watumishi wasio walimu inakamilika kutokana na uhitaji wa shule? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zainabu Mwamwindi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba uniruhusu nimpongeze Mheshimiwa Mwamwindi kwa jinsi ambavyo amekuwa akiwapigania wananchi wake wa Mkoa wa Iringa katika kuhakikisha kwamba wanapata huduma. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la kutaka kujua Serikali ina mkakati gani, kwanza naomba nitumie fursa hii kuagiza Wakurugenzi wote kwa sababu umeshatoka Waraka kutoka Ofisi ya Rai, TAMISEMI ukiwataka Wakurugenzi wahakikishe kwamba wale walimu ambao wamejifunza elimu maalum wanapelekwa kufundisha katika shule maalum kwa sababu wana ujuzi nao. Kwa hiyo, ndani ya Mkoa wa Iringa na maeneo jirani ni vizuri Wakurugenzi wakahakikisha stock inachukuliwa ili wale walimu wote ambao wana ujuzi maalum waweze kupelekwa kabla huo mkakati wa pili wa ajira haujatekelezwa kama ambavyo nimejibu katika jibu langu la msingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na upungufu wa watumishi ambao siyo wa taaluma ya elimu, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba watumishi hawa wanapatikana kwa mujibu wa ikama lakini pia itategemea bajeti itakavyoruhusu.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINABU N. MWAMWINDI aliuliza:- Shule ya Msingi Kipela, Wilayani ya Iringa, inahudumia wanafunzi wenye mahitaji maalum (albinism) lakini haina miundombinu rafiki, watumishi wa kutosha, huduma za afya stahiki na umeme:- Je, lini Serikali itarekebisha mapungufu hayo?

Supplementary Question 2

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kumekuwa na shida ya walimu wa alama kwa ajili ya wanafunzi viziwi. Je, Serikali inatoa commitment gani kuhakikisha tunapata walimu zaidi kuweza kuwasaidia watu wanaotumia alama katika kujifunza? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu katika jibu langu la msingi hawa walimu ambao wanatumia alama nayo ni elimu maalum. Kwa hiyo, sisi tunalitazama kwa mapana yake yote na ndiyo maana nimesema kwamba katika hao walimu watakaoajiriwa, naamini na hao wanaotumia alama ni miongoni mwa hao wenye uhitaji maalum na watachukuliwa ili kuweza kuhudumia wanafunzi wanaohitaji walimu wenye kutumia alama.