Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 39 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 322 2018-05-29

Name

Zainabu Nuhu Mwamwindi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINABU N. MWAMWINDI aliuliza:-
Shule ya Msingi Kipela, Wilayani ya Iringa, inahudumia wanafunzi wenye mahitaji maalum (albinism) lakini haina miundombinu rafiki, watumishi wa kutosha, huduma za afya stahiki na umeme:-
Je, lini Serikali itarekebisha mapungufu hayo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zainabu Nuru Mwamwindi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Shule ya Msingi Kipela ina jumla ya wanafunzi 701 wakiwemo wanafunzi 93 wenye mahitaji maalum ambao wote wanakaa bweni. Shule hii ina hitaji la walimu wataalam wa elimu maalum 17 ambapo kwa sasa wapo walimu 7 na hitaji la watumishi wasio walimu 13, kwa sasa wapo 7. Vilevile shule hii ina mahitaji ya vyumba vya madarasa 16 kwa sasa vipo 12.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Shule ya Msingi Kipela ipo umbali wa kilometa 8 toka Makao Makuu ya Kata ya Mzihi ambapo ndiko kuliko na umeme wa gridi ya Taifa kwa sababu hiyo, kwa sasa shule hii inatumia umeme wa jua (solar). Aidha, shule inapata huduma za afya kwenye Zahanati ya Kanisa Katoliki iliyopo jirani na shule. Huduma hii, huchangiwa kwa malipo kidogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na miundombinu ya shule hiyo, Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imepeleka jumla ya shilingi milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa bweni rafiki na la kisasa kwa ajili ya wanafunzi hao. Aidha, Serikali kwa kushirikiana na wadau wengine wa elimu itaendelea kuboresha miundombinu hiyo pamoja na shule zingine za aina hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na ajira, Serikali ipo kwenye mchakato wa kuajiri walimu wa shule za msingi 4,785 wakiwemo walimu wa mahitaji maalum. Shule ya Msingi Kipela ni miongoni mwa shule za wanafunzi wenye mahitaji maalum zitakazopangiwa baadhi ya walimu hao.